Umuhimu wa kutambua kusudi - II

3:43:00 PM Unknown 0 Comments


UMUHIMU WA KUTAMBUA KUSUDI-II
Tofauti kati ya Kusudi (Purpose) na Maono (Vision)

Kusudi maana yake ni sababu iliyofanya au inayofanya kilichopo kiwepo au kitengenezwe jinsi kilivyo (design) ili kutimiza kazi maalumu; katika kufikia malengo yaliyokuwa yamekusudiwa awali kabla ya kitu hicho kuwepo au kutengenezwa.

Kusudi ni kongwe kuliko mtu au kitu husika. Kusudi huishi moyoni mwa msanii au muumbaji kwa muda mrefu. Mtu hapangi kusudi lake kwa kuwa halitoki akilini mwa mtu, bali hutoka moyoni mwa Mungu muumbaji. Haulichagui bali unaweza kuligundua. Lipo kabla ya mtu, ni kazi ya mtu kulijua. Mark Twain mshairi mwenye alama ya aina yake ulimwenguni amewahi kusema kwamba, “Siku mbili muhimu kwa mtu ni siku aliyozaliwa na siku aliyogundua kwa nini amezaliwa.”
Neno maono linawezakuwa na tafasiri nyingi; lakini kwa makusudi ya somo hili, Maono maana yake ni picha ya kusudi inayowekwa wazi/kufunuliwa (revealed) ndani ya moyo wa mtu. Kusudi la kitu/mtu linapojulikana na mtu huyo ndipo huitwa maono. True vision is born when purpose is known.
Kusudi linaonesha sababu ya kuwepo kitu; Na kusudi hilo linapojulikana au kuwekwa wazi ndipo huitwa maono. Hivyo basi, Maono ni kusudi lililowekwa wazi na kujulikana ndani ya moyo [mind] wa mtu.
Kusudi huonesha hali ya mwisho wa jambo/kitu/mtu, jinsi anavyotakiwa au anavyopaswa [kusudiwa] kuwa kulingana na malengo ya aliyefanya jambo hilo au kitu hicho kuwepo. Maono huonesha picha hiyo ya mwishoni mwanzoni; maono huonesha picha ya kusudi iliyo mbele mwanzoni ili mtu apate kuiendea kwa ujasiri na kuwa na uhakika wa kuifikia picha hiyo kwa maana ni Mungu ameadhimia iwe hivyo. Inakupa kujua mwisho wa safari kabla ya kuanza safari. [Isaya 46:9-11]
Kusudi la kitu/mtu huwepo kabla ya kuumbwa kwa mtu; kusudi hilo hufunuliwa na kuwa maono [ndoto, njozi] kwa msaada wa Roho Mtakatifu [Yoeli 2:28]. Bila ya Roho Mtakatifu kututambulisha kusudi la Mungu, maisha hujawa na majaribio. Maono ni tunda la mahusiano na Mungu, kwa kadiri unavyohusiana naye ndivyo anavyozidi kukufunulia na kukuonesha maono yako hatua kwa hatua. [Mwanzo37:5-11]
Kusudi halihitaji umjue Mungu; ile kwamba umeumbwa tu lenyewe lipo, hata kama humjui Mungu na hutaki kumjua. Wengi wamekufa pasipo kuona maono kuhusu maisha yao yaani, pasipo kujua wameumbwa na kuletwa duniani kwa kusudi gani. Maono ya kweli yanahitaji uwepo wa Mungu katika Roho Mtakatifu ili kukuwezesha kuyajua. [1Kor 2:11-12]
Mfano mzuri ni Mtume Paulo, katika Galatia 1:13-16 na Matendo ya Mitume 9:6, 15-18. Kumjua YESU kama Bwana Na Mwokozi wa maisha yako, hakukupi tu uhakika wa maisha yako bada ya kufa, lakini pia unapata fursa ya kuishi maisha yenye ufanisi na kuleta maana hapa duniani.
See you at the top

0 comments :