Yesu ni mwalimu mwema

12:19:00 PM Unknown 0 Comments

 
YESU NI MWALIMU MWEMA.
Tuyatii Maagizo Yake
Kijana mmoja tajiri alimwendea Yesu na kumwita, “mwalimu mwema” naye Yesu akitaka sana kumtukuza Baba wa Mbinguni akasema, “aliye mwema ni mmoja”. Kwa kawaida mtu anapokusifu au anapokupa heshima yako huonesha utii kwa nafasi yako. Katika dunia ya leo tunawasomi wanaoitwa daktari bigwa, Profesa, wako wahandisi hata marubani.
Kuwasifia wataalamu hawa pasipo kutekeleza wanachosema ni sawa na kufukuza upepo, ni kuwavisha kilemba cha ukoka. Kumwita mtu Daktari bingwa hakuleti maana ikiwa akikikushauri jambo lihusulo afya utakataa . Ni heri asiyemwita kwa cheo lakini akafuata maelekezo yake. Vivyo hivyo haileti maana tumwitapo Yesu mwalimu ilhali hatufuati asemalo. Ukimjua Yesu kama mwalimu mwema lazima ukubali kufanya asemalo hata kama kwa akili za kawaida linaonekana ni la ki-puuzi au ni la kuaibisha.
“Ukimjua Yesu kama mwalimu mwema lazima ukubali kufanya asemalo hata kama kwa akili za kawaida linaonekana ni la ki-puuzi au ni la kuaibisha”
“Na tazama, mtu mmoja akamwendea akamwambia, Mwalimu, nitende jambo gani jema, ili nipate uzima wa milele? Akamwambia Kwani kuniuliza habari ya wema? Aliye mwema ni mmoja. Lakini ukitaka kuingia katika uzima, zishike amri. Akamwambia, Zipi? Yesu akasema, Ni hizi, Usiue, Usizini, Usiibe, Usishuhudie uongo, Waheshimu baba yako na mama yako, na, Mpende jirani yako kama nafsi yako. Yule kijana akamwambia, Haya yote nimeyashika; nimepungukiwa na nini tena?  Yesu akamwambia, Ukitaka kuwa mkamilifu, enenda ukauze ulivyo navyo, uwape maskini, nawe utakuwa na hazina mbinguni; kisha njoo unifuate. Yule kijana alipolisikia neno lile, akaenda zake kwa huzuni; kwa sababu alikuwa na mali nyingi.” Mathayo 19:17-22
Licha ya kumwita Yesu mwalimu mwema yaani, “Good Master” lakini kijana hakukubali ushauri wa Yesu. Alipoambiwa auze kila kitu na kuwapa masikini hakukubali. Anajua Yesu ni mwalimu mwema, anajua Yesu ni mtaalamu wa roho, mwili na nafisi za  wanadamu lakini hataki kumtii anachosema. Alijua Yesu ni kila kitu lakini hakutaka kumsikia. Wako wengi wanamwita Yesu Bwana, wengine wanasema, “nakupenda Yesu” lakini hawataki kutii neno lake. Yeye mwenyewe anasema, “mkinipenda mtalishika neno langu”
Naamani Yule Jemedari anafanana na huyu kijana tajiri. Yeye alipokwenda kwa Elisha nabii hakutaka kujichovya mtoni mara saba. Alitaka Elisha amwekee mkono. Mara nyingi tunapokwenda mbele za Mungu tunakosea, tunakwenda kumwagiza badala ya kwenda kumsikiliza. Mungu anaweza asiseme na wewe kwa njozi, wala kwa nabii wala kwa dalili. Lakini kupitia neno lake (Biblia) anasema nasi kila siku. Kila tunaposoma maandiko tunasikia sauti ya Mungu. Biblia ni redio yake, isome na usikilize. Naamani hakutaka kusikia maagizo ya nabii bali alitaka nabii ndiye afuate mawazo na maagizo yake. Lakini Naamani akakasirika, akaondoka, akasema, Tazama, nalidhania, Bila shaka atatoka kwangu, na kusimama, na kuomba kwa jina la Bwana, Mungu wake, na kupitisha mkono wake mahali penye ugonjwa, na kuniponya mimi mwenye ukoma.”2 Wafalme 5:11
Jambo zuri ni kwamba, kijana tajiri alimuuliza Yesu swali ambalo kila mwenye akili timamu anapaswa kujiuliza. Mtu mzima hapaswi kujiuliza maswali ya kisiasi tu, bali anapaswa kujiuliza maswali yahusuyo umilele wake na watoto wake. Kijana akamuuliza Yesu, “nifanye nini ili nirithi uzima wa milele?”. Hakuuliza kwa habari ya Simba na Yanga, wala hakuuliza kwa habari ya CHADEMA na CCM, hakugusa habari za kuoa na kuolewa wala hakuhoji kwa habari ya Manchester United na Arsenal bali alihoji kuhusu uzima wa milele. Kwa hili ninampongeza. Kila mwenye hekima ni lazima ajue atakuwa wapi baada ya kifo. Swali hili linapaswa kutawala akili ya kila mwanadamu. Uzima wa milele! Uzima wa milele! Uzima wa milele!
“Si vibaya kumiliki pesa, lakini ni hatari kama pesa zitatumiliki sisi hata tushindwe kumpa Mungu nafasi ya kwanza””
Yesu akimjibu Yule kijana alimwambia akitaka uzima wa milele azishike amri, wewe na mimi pia tukitaka uzima wa milele ni muhimu tuzishike amri zake Mungu. Si vibaya kumiliki pesa, lakini ni hatari kama pesa zitatumiliki sisi hata tushindwe kumpa Mungu nafasi ya kwanza. Yule kijana aliiona ni heri akose ukamilifu lakini abakie na pesa. Aliona bora akose furaha lakini abakie na pesa. Aliondoka kwa huzuni, watu wengi wana pesa lakini hawana furaha ya kweli, mali zao zimewatenga na ukamilifu.
Uzima wa milele unapatika kwa kumwamini BWANA YESU. Tena kila aliaminiye jina lake anao uzima wa milele. Ukimwamini leo na kuisikia sauti yake utaokoka. Usimwite BWANA kama hutaki kufanya aliyokuamuru yaani, kushika amri zake. 
Siku ya mwisho Yesu atawaita mashahidi wawili, ataliita neno lake na kupima utii wetu kwa neno lake. Agano jipya ni shahidi wa pili na Agano la kale ni shahidi kwanza. Mashahidi hawa wawili watapima utendaji wetu wa neno. Nami nitawaruhusu mashahidi wangu wawili,”Ufunuo 11:3a

0 comments :

Baada ya kulitambua kusudi la kuumbwa kwako

9:23:00 AM Unknown 0 Comments



BAADA YA KULITAMBUA KUSUDI LA KUUMBWA KWAKO
Ukishafikia hatua ya kutambua kusudi la Mungu juu ya maisha yako hatua zifuatazo ni muhimu sana:
  1. Liandike
Ni muhimu sana kila mtu kuandika kusudi lake au maono yake katika aya yenye sentensi chache iwezekanavyo. Hii itakusaidia kulikumbuka daima kila unapoona sentensi hiyo na kukupa nguvu ya kuiendea hadi mwisho [Habakuki2:2—3].
“Ni vizuri kuibandika karatasi hiyo inayoelezea picha ya maono ya maisha yako ya baadae [kwa ufupi], chumbani au mahali popote pa wazi ili kila uisomapo uweze kukumbusha na kukuhamasisha”
Nimewahi kusoma mwandishi mmoja ambaye yeye anashauri sentensi  hizo zisizidi tatu, lakini kwa maoni yangu si mbaya hata zikifika tano. Tazama kusudi la Yohana mbatizaji lilivyo katika sentensi chache.Palitokea mtu, ametumwa kutoka kwa Mungu, jina lake Yohana. Huyo alikuja kwa ushuhuda, ili aishuhudie ile nuru, wote wapate kuamini kwa yeyeYohana 1:6
Ni vizuri kuibandika karatasi hiyo inayoelezea picha ya maono ya maisha yako ya baadae [kwa ufupi], chumbani au mahali popote pa wazi ili kila uisomapo uweze kukumbusha na kukuhamasisha. Kwa mfano zifuatazo ni sentensi ambazo nimeandika ili kuelezea kusudi la kuumbwa kwa watu kadhaa ukianza na mimi:
1.      “My purpose is to you use all I have, to give myself into the preaching of the gospel and inspire others to live for Christ” Alphonce Luhamba’s vision (purpose) statement
2.     “To uplift humanity consciousness through business”
3.     “To inspire and empower people to live their highest vision in context of love and joy”
4.     “To create and inspire one million millionaires who each will donate one million dollar to his or her church charity”
Ni vema kurahisisha kwa kuandika au kuchora alama zenye kuonesha picha ya kusudi la kuumbwa kwako. Mchoro huo au maneno hayo ni lazima yawe yanakuvutia, yaweze kukuhamasisha na kukupa changamoto ya kuyafanyia kazi katika kutimiza kusudi hilo.  [Your Vision or purpose paragraph must challenge your comfort zone.]
Ni vizuri kulisoma kusudi lako kila siku, ni vema kuliacha liimbe kichwani mwako kila dakika. Kama Ilivyokuwa kwa Yohana mbatizaji wewe pia umetumwa na Mungu, na umetoka kwa Mungu. Haupo duniani kitalii, upo kikazi. Muda wote tuwapo duniani tupo safarini kwa kazi maalumu. Badala ya Yohana, waweza kuweka jina lako. Palitokea mtu, ametumwa kutoka kwa Mungu, jina lake.....Yohana 1:6
  1. Achana na utafiti.
Ukishajua kusudi au maono yako haunabudi kuacha kujiuliza uliza maswali mengi. Hakuna haja ya kuogopa. Ni muhimu kudumu katika Neno la Mungu ambalo ndio chakula muhimu kwa kila mbeba maono na makusudi ya Mungu. Kusudi lako litaendana na Neno la Mungu hivyo usiache kulisoma.
“Kuachana na utafiti usio na tija kutakujengea ujasiri na uhakika wa kupata ushindi; na matokeo yake Imani yako kwa Mungu juu ya maono hayo itaongezeka”
Katika kusudi ushindi lazima. Kuachana na utafiti usio na tija kutakujengea ujasiri na uhakika wa kupata ushindi; na matokeo yake Imani yako kwa Mungu juu ya maono hayo itaongezeka. Achana na maswali ya nitaweza au sitaweza, Mungu aliyekuita atakuwezesha. Tunapokuwa katika kusudi la Mungu tuna uhakika na ushindi wala hatubahatishi.
Baada ya kuachana na maswali, unapaswa kubaki na maneno machache tu ya ushindi. “Nitaweza na nitafanya na nitakuwa vile ambavyo Mungu anataka niwe. Unapaswa kusema kama Daudi, Sitakufa mimi bali nitaishi, ili kufanya kazi niliyoitiwa na BWANA.
  1. Litende na kuimaliza kazi kwa gharama yoyote ile.
Kwa sababu ya hofu ya kulipa gharama mara kadhaa utajikuta katika nafasi ambayo ni rahisi kufanya kila kitu isipokuwa kusudi la kuumbwa kwako, hata hivyo unapaswa kulichagua kusudi lako hata kwa mateso. “Chakula change ndicho hiki niyatende mapenzi yake yeye aliyenipeleka, nikaimalize kazi yake…”Yohana4:34. Jim Rohn anaandika, “Kama una nia ya kutaka kufanya jambo, utatafuta njia ili kulifanya; kama huna nia, utatafuta visingizio kwanini hauwezi kufanya” (Tafasiri isiyo rasmi)
Gharama inaweza kubwa lakini ni muhimu kuhakikisha kwamba kusudi linatendeka, maana gharama huakisi uzuri wa taji yako. Gharama inawezakuwa ya juu (steeper) kama vile: Kuacha kazi fulani, kurudi tena shule au kutengwa, kujikatalia mambo ya kidunia, kuonekana mshamba au kukosa muda wa kupumzika. Kusudi la Yesu lilimnyima hata muda wa kulaza ubavu wake. Ili kufanikisha jambo lenye kuleta maana duniani mwenye hekima mmoja anaandika, “Hakikisha kazi inafanyika kwa gharama yoyote”.
  1. Weka na kupanga  mipango
Maono au mipango ni ulinzi wako. Hatuhitaji “body guard” kama Rais, tunahitaji maono ili kutuokoka katika maangamizi. Mipango mizuri ya baadaye ni ulinzi tosha, itakuzuia na itakuruhusu pia. Pasipo maono na mipango dhabiti, watu huacha kujizuia na hivyo huangamia.
Mipango ni njia ya kuiendee hatima yako. Mipango ni hatua kuelekea katika hatima iliyowekwa mbele yako kwa sura ya maono [Mithali 16:9]. Ni vizuri mipango yako ikazingatia muda. Usikubali  kubahatisha au kupangiwa na mtu. Ni vizuri ukaweka mipango dhabiti ili kutekeleza kusudi la Mungu katika maisha yako. Mipango inakufanya uone mbele, inakusaidia usirejee nyuma. Mipango inakupatia nafasi ya kuishi maisha ulikwisha yafikiri. Pasipo mipango au maono watu hurejea nyuma na hivyo huangamia.
“Watu wanaopenda kufuata mkumbo hawapendi kupanga mipango yao wenyewe, wanaridhika kuwa mashabiki wa watu fulani au wa kikundi fulani”
Ukiwaruhusu watu wapange kwa ajili yako watakupangia kijisehemu kidogo; tofauti na wito au uwezo ambao Mungu ameweka ndani.  Mipango ni wajibu wako binafsi usioweza kukaimishwa [delegate] kwa mtu yeyote. Watu wanaopenda kufuata mkumbo hawapendi kupanga mipango yao wenyewe, wanaridhika kuwa mashabiki wa watu fulani au wa kikundi fulani. Usipopanga mipango yako, utaangukia katika mipango ya mtu mwingine; hii haikupi uhakika wa kufikia kilele cha mafanikio yako.  
“Utahitaji kuchochea kipawa chako; na hapa ni muhimu utafute maarifa na ujuzi sahihi ili kukuwezesha kutumia vyema kipawa chako”
  1. Tafuta maarifa
Wakati mwingine kusudi lako linaweza kukuhitaji utafute maarifa na weledi wa juu ili kulitekeleza kwa ufanisi.  Utahitaji kutoka kwenye “kipawa [gift/talent]” mpaka kwenye “ujuzi [Skills]”. Utahitaji kuchochea kipawa chako; na hapa ni muhimu utafute maarifa na ujuzi sahihi ili kukuwezesha kutumia vyema kipawa chako. Waweza kwenda shule ya muziki, au utahitaji kwenda shule ya sheria, au kurudi tena shule hata kama mwanzoni uliishia njiani, waweza kwenda shule ya Biblia ikibidi, waweza kuwa mfuasi wa mtu mwaminifu aliyefanikiwa katika eneo unalotaka kufanikiwa ili kujifunza kutoka kwake [mentorship/coaching].
Watu wengi wenye vipawa hufanana lakini juhudi, ujuzi na maarifa hufanya watofautiane; inawezekana wote ni waimbaji, lakini mmoja anaimba kwa ujuzi [skills] na mwingine hana ujuzi huo. Marafiki sahihi, usomaji wa vitabu na utazamaji wa vipindi vinavyolisha maono yako ni mambo yenye kukupatia msaada na kulifanya kusudi lako litendeke kirahisi, kwa ufanisi na kwa mafanikio makubwa.

0 comments :

Umuhimu wa kutambua kusudi - II

3:43:00 PM Unknown 0 Comments


UMUHIMU WA KUTAMBUA KUSUDI-II
Tofauti kati ya Kusudi (Purpose) na Maono (Vision)

Kusudi maana yake ni sababu iliyofanya au inayofanya kilichopo kiwepo au kitengenezwe jinsi kilivyo (design) ili kutimiza kazi maalumu; katika kufikia malengo yaliyokuwa yamekusudiwa awali kabla ya kitu hicho kuwepo au kutengenezwa.

0 comments :

ULIMWENGU MKAMILIFU

11:24:00 AM Unknown 0 Comments


ULIMWENGU MKAMILIFU
“Imagine a world without a loser, a world without a purposeless person”
Dunia kamilifu inategemea sana ukamilifu wa mwanadamu. Kwa asili mwanadamu ni mkamilifu na mwenyehaki. Hebu jaribu kufikiri kwamba ulimwengu ungekuwa mkamilifu ungependeza namna gani; hata hivyo ukamilifu wake unategemea wanadamu. “Basi ninyi mtakuwa wakamilifu, kama Baba yenu wa mbinguni alivyo mkamilifu.”Mathayo 5:48

0 comments :

Umuhimu wa kutambua kusudi - I

8:33:00 PM Unknown 0 Comments

UMUHIMU WA KUTAMBUA KUSUDI - I
Umezaliwa ili kufanikisha jambo mahususi katika maisha yako. Kuzaliwa kwako ni jibu la Mungu juu ya uhitaji ulipo katika kizazi chako. Kazi kubwa ya kwanza ulionayo ni kutambua jambo hilo ndipo uweze kuishi kwa ufanisi. Tafiti mbali mbali zinaonesha, watu waliofanya mambo makuu duniani, ndani ya mioyo yao walishawishika na ukweli huu, ya kwamba wameumbwa kwa ajili ya kufanikisha jambo fulani mahususi. Jambo hilo ndilo huitwa kusudi la kuzaliwa kwako.

Kusudi maana yake ni sababu iliyofanya au inayofanya kilichopo kiwepo au kitengenezwe jinsi kilivyo ili kutimiza kazi maalumu katika kufikia malengo yaliyokuwa yamekusudiwa awali kabla ya kitu hicho kuwepo au kutengenezwa.  Kutambua sababu ya kuwepo kwako ni jambo la msingi kuliko yote unayoweza kufanya.

Ile kwamba kila kitu kimeumbwa kwa kusudi maalumu haina maana kwamba kila kitu kinaishi kulingana na kusudi hilo la kuwepo kwake. Kumbuka jambo hili: Tumepewa muda wa kuishi; hatujapewa muda wa majaribio ya kuishi. Ni hasara kwa mtu kukutwa na mauti wakati bado yupo kwenye majaribio ya kuishi.

Kwanini kutambua kusudi la Mungu juu ya maisha yako ni jambo muhimu:

  1. Kusudi ndilo linalokupa kujua sababu ya kuumbwa kwako. Ni hasara kwa mtu kufanya kila kitu katika maisha yake isipokuwa kufanya alichokusudiwa kufanya.
  2. Kusudi ndio chanzo cha utoshelevu wa kweli katika maisha ya mtu (sense of fulfillment).
  3. Kusudi hutupa msukumo na ujasiri wa kusonga mbele katika maisha yetu ya kila siku bila ya kukwamisha na changamoto zinazojitokeza.
  4. Kusudi linakupa uhakika juu ya maisha yako ya kesho leo. Na hivyo hukupa msingi imara ya Imani isiyoweza kuyumbishwa na kitu chochote. Kukupa uhakika juu ya mambo yatarajiwayo. [Habakuki 2:3-4]
  5. Mungu hufanya kazi kwa kuliangalia/kuzingatia kusudi lake. [Waefeso 1:11].
  6. Mungu hufanya kazi kwa kuhakikisha kusudi lake linatimia (He is committed to His purposes) Isaya 14:24
  7. Unapotambua kusudi, hofu hutoweka. Unapotambua ulipokusudiwa kwenda inakupa kujua kuwa ulipo sasa ni kwa kitambo tu. When you know where you are going, where you are becomes an adventure.  [Zaburi 23:3-5]

Hizo ni baadhi ya sababu kwanini kutambua kusudi la Mungu katika maisha yetu ni muhimu. Ikiwa Mungu hufanya kazi kwa kuhakikisha kusudi lake linatimia, hii inatupa uhakika na ujasiri wa kutembea katika mafanikio ya kweli siku zote  kwa kuwa Mungu anakuwa upande wetu ili kutufanikisha.

Kabla ya Mungu kukufunulia kusudi lake kwa maisha yako, Hujifunua kwako kwanzo; Hukukutanisha na U-Mungu wake. Ndio maana kumpokea Yesu kama Bwana na Mwokozi wa maisha yako ni Muhimu, si tu kwa ajili ya kwenda Mbinguni lakini pia unapata fursa ya kutambua kusudi la Mungu kwako na kukuwezesha kuishi maisha yenye ufanisi na mafanikio ya kweli.
See you at the top

0 comments :

Acha Kujipima Kimwili

8:28:00 PM Unknown 0 Comments


ACHA KUJIPIMA KIMWILI

Unaweza kuwa na urafiki hai na Yesu na bado ukawa masikini wa mali na fedha wala si ajabu, unaweza kuugua na bado ukawa na urafiki mzuri na Yesu. Lazaro alikuwa masikini na alikuwa mgonjwa lakini bado urafiki wake na Yesu ulikuwa hai. Kamwe vitu na hali ya afya au fedha si jawabu la mwisho la kuonyesha uhusiano wa mtu na Mungu, Yohana 11:2. Pastor Chris Oyakhilome anaandika katika utenzi wake, “jambo muhimu kabisa katika maisha haya si umiliki wa mali, bali ni kugundua kusudi la Mungu na kulitimiza”.  Maisha hayahusu milki za mali, unaweza ukawa unamiliki kila kitu hapa duniani na bado isikufaidie chochote. Yesu Alishasema, “…maana uzima wa mtu haumo katika wingi wa vitu vyake alivyonavyo.” Luka 12:15
Unapompokea Yesu unapokea kwanza mambo ya msingi na ya lazima kama vile: uzima wa milele, Roho wake mwema, imani ya kweli, uponyaji na unafanyika makao yake. Haupokei aina mbalimbali za magari Toyota Carina, Vos wagon wala Isuzu, haya hata yakija huitwa ziada, cha msingi uzima wa milele. Vitu ni vitu na mtu ni mtu. Kamwe uzima wa mtu haumo katika mali au alama za juu katika tasnia fulani, bali umo ndani ya Kristo Yesu. Hata upewe ulimwengu mzima ni bure kabisa kama hautaweza kudumu katika kusudi la Mungu. Nafsi yako haiwezi kununuliwa na jumla ya utajiri wote wa dunia hii. “Kwa kuwa itamfaidia mtu nini kuupata ulimwengu wote, akipata hasara ya nafsi yake?” Marko 8:36

Shabaha ya shetani ni kuwaona watu wakimlaani na kumlaumu Mungu wao, kwani adui anajua wazi Mungu hapendi kulaumiwa. Mafanikio ya kiroho hayapimwi kwa alama za juu darasani, nyumba gari au fedha nyingi. Baraka ni muhimu ila si kipimo sahihi. Kujipima kimwili ni sababu kubwa inayofanya watu wa kiroho wamlaumu Mungu na kujuta.

Ukikwepa kusudi la Mungu baadaye utajiona huna faida, hautaacha kulaumu kwa kuwa mazingira yatakuwa kinyume na wewe. Utaona umekuja duniani kama mtalii tu, wala hakuna ulichokamilisha. Mtu hana faida nje ya wito na kusudi aliloitiwa na Mungu. Maneno ya Solomoni kwamba, “mtu ana faida gani ya kazi yake…” yanafanana na yale ya nabii Malaki, “Mmesema, Kumtumikia Mungu hakuna faida;” haya ni maneno ya watu waliosahau kusudi la Mungu, na kujikuta wakipenda dini, mali, wake zao, serikali, vitu, marafiki au watoto kuliko kusudi la Mungu.

Nilijifunza mahali fulani kwamba watu wa ki-dunia huutafuta mkono wa Mungu (vitu) lakini sisi tunautafuta uso wa Mungu (uwepo). Ukiwa mtu wa kiroho jipime kiroho. Usijipime kwa kuangalia jinsi waovu au wasio mtii Mungu wanavyofanikiwa. Cha msingi angalie kama unalitendea kazi kusudi la Mungu kukuumba wewe.

Ukipenda kujilinganisha na watu na vitu matokeo utakayopata ni kuona utumishi wako hauna faida. Utaona kumtumikia Mungu hakuna faida, na matokeo yake ni kuleta laana katika maisha yako. Mungu anajua kila amtumikiaye anapata faida ndio maana hapendi watu wake waseme hakuna faida katika utumishi.

"Maneno yenu yamekuwa magumu juu yangu, asema Bwana. Lakini ninyi mwasema, Tumesema maneno juu yako kwa namna gani? Mmesema, Kumtumikia Mungu hakuna faida; na, Tumepata faida gani kwa kuyashika maagizo yake, na kwa kwenda kwa huzuni mbele za Bwana wa majeshi? Na sasa twasema ya kwamba wenye kiburi ndio walio heri; naam, watendao uovu ndio wajengwao; naam, wamjaribuo Mungu ndio waponywao.” Malaki 3:13-18

Hatupaswi kujipima kimwili bali na tujipime kiroho kwa kuzingatia kusudi la kuumbwa kwetu. Unaweza ukawa na fedha nyingi, cheo kikubwa, mavazi mazuri na mke mzuri, lakini kama hujatumikia kusudi la Mungu katika hayo basi ulichofanya ni bure tena ni sawa na kufukuza upepo. "Mhubiri asema, Ubatili mtupu, ubatili mtupu, mambo yote ni ubatili. Mtu ana faida gani ya kazi yake yote aifanyayo chini ya jua?” Mhubiri 1:2-3



0 comments :

Chagua Heshima

4:07:00 PM Unknown 0 Comments


CHAGUA HESHIMA

Jitahidi uwe chombo cha dhahabu

Watu wengi wanapata heshima katika jamiii kwa sababu mbalimbali ambazo huhusisha pia mafanikio yao. Lakini si wote wanaoheshimiwa na wanadamu huheshimiwa na Mungu pia. Watu wengi tunapata heshima ya wanadamu huku tukikosa heshima mbele za Mungu. Basi katika nyumba kubwa havimo vyombo vya dhahabu na fedha tu, bali na vya mti, na vya udongo; vingine vina heshima, vingine havina. Basi ikiwa mtu amejitakasa kwa kujitenga na hao, atakuwa chombo cha kupata heshima, kilichosafishwa, kimfaacho Bwana, kimetengenezwa kwa kila kazi iliyo njema.”  2Timotheo 2:20-21
Mungu akikuheshimu atakutumia. Atakutumia kuleta mapinduzi, atakutumia katika vita, atakutumia katika injili, atakutumia katika uamsho, atakutumia katika uimbaji hata katika biashara. Si wote wafanyao hayo hutumiwa na Mungu, ila wako ambao Mungu huwatuma na kuwatumia katika hayo.
Aliwatumia Yefta na Daudi katika vita, alimtumia Yeremia katika unabii, alimtumia Sauli katika ufalme na Musa na Haruni katika Ukuhani. Alimtumia Mariamu katika kumleta mkombozi Yesu na Elizabeth katika kumleta mwijilisti Yohana mbatizaji. Atakutumia pia.
Lakini Mungu ana kanuni moja, anamtaka mtu ajitenge na uovu. Kama unataka heshima mbele zake basi ni lazima ujitenge na ouvu. Ukikimbia dhambi atakuheshimu, ukishinda vishawishi atakuheshimu pia. Heshima si neema, ni jambo la kuamua. Heshima huleta na mafanikio, na mafanikio anayotaka Mungu kuyaona kwetu ni ushindi dhidi ya dhambi.
Katika nyumba kuna vyombo vyenye heshima na visivyo na heshima. Vya dhahabu hupata heshima kubwa kuliko vya udongo na vya mbao au miti. Ni wewe ndiye mwenye jukumu la kuchagua uwe chombo cha dhahabu, chombo cha udongo au cha miti. Njia ni moja kujitenga na uovu. Basi katika nyumba kubwa havimo vyombo vya dhahabu na fedha tu, bali na vya mti, na vya udongo; vingine vina heshima, vingine havina. Basi ikiwa mtu amejitakasa kwa kujitenga na hao, atakuwa chombo cha kupata heshima, kilichosafishwa, kimfaacho Bwana, kimetengenezwa kwa kila kazi iliyo njema.” 2Timotheo 2:21
Mtu aliyejitakasa, anaheshima mbele za Mungu kuliko wapigania uhuru waovu, kuliko mastaa wazinzi, kuliko matajiri watoa kafara, naam kuliko watumishi wa Mungu wasiohubiri kweli ya Kristo ili kujipatia faida.
Tukijitenga na uovu Mungu atatuheshimu. Tutakua lulu kwake na dhahabu. Atatutumia sana kwa ngazi nyingine na kwa viwango vya juu. Kila siku nimekuwa nikimshukuru Mungu kwa kutupa upendeleo wa kuwa watangazaji wa injili. Ndiyo angeweza kuchagua wachina tu kwani wako zaidi ya bilioni moja, akikuchagua amekupendelea. Tafadhali jitakase.
“Oh! Choose to be a gold vessel”

