Enendeni mkabadilishe .....

3:18:00 PM Unknown 0 Comments


ENENDENI MKABADILISHE UTAMADUNI WAO
(Mbingu duniani)
 “Akawaambia, Enendeni ulimwenguni mwote, mkaihubiri Injili kwa kila kiumbe.” Marko 16:15
Wakristo wa sasa wanaogopa ulimwengu na mifumuo yake, ilhali BWANA ameagiza akisema enendeni ulimwenguni kote. Kanisa linalopatikana ulimwenguni ndilo kanisa lenye bidii. Kanisa lazima lipenyeze katikati ya mifumo ya kifedha, utawala, ulinzi, elimu, habari, sayansi, bunge na tasnia nyingine zote.
Kanisa limeokolewa ili likaokoe, ‘she was delivered to deliver’, wakristo hawapaswi kujifungia ndani bali wanapaswa kuonekana mitaani, misibani, redioni, magazetini, mashuleni, vyuoni na katika maeneo ya kazi wakimshuhudia Yesu kwamba, ni Kristo.
Jijini Dar-es-Salaam maeneo ya Tegeta kwa ndevu kuna mkusanyiko wa watu na pembezoni mwa ile barabara liko kanisa moja. Jioni watu wa kanisa lile hutoka nje na kuanza kuhubiri, na kwa kuwa kanisa lao liko karibu na soko na maduka injili yao husikiwa na wengi. Mkao wa lile kanisa [ingawa liko katika hifadhi ya barabara] unatufundisha sisi sote kama wanakanisa namna tunavyotakiwa kukaa kiroho kwa ushuhuda katikati ya jamii zetu. Kanisa halina tofauti na wamachinga katika kuenenda kwake kiroho lisikubali kwenda pasipokuwa na watu.
John Wesley ni moja ya wahubiri wa injili na wahudumu waliofanya kazi kubwa katika kumtangaza Yesu Kristo. Moja ya kauli zake alisema, “Naona Dunia yote kama parokia yangu.” Alikua na kiu ya kuinjilisha iliyomfanya asione mipaka iliyopo ulimwenguni. Unapotazama dunia kama parokia yako maana yake unajipa wajibu mkubwa wa kuwahudumia na kuwalisha kondoo wa BWANA. Cha kushangaza ni kwamba, wakati Wesley anapanga kuinjilisha dunia yote wengi hawana mpango wa kuinjilisha hata familia zao. Hawataki kujisumbua kupeleka ujumbe katika kijiji chao, shuleni aliposoma au katika jumuiya anayosali.
Yesu aliposema twende ulimwenguni alitaka utamaduni wa mbinguni uje duniani (Heaven on Earth). Agizo lake lililenga mapinduzi ya utamaduni. Alitaka wakristo waende katika sehemu tisa muhimu kwa kila taifa na kuweka sura ya injili katika nyanja hizo zote.
Kila taifa lina vitu (componentxs) vifuatavyo ambavyo ni kazi yetu kupeleka nuru katika maeneo haya:
  1. Familia -Ndiyo msingi wa kila jamii na taifa na ni mahali ambapo tunu huzaliwa. Utamaduni wa ki-kristo unapaswa uanzie hapa.
  2. Habari na mawasiliano - kazi yao ni kutangaza na kukuza tunