Rafiki yako ni nani?

4:04:00 PM Unknown 0 Comments

RAFIKI YAKO NI NANI?
[Aina ya marafiki ni dalili ya hatima yako] 
Rafiki ni mtu ambaye mna vitu au mwelekeo unaofanana. Rafiki ni Yule ambaye mna mwelekeo wa pamoja katika imani, biashara au kazi. Rafiki ni yule umpendaye na ungependa kuwa na muda mwingi pamoja naye.
Unaweza kufanya urafiki na mtu, na cheo chake, na kitu au vitu. Urafiki na Kaizari ni urafiki na cheo ili upate manufaa  fulani, urafiki wa Yesu na Lazaro ni mfano wa urafiki kati ya watu na upendo kati ya Yuda Iskariote na pesa ni mfano wa watu ambao wako tayari kuwa peke yao ilmradi wawe na pesa.
Kuna nyimbo rafiki tunazozipenda ambazo mara nyingi tunazisikiliza, halikadhalika kuna video rafiki, kipindi cha televisheni rafiki na hata kaseti ya redio rafiki. Tuna kitabu rafiki tena kuna majarida na magazeti rafiki. Ukifanya urafiki na mpumbavu lazima uumie, nyimbo za kipumbavu zinaumiza mioyo, zinaondoa usafi wa moyo kwakuleta mawazo machafu. Biblia inasema, “Enenda pamoja na wenye hekima, nawe utakuwa na hekima; Bali rafiki wa wapumbavu ataumia.” Mithali 13:20
Kuna nyimbo za kipumbavu ambazo ukifanyo nazo urafiki lazima uumie, kuna video za kipumbavu, kuna vipindi vya redio vya kipumbavu halikadhalika kuna majarida na vitabu vya kipumbavu. Kuna magazeti ya kipumbavu [udaku] rafiki wa hayo lazima aumie. Moyo wake hautakuwa safi, utawaza uchafu wa picha ya mbele ya magazeti hayo. Msisitizo wangu uko hapa: Bali rafiki wa wapumbavu ataumia.” Mithali 13:20b
Nimejikataza kuendelea kuitazama vitu kwenye “you tube” kwani picha za matangazo na picha chafu zinazowekwa makusudi zimekuwa kama mtego kwangu. Kuliko kumkosea Mungu kila siku ni bora nisiingie kabisa. Kila mtu ana eneo lake analojaribiwa kwalo, wengine ni urafiki na magazeti, wengine mitandaoni, wengine mavazi na wengine mazungumzo mabaya. Wengine hujaribiwa kwa kutaka kuvutia au kupendwa na watu, hawa huweka picha za mtego wakitegemea aonaye awape, “like” au awakubali.
Rafiki ni yule anayezungumza nawe, magazeti, vitabu, majarida na picha huzungumza nasi. Lengo la mwandishi ni kuona msomajia ua mtazamaji anapata ujumbe kusudiwa. Mara nyingi huwa sitazami wala kusikia nyimbo za kidunia [kipumbavu] lakini huwa inanilazimu nikiwa safarini. Nyimbo hizo hupigwa ndani ya basi na madhara yake ni hasi. Huwa nasafiri nikiwa na vitabu na majarida mazuri ya kusoma lakini bado kwa masaa kumi na nne au kumi ya safari nyimbo za kipumbavu huleta kero na uchafuzi wa moyo. Kama watu watapata ajali huku wakitazama nyimbo chafu basi mioyo yao itakuwa katika hali mbaya.
Tunaweza kujaribiwa kwa kuwa na makundi yenye mazungumzo mabaya lakini kwa kuwa na tabia ya kuchagua vitu vinachochea tamaa mbaya. Ni muda mzuri leo wa kuamua kuacha kabisa urafiki na kipindi kichafu cha redio au televisheni, ni muda mzuri wa kuvunja urafiki mbaya. Rafiki mpumbavu atafanya uangamie, napenda tafsiri hii: “The companion of fools will suffer harm
Mfano mzuri wa madhara yanayompata rafiki wa mpumbavu ni yale ya nchi ya Japani iliyoyapata kutoka Marekani kufuatia urafiki wao na Hiltrer wa Ujerumani. Japani walifanya urafiki na Ujerumani kwa kusaini mkataba wa ulinzi na usalama wa mwaka 1940 matokeo yake mbeleni walivamia kisiwa kimoja nchini marekani na kuambulia kupigwa mabomu ambayo mpaka sasa wanayaonja madhara yake. Yote hayo ni kwa sababu ya rafiki mpumbavu. Nakushauri achana naye na kesho yako itakuwa njema.

0 comments :