UTAJIRI WETU KATIKA KRISTO YESU-II

8:25:00 PM Unknown 0 Comments


UTAJIRI WETU KATIKA KRISTO YESU-II
Njia kuu ya kutambua mapenzi ya Mungu juu ya maisha yetu, ni kwa kulisoma Neno lake. Neno la Mungu linatupa fursa ya kuyajua mawazo ya Mungu na mipango yake juu yetu katika siku zetu za kukaa hapa duniani. Neno la Mungu ni kama kioo, tunachopaswa kijitizama ili kuona kama maisha yetu yanaendana na mpango wake uliowekwa wazi katika Neno hilo.
Mpenzi naomba ufanikiwe katika mambo yote na kuwa na afya yao, kama vile roho yako ifanikiwavyo”3Yohana1:2
Jambo moja wapo tunalopaswa kutambua ni utajiri wetu tulionao katika Kristo juu ya afya. Ni mpango wa Mungu ulio kamili kwa watu wake kutembea katika afya njema siku zote za maisha yao. Si mapenzi ya Mungu usumbuliwe na magonjwa. Ukombozi wa mwanadamu hakuishia tu katika kukomboa roho yake, bali pia ulihusu ukombozi kwa nafsi, mwili na mazingira yake pia.
“Yeye mwenyewe alizichukua dhambi zetu katika mwili wake juu ya mti….; na kwa kupigwa kwake mliponya
1Petro 2:24
Biblia inasema kwa kupigwa kwake mliponywa, haisemi mtaponywa; hii inatupa kujua kuwa uponyaji wetu umekwisha kutolewa tayari, yaani gharama imekwisha kulipwa, hivyo magonjwa ya aina yoyote ile hayana uhalali wa kuwepo katika maisha yetu. Yesu Kristo alichukua madhaifu yetu [Math 8:17] hakuchukua udhaifu wetu ili aturudishie baada ya muda, alichukua ili kutupa fursa ya kufurahia uzima wa Mungu katika maisha yetu kwani alikufa mara moja na yupo hai kwa ajili yetu.
Ikiwa Yesu allichukua magonjwa na madhaifu yetu, sisi tulioitwa kwa Neema yake tumebakiwa na jambo moja tu nalo ni Afya, mahali ambapo ugonjwa au udhaifu umeondolewa ni jambo moja tu ambalo hubaki kutawala, nalo ni Afya dhabiti. Kumbuka, Yesu hakufa msalabani ili tu aokoe roho zetu, kifo chake kimelipia afya ya miili yetu pia ili ipate kutumika kama Hekalu la Roho wake Mtakatifu kueneza Ufalme wa Mungu hapa duniani. Kuishi bila ya kusumbuliwa na magonjwa au madhaifu katika maisha yetu hapa duniani inawezekana, shetani hakuna anachodai.
Ni kweli shetani ni mungu wa ulimwengu huu [2Kor10:4], lakini Neno la Mungu liko wazo kuwa, wewe si wa ulimwengu huu; hivyo basi shetani hana mamlaka juu yako wala juu ya afya yako. Una uhalali wa kutembea kifua mbele kwa kuwa upo katika ulimwengu ambao Yesu Kristo ndiye Mungu anayetawala, na katika Yeye hakuna magonjwa [Kolosai 1:13].
Kumbuka jambo hili, Ikiwa Yesu Kristo ndiye aliyekuweka huru, hakuna anayeweza kukuweka katika utumwa tena. Ikiwa ni Kristo ndiye aliyekubariki, hakika hakuna anayeweza kukulaani, ikiwa ni Yesu Kristo aliyechukua magonjwa na madhaifu yetu, je ni nani anayeweza kutuzuia kuwa na afya dhabiti? Tukiijua kweli, kweli itatuweka huru na hakuna atakayeweza kuchukua uhuru wetu.
Sawasawa na imani yako unapokea
.
Tunapokosa kujua utajiri tulionao ndani ya Yesu Kristo katika eneo fulani la maisha yetu, tunakuwa watumwa katika eneo hilo. Ndio maana Mungu hulituma Neno lake ili kuokoa. Biblia inasema watu “wanaangamizwa” kwa kukosa maarifa; maana yake ni kwamba “huyo” anayewaangamiza anatumia ujinga [ukosefu wa maarifa] wa hao watu wa Mungu kama mtaji wa kuwaangamizia. Watu wamechukuliwa mateka si kwa sababu ni wanyonge hawana nguvu bali wamechukuliwa mateka kwa sababu ya kukosa maarifa.   
“Kwa sababu hiyo watu wangu wamechukuliwa mateka, kwa kukosa kuwa na maarifa; na watu wao wenye cheo wana njaa, na wengi wao waona kiu sana”
Isaya 5:13
Nabii Isaya anasema, “Ni nani aliyesadiki habari tuliyoileta? Na mkono wa BWANA amefunuliwa nani?... (Isaya 53:1-8)! Mkono wa Mungu hufunuliwa kwake yeye anayesadiki habari iliyotolewa juu ya kile ambacho Mungu amesema. Uweza wa Mungu hufunuliwa na kuwekwa dhahiri kwetu ili kutusaidia na kutuokoa, pale tunapoamini ujumbe wa Neno lake. Mpaka tumejua na kukubali mioyoni mwetu kuwa kazi moja wapo ya msalaba ni kutupatia afya dhabiti, hatutaweza kufurahia afya ya Ki-Mungu katika maisha yetu.
Naye heri aliyesadiki, kwa maaana yatatimizwa aliyoambiwa na Bwana” Luka 1:45
Jambo kubwa ambalo tunataka ulipate siku hii ya leo ni kwamba, Mungu anajali mafanikio ya roho yako, nafsi yako, mwili wako na mambo yako YOTE [3Yoh1:2]. Kwa kifo na ufufuko wake, una uhalali wa kuwa mzima na kuanza kufurahia uponyaji na afya kamili juu ya jambo lolote lililokuwa likikusumbua. Katika Jina la Yesu Kristo, kama ulikuwa mgonjwa uwe mzima, kwa imani pokea Afya tele tangu leo; kwa kuwa Damu ya Yesu imeshakwisha kumwagika, na gharama imeshalipwa kwa ajili yako; Na sasa ni wakati wa kuishi maisha ya Ushindi katika Kristo Yesu kama ulivyokuwa umekusudiwa tangu awali.

Mtizamo wako juu ya changamoto

3:15:00 PM Unknown 0 Comments


MTIZAMO WAKO JUU YA CHANGAMOTO
Jambo kubwa linalokwamisha watu wengi kufikia kilele cha mfanikio katika mambo mengi ni mtizamo wanaokuwa nao hasa wanapokutana na changamoto kadhaa katika maisha yao ili kufikia mafanikio hayo. Hakuna mtu anayeweza kwenda mbali zaidi ya mawazo yake na mtizamo wake [Your attitude determines your altitude].
Watu wa Israeli wakasema, Je! Mmemwona mtu aliyepanda huko? Hakika ametoka ili awatukane Israeli; basi, itakuwa, mtu Yule atakayemwua, mfalme atamtajirisha kwa utajiri mwingi, naye atamwoa binti yake, na kuifanya mbari ya baba yake kuwa huru katika Israeli” 1 Sam 17:25
Kila mtu alimuona Goliath kama kikwazo cha mafanikio katika taifa la Israeli, kwa upande wa Daudi, Goliath alikuwa njia kuelekea na kufikia  maendeleo na mafanikio yake binafsi, mafanikio ya familia yake na taifa kwa ujumla, hakumuona kama kikwazo cha mafanikio bali njia ya mafanikio. 1Sam17:25-26, 48!
Wakati kila mtu alikuwa akiogopa kuingia Kaanani wa kuhofia majitu, Joshua na Caleb waliwaambia wana wa Israeli kuwa hawa ni chakula chetu, na Mungu alimpa kuona mafanikio ya nchi ya Kaanani (Hesabu14:9). Je una mtizamo gani juu ya changamoto iliyoko mbele yako au inayohusu familia au taifa lako? Je unaona ni kikwazo cha mafanikio yako au unaona ni mlango na njia ya kuelekea mafanikio yako.
Unaona nini?
Changamoto katika ulimwengu huu si jambo la kuepukika. Mara nyingi tunapotatua changamoto moja huibuka nyingine; kuna changamoto mbalimbali katika maisha ya mtu.  Wakati mwingine tunapokutana na changamoto mtu huweza kujihisi hana msaada; na tena hakuna namna anavyoweza kutoka salama katika changamoto hiyo. Mtu anapopitia wakati mgumu, huweza kufikiri ndio mwisho wa maisha yake, au mwisho wa ndoto na mipango yake. Ukweli ni kwamba hakuna changamoto itakayo dumu milele, kila jambo ni kwa wakati tu.
Mpaka tumechagua kuona kama Mungu anavyoona, changamoto hazitakuwa njia ya kuelekea mafanikio yetu bali vikwazo. Mpaka tumechagua kuona kama Mungu anavyoona hatutaweza kusema kama Daudi, “Nijapopita katika bonde la uvuli wa mauiti sitaogopa mabaya…!” BWANA alimuuliza Yeremia anaona nini, Yeremia aliona ufito lakini Mungu alilitazama Neno lake alilosema juu ya Yeremia ya kwamba atakuwa kiongozi wa mataifa na hakuna jambo litakaloweza kumzuia kufikia mafanikio hayo. [Yeremia 1:4-12]
“Kama sisi hatuamini,  yeye hudumu wa kuaminiwa. Kwamaana hawezi kujikana mwenyewe”2Timotheo2:13
Hii inatupa kujua kuwa haijalisha ni jambo gani linatokea, endapo mtu atachagua kuamini Neno la Mungu juu ya Maisha yake, hakika litatimizwa. Mungu analo Neno juu ya Afya yako, familia, biashara, ndoa, masomo n.k. Ni jukumu letu kujua Mungu anasema nini katika Neno lake juu ya maisha yetu. Hakuna upande salama isipokuwa upande wa Neno la Mungu. Katika Israeli wafalme walienda vitani baada ya kujua Neno la Bwana linasema nini juu yao kwa wakati wao, Mungu aliposema waende walienda hata walipokuwa wachache kwa kuwa walikuwa na Uhakika ya kuwa Mungu atafanya yale yote aliyoyaahidi.
Daudi akauliza kwa Bwana, akasema, Je! Nikiwafuata jeshi hili, nitawapata? Naye akamjibu, Fuata; kwa kuwa hakika utawapata, nawe hukosi utawapokonya wote. Basi Daudi akaenda…” 1Sam 30:1-9
Uweza wa Mungu unafunuliwa na kuwekwa dhahiri kwetu ili kutusaidi na kutuokoa pale tunapoamini Neno la Kinywa chake. Mt. Luka anaandika, “Heri aliyesadiki, kwa maaana yatatimizwa aliyoambiwa na Bwana”

Si kwa kazi wala si kwa matendo mema

2:28:00 PM Unknown 0 Comments



SI KWA KAZI WALA SI KWA MATENDO MEMA
Tumeokolewa bure

Biblia inanena wazi wazi kwamba, tumeokolewa kwa Neema kwa njia ya imani katika Yesu Kristo. Hakuna kazi inayoweza kutosha kumwokoa mwanadamu isipokuwa kazi ya msalaba tu, ni ile ambayo Kristo aliitenda. Kazi ya msalaba ni kazi timilifu hatuwezi kuchangia kitu. Iliyo kamili haihitaji kusaidiwa, Yesu alishasema imekwisha. Hakuna namna unavyoweza kuikamilisha iliyo kamili badala yake unapaswa kuamini tu. Kwa maana mmeokolewa kwa neema, kwa njia ya imani; ambayo hiyo haikutokana na nafsi zenu, ni kipawa cha Mungu; wala si kwa matendo, mtu awaye yote asije akajisifu.” Waefeso 2:8-9

Ongeza ufanisi ......

11:27:00 AM Unknown 0 Comments



ONGEZA UFANISI WAKO KUPITIA VIPAUMBELE
Uwezo wa mwanadamu unakikomo chake katika kila afanyalo. Ndio maana kuweka vipaumbele ni jambo la msingi. Nguvu za mwanadamu ni kidogo, hawezi kufanya vizuri kila kitu kwa wakati mmoja. Hawezi kuwekeza katika kila mradi. Hawezi kumfikia kila mtu. Kwa kuwa pesa tulizonazo ni kidogo, muda nao hautoshi na watu tulionao wanamajukumu mengi ndio maana tunahitaji kuweka vipaumbele.

Utajiri wetu katika Kristo Yesu

9:19:00 PM Unknown 0 Comments

UTAJIRI WETU KATIKA KRISTO YESU 
(Waefeso1:17-23)

Biblia imeweka wazi kwamba, watu wamjuao Mungu wao watatenda mambo makuu. Ufunguo wa maisha yenye ufanisi upo katika kupata maarifa, ufahamu na kujua hekima ya jinsi itupasavyo kuenenda ili kuishi maisha ya ushindi katika Kristo Yesu. Ili kuona na kuishi ushindi katika maisha yetu ya kila siku itategemea na kiwango cha maarifa na ufahamu wetu juu ya “siri” za ufalme wa Mungu. Hakuna njia ya mkato katika hilo. [Mithali 4:7-9]

Linda Maamuzi yako ...

8:24:00 PM Unknown 0 Comments

LINDA MAAMUZI YAKO, HASA WAKATI UNAPOKUTANA NA CHANGAMOTO
Je baada ya miaka mitano au kumi au baada ya muda kupita kutoka sasa, utajipongeza kwa uamuzi uliochukua au utajilaumu? Utafurahi na kushangilia au utajutia na kutamani kurudi nyuma ili kusahihisha uamuzi uliochukua? Kumbuka kila kitu kipo katika uweza wa mtu mwenyewe na anawajibika kwa matokeo yote ya uchaguzi na uamuzi wake.

Fikra huru kamwe hazifungwi

7:42:00 PM Unknown 0 Comments


FIKRA HURU KAMWE HAZIFUNGWI
Mwili waweza kufungwa lakini fikra huru kamwe hazifungwi. Huwezi kubaki jela kama tayari akili yako iko nje kwenye uhuru. Kuwa na fikra chanya na sahihi ni oparesheni (brain surgery) unayoweza kuifanya mwenyewe. Ili kuwa na fikra chanya hauhitaji kwenda hospitali ya Apollo nchini India au kule John Hopkins Marekani , unahitaji taarifa sahihi tu. Neno la Mungu ambalo ni Habari njema ndio taarifa sahihi. Neno la Mungu ni taa ya miguu yetu, hutupa hekima kuliko watu wa rika letu. 

Pasipo Msongo wa Mawazo II

6:38:00 PM Unknown 0 Comments



PASIPO MSONGO WA MAWAZO II
(STRESS FREE ZONE)
1.    Mpaka lini?
Wabeba maono wengi, watu wenye mipango ya muda mrefu na wenye shabaha za kipekee wanaweza kuwa wahanga wa swali hili. Hili huwakumba wengi ambao wanaona umri unakwenda, wanatamani wasimamishe saa ili watekeleze mpango kazi wao. Wana mipango na mawazo ya kiuchumi na kijamii ambayo wanashuhudia waziwazi  yakipishana na muda. Swali hili huua moyo wa Rick Warren anasema, “Hurry Kills Prayer.” sala na kutangaza maombolezo.

Pasipo Msongo

5:13:00 PM Unknown 0 Comments

PASIPO MSONGO WA MAWAZO - I

[Stress Free Zone]
Katika maisha haya ya sasa watu wengi wanakabiriwa na maswali mengi; na wale wasio na maswali wana majawabu ya uongo yaani, ambayo si sahihi. Lini nitaajiriwa? Lini nitaolewa? Nitavaa nini? Nini itakuwa hatima ya maisha yangu? Ni miongoni mwa maswali tata katika kizazi chetu.
Kwa kuwa ukombozi wa Yesu Kristo unahusisha; mwili nafsi na roho hakuna namna tunavyoweza kuepuka kujibu maswali haya kama viongozi na watumishi katika Kristo. Kwa wanasiasa baadhi ya maswali haya ni mtaji wao wa kuwafikisha katika matarajio yao.

Unayo nafasi

7:34:00 PM Unknown 0 Comments

UNAYO NAFASI YA KUANDIKA HISTORIA YAKO-II
Watu na wafanikiwe kupitia kufanikiwa kwako
Kila mtu ana shauku ya kutaka kujua namna ya kufanikiwa na kumiliki vitu. Vitabu vyenye picha za fedha, majumba na vitu vya thamani huchapishwa, makampuni hufunguliwa na mahubiri hutolewa yakiwa na lengo la kuvutia watu katika kufikia ndoto zao. 

0 comments :

Itifaki ya Upendo

10:24:00 AM Unknown 2 Comments


ITIFAKI YA UPENDO
(Love Protocol)
Mambo mengi katika maisha ya sasa yanazingatia itifaki. Sote tu mashahidi wa jambo hili, mara nyingi katika kutambulisha, ofisini na hata katika ngazi ya familia itifaki huzingatiwa. Jamii nyingi katika chakula ni wazee ambao hutangulia kunawa au kunawishwa mikono yao kwanza kabla ya rika la vijana na watoto. Mahali pengine ni viongozi wa ngazi za juu huwasili mwishoni baada ya kutanguliwa na wale ngazi za chini, na inafahamika wazi kwamba, viongozi wa meza kuu ndiyo hutambulishwa kwanza. Yote hii ni itifaki.
Amri kumi za Mungu zimekaa katika namna au mpangilio wa ki-itifaki. Ukizisoma kwa utulivu utaona kuna itifaki ndani yake. Zinaanza kwa kuonesha kwamba Mungu peke yake ndiye astahiliye kuabudiwa, zinaendelea na umuhimu wa kuheshimu wazazi na kuwapenda, baadaye zinatufunza namna njema ya kukaa na jirani zetu na kuwapenda.
“Alishatoa kila kitu kwa ajili yetu, hivi sasa hakuna kilichosalia mbinguni. Alipomtoa Yesu alitoa kilicho cha thamani kutoka mbinguni”
Leo tunatamani msomaji wetu uijue itifaki ya upendo (love protocol) ambayo ni muhimu katika maisha yetu ya kila siku. Ni rahisi kabisa, itifaki ya upendo inataka aanze Mungu, ufuate wewe, wazazi na baadaye jirani yako. Mpende BWANA Mungu wako, jipende, na mpende jirani yako kama unavyojipenda.  Mathayo 22:37-39
MUNGU; Ni Baba yetu mwema Yeye alitupenda kwanza, alitupenda upeo. Alishatoa kila kitu kwa ajili yetu, hivi sasa hakuna kilichosalia mbinguni. Alipomtoa Yesu alitoa kilicho cha thamani kutoka mbinguni (Warumi 8:32). Mbele za Mungu Baba, Yesu alikuwa ni kila kitu, ni zaidi ya jinsi Ibrahim alivyompenda Isaka. Lakini kwa ajili yako na yangu alimtoa. MUNGU ndiye anayetutunza, asubuhi hutoka kwake; Yeye ndiye aliyetuumba, tena tu kazi ya mikono yake. Hatuna budi kumpenda kuliko yeyote na kupita chochote. Itifaki ya upendo inadai MUNGU kwanza wengine baadaye. Si vema kujipenda zaidi kuliko kumpenda Mungu. Mpe kipaumbele asubuhi, mtukuze jioni, mtafakari usiku. Mzee Yohana anaeleza vizuri katika 1Yohana 4:10-11: “Hili ndilo pendo, si kwamba sisi tulimpenda Mungu, bali kwamba yeye alitupenda sisi, akamtuma Mwanawe kuwa kipatanisho kwa dhambi zetu. Wapenzi ikiwa Mungu alitupenda sisi hivi, imetupasa na sisi kupendana.
“Unatakiwa kujipenda kiasi kwamba ikitokea nafasi ya kuumbwa tena uchague kuwa wewe katika rangi hiyo hiyo na urefu huo huo”
WEWE; Mara nyingi tumewakumbatia wale waliotuumiza na kutitirisha machozi kila uchwao, huko ni kukosa kujipenda; huwezi kumpenda jirani yako kama hujipendi. Huwezi kutoa usichonacho. Katika usanii wa hali ya juu ni pale ambapo asiyejipenda anajaribu kupenda, hahaha ni vituko! Kujichubua ngozi kwa vipodozi (kuji-cream) ni matokeo ya kutojipenda. Mtu anayetamani kwenda ulaya hata kuhatarisha uhai wake utadhani pamekuwa Mbinguni ni matokeo ya kutojipenda, binafsi natamani kwenda mbinguni kazi yangu ikiisha. Mungu ndiye aliyeweka mipaka, anasababu ya kufanya uwepo katika nchi uliyopo. Kutamani kuzaliwa mzungu badala ya Mtanzania au Mwana wa Afrika ni kutojipenda pia. Unatakiwa kujipenda kiasi kwamba ikitokea nafasi ya kuumbwa tena uchague kuwa wewe katika rangi hiyo hiyo na urefu huo huo. Usitamani kuwa fulani bali tamani kuwa wewe ambaye Mungu anataka uwe. Kujipenda ni kujikubali hata kama hujavaa nguo fulani, hujazaliwa familia fulani au hujaenda nchi fulani. Ninajipenda kiasi kwamba hujitoa katika mtoko wa jioni, najifurahia, najisemea mwenyewe na ninajiheshimu kabla mtu mwingine hajaniheshimu. Zingatia itifaki jipende tafadhali! Usipate hadhi au kupanda chati kwa sababu umevaa nguo fulani bali nguo ipate hadhi kwa sababu wewe umeivaa.
WAZAZI; Itifaki inataka tuwapende wazazi wetu. Biblia imewataja moja kwa moja kwamba, tunapaswa kuwaheshimu. Wazazi ni lango la baraka, anaweza asikupe mtaji wa biashara lakini maneno yake tu ni “dili”. Kumbuka Yakobo na Esau, walitaka haki ya mzaliwa wa kwanza ambayo hutolewa kwa maneno tu. Nakumbuka siku moja Baba yangu alinipigia simu akaniambia nitafanikiwa kwani, sijachukua cha mtu na nikaamini nitafanikiwa; Ukiniuliza kwa nini nitakujibu, ‘baba kasema’. Japo nasoma maandiko na najua jinsi Yesu alivyotufanikisha kwa Damu yake lakini sipuuzi Baraka ya wazazi. Mwalimu Mwakasege anaandika, “Ukitaka kujua mchumba wako ataishi muda gani angalia anachowatendea wazazi wake.” Sasa kama unataka kuwa mjane mapema si lazima kujua hili. Usisahau hili, heshima kwa wazazi huamua juu ya urefu wa maisha yako hapa duniani. Wasamehe wakikosa, wasikilize wakikuonya, wasaidie kila upatapo nafasi. Wapende.
“Je uko tayari kuvunja uhusiano wowote unaoharibu itifaki ya upendo katika ngazi ya Muumba wako? Je, unaweza kukaa mbali na huyo mtu anayekuwa chanzo cha kuharibu uhusiano wako na Mungu?”
JIRANI; ujirani si habari ya nyumba au ya kuishi mtaa mmoja. Ujirani ni nafasi ya kusaidia. Kila unapokuwa na nafasi ya kumsaidia mtu unafanyika jirani yake. Safarini kuna majirani, barabarani kuna majirani, ofisini kuna majirani, kanisani kuna watu huhitaji msaada pia. Ni ajabu kama hatutatambua hisia na mahitaji ya watu wengine na tukaendelea kujiita wakristo. Ukianguka barabarani ungependa watu wakutendee nini? Siku yako ya kuzaliwa ungependa watu wafanye nini? Ukiugua ungepende watu wachukue hatua gani?  Ukipata msiba ungependa watu wachukue jukumu gani? Ukishindwa masomo ungependa watu wazungumze maneno gani? Ukigombea nafasi ya uongozi na usiipate au ukakatwa, ungependa watu wanene maneno gani? Yale ambayo ungependa ufanyiwe basi watendee na wengine pia. Maneno ambayo ungependa kusikia, wasikilizishe na wengine pia na huo ndio ujirani.
ANGALIZO; Unajua itifaki inaweza kuvamiwa au kuingiliwa, wengine husahau na hivyo kushindwa kuzingatia itifaki. Mahali ambapo baba na mama wapo usianze kuwatambua mashemeji zako kwanza, mahali ambapo mwenyekiti yupo usianze kumtambua mweka hazini kwanza. Wengine hutambua vitu kabla ya watu na utu, wengine hutambua wapendwa wao kabla ya Mungu. Ibrahimu alikuwa tayari kumpoteza Isaka ilimradi itifaki ya kwamba Mungu ni Mkuu izingatiwe. Biblia inasema kidole chako kikikukosesha ukikate, Je uko tayari kuvunja uhusiano wowote unaoharibu itifaki ya upendo katika ngazi ya Muumba wako? Je, unaweza kukaa mbali na huyo mtu anayekuwa chanzo cha kuharibu uhusiano wako na Mungu?
Kuhani hupenda ibada, mwinjilisti hupenda mahubiri, manabii hupenda unabii; heshima ya nabii ni kutimia kwa unabii wake. Lakini Mungu hupenda watu hatulii hadi aone usalama wa viumbe vyake. Yona alivunja itifaki, alipenda unabii wake kuliko watu. Alisikitika kwa nini Mungu hajawaangamiza watu wa Ninawi kama alivyotabiri. Kwake yeye bora watu wafe ilimradi unabii utimie, kwa Mungu bora unabii ubatilike lakini watu waokolewe. Yona 4:1
Yesu alizungumza kwa habari ya kuhani aliyependa ibada kuliko utu. Alimwacha mgonjwa aliyevamiwa na wevi kwa sababu anawahi ibada, huyu naye hakujua itifaki ya upendo. Mungu kwanza, wewe na jirani ndio mnafuata; Karama na vitu huja baadaye, Haleluyah! Itifaki ya ki-kristo inatutaka tuwapenda adui zetu na tuwatakie mema hili nalo si jambo la kubezwa. Tafadhali itifaki izingatiwe na neno la BWANA lizingatiwe kwa vitendo.
Tukutane katika mbingu mpya na nchi mpya.
Naomba kuwasilisha.

2 comments :

Ogopa Kougopa

10:46:00 AM Unknown 0 Comments


OGOPA KUOGOPA
(FEAR To FEAR)

Kuna nyakati Mtunga zaburi amewahi kusema, “Ee nafsi yangu kwa nini kuinama (kufadhaika/kuogopa)”. Ni wazi hakupendezwa na hofu, wala hali ya kutokujiamini iliyokuwa ndani yake. Moja wapo ya sababu kubwa inayofanya watu wengi kushindwa kufikia kilele cha mafanikio yao ni hofu ya kushindwa. Nashawishika kusema, hofu ya kushindwa imewafanya watu wengi kushindwa kufikia mafanikio yao kuliko kushindwa kwenyewe (Fear of failure has failed a lot of people than failure itself)
“hofu ya kushindwaimewafanya watu wengi kushindwa kufikia mafanikio yao kuliko kushindwa kwenyewe”

Hata watu wakuu walikutana na hofu walipoanza kutekeleza majukumu yao. Tofauti yao na watu wengine, ni kwamba hawakuruhusu mashaka na hofu zao kuwa kubwa kuliko picha ya mafanikio iliyokuwa mbele yao (vision); na hivyo walisonga mbele na kufanya mambo makubwa yaliyopata heshima katika vizazi vyao na vizazi vilivyofuata baada yao.  Walijua kuwa picha ilikuwa ndani yao ni halisi kuliko mazingira ya hofu yaliyokuwa yakiwazunguka kwa wakati huo.
Rick Warren amewahi kuandika, “Kila tunaposhindwa, kuna uongo nyuma tuliouamini” (Behind every self-defeating act is a lie you believe); hii ni kauli yenye kuhekimisha. Hofu ni moja ya uongo, hofu hufanya watu washindwe masomo kabla ya mitihani, hupelekea bondia apigwe nje ya ulingo, hofu huua kabla hata mtu hajafumba macho; hofu humpa mtu talaka kabla ya ndoa.
Kuna usemi usemao, “Njia ya muongo ni fupi.” Hofu ni uongo na hivyo njia yake ni fupi. Tunaweza kuiaibisha hofu na kuikamata katika uongo wake kwa kuyafanya yale yanayotutisha. Watu wakuu waliiaibisha na kuikamata hofu katika uongo wake baada ya kwenda mbele na kufanya walioyaogopa kwa Msaada wa BWANA. Hofu hutoweka tunapofanya tunayoyaogopa.   Oh! Mungu akusaidie kupata hisia za Daudi baada ya kumuua Goliathi. Oh Glory…I can feel it, how beautiful it was, to kill what was scared by the whole Nation.
Kwa sababu ya hofu ya kushindwa wapo waliokufa na biashara, makampuni, huduma, sanaa, miradi na vumbuzi mbalimbali (zilizoishia kuwa mawazo na ndoto tu) walizopewa kwa makusudi ya kuboresha maisha ya watu wengi katika vizazi vyao na kwa ajili ya vizazi vitakavyofuata baada yao. Kila mtu ameumbwa kwa kusudi maalumu, na kila mtu anacho kitu cha kuchangia katika kizazi chake na vizazi baada yake; lakini kwa sababu ya hofu, vitu vingi vimebaki kuwa mawazo na ndoto tu katika mioyo ya watu wengi.

Aliyeahidi ni mwaminifu.

Ili kupata uhakika kama ahadi uliyopewa itatimizwa au haitatimizwa, jambo la kuangalia si uzuri wa ahadi iliyotolewa bali mtu aliyetoa ahadi hiyo. Ahadi inaweza kuwa nzuri lakini aliyetoa asiwe na uwezo wa kutekeleza. Ibrahimu alijua siri hii muhimu; hata alipooneshwa picha, ya kuwa katika yeye mataifa yote watabarikiwa, na mazingira yake hayakuonyesha kama jambo hilo litawezekana jambo moja tu alijua nalo ni kwamba, Aliyeahidi ni mwaminifu hakika atatekeleza alichoahidi. Ukweli huu ulinyima nafasi ya hofu kudhoofisha (paralyse) imani yake.
“Watu wakuu walishinda hofu zao kwa kuwa ndani yao walijua picha walionayo ndani ya mioyo yao ni halisi kuliko mazingira yao na tena imani yao haikuwa kwenye ahadi walizopewa bali imani zao waliziweka kwa Mtoa Ahadi”

Mungu anapokupa wazo ulifanyie kazi au maono (vision), mara nyingi mazingira yako hayatalingana na maono hayo. Hofu huwa kubwa pale tunapoacha kuangali ahadi ya Mungu na picha iliyowekwa mbele yetu na kuanza kuangalia mazingira au hali zinazotuzunguka kwa wakati huo. Watu wakuu walishinda hofu zao kwa kuwa ndani yao walijua picha walionayo ndani ya mioyo yao ni halisi kuliko mazingira yao na tena imani yao haikuwa kwenye ahadi walizopewa bali imani zao waliziweka kwa Mtoa Ahadi.
“Lakini akiiona ahadi ya Mungu hakusita kwa kutoamini, bali alitiwa nguvu katika imani,Akimtukuza Mungu. Huku akijua hakika ya kuwa Mungu aweza kufanya yale aliyoahidi” Warumi 4:20-21 (msisitizo umeongezwa)
Vita kubwa ya adui ni kutushawishi tusiamini na tutilie mashaka (doubt) juu ya kile ambacho Mungu amesema katika Neno lake kuhusu maisha yetu; kuamini kuwa unao uwezo ambao Mungu amesema unao; ya kuwa unaweza kufanya mambo ambayo Mungu amesema unaweza kufanya; unaweza kupata mambo ambayo Mungu amesema utapata amba kuwa Mungu anaweza kufanya yale aliyoahidi.
Kukosekana kwa imani huipa hofu nafasi ya kukua, kuongezeka kwa mizizi yake ndani yetu, hata kuwa mikubwa kiasi cha kutuzuia kufikia matarajio na mipango yetu ya kila siku; Pale tunapoanza kuamini uongo tu; ndipo uongo huo huanza kuwa dhahiri (manifested) katika maisha yetu (Ayubu3:25-26). Muamini Mungu, kuwa anaweza kutekeleza kile alichosema, na hakika atatekeleza kwa maana Yeye ni Kweli hakuna uongo katika maneno yake! Mtu mmoja amewahi kusema, “Usitie shaka kumuamini Mungu anayejulikana; kwa ajili ya mambo yasiyojulikana”

Tujifunze kwa Joshua na Kalebu.

Kuujua ukweli huu utakupa fursa ya kuishi maisha yenye ujasiri utakao itupa mbali hofu yako. Neno la Mungu na maono (vision) uliyonayo yanakupa uhakika na ujasiri kwamba, haijalishi mazingira uliyopo sasa, jambo hilo au mazingira hayo ni kwa muda tu kwa kuwa Aliyeahidi hakika atatimiza alichoahidi. Kama mazingira uliyopo hayafanani na picha ya mafanikio iliyopo ndani yako, usitie shaka upo hapo kwa muda tu.
Kama ndani yako unaona picha (vision) unamiliki kampuni yako mwenye yenye lengo la kuboresha maisha ya wengi na kumletea Mungu utukufu, basi mazingira yako ya sasa kwamba umeajiriwa au huna hata ajira yasikutie hofu ya kutokufikia picha hiyo. Kile usichokuwa nacho leo utakuwa nacho kesho, endapo tu utasonga mbele kuelekea picha hiyo bila ya kusikiliza kelele zinazopigwa na hofu.
“Wakati wewe unaogopa kufanya upendalo ili kutimiza ndoto zako, wenzako wanaogopa kuogopa na hivyo wanafanya”
Wewe pia ukimhesabu Mungu kuwa mwaminifu utashinda, hauna sababu ya kuogopa, kama iko sababu ambai ya kuogopa hofu yako (to fear your fear). Wakati wewe unaogopa kufanya upendalo ili kutimiza ndoto zako, wenzako wanaogopa kuogopa na hivyo wanafanya. Sababu moja wapo inayofanya tumwite Mungu katika sala ni ili kuondoa hofu zetu, tunapoomba tunakuwa jasiri kama amba na hapo tunafanya hata kupita tuwazavyo. Daudi anasema, “Nalimtafuta BWANA akanijibu, Akaniponya na hofu zangu zote” Zaburi 34:4!
Hiki ndicho kilichowapa nguvu Joshua na Kalebu, waiijua ahadi ya Mungu; ndani yao walikuwa na picha ya nchi mpya baada ya kuishi katika utumwa kwa muda mrefu. Neno la Mungu na picha ya maono waliyokuwa nayo, iliwapa ujasiri wa kusonga mbele hata pale walipokuta na mazingira ya kuwatia hofu. Kila walipokutana na changamoto katika kufikia kilele cha mafanikio yao jambo moja walizingatia, nalo ni kwamba, aliyeahidi ni Mwaminifu na Hakika Atatimiza Alichoahidi. (Hesabu 13:30-31, 14:24)
See you at the top…!

0 comments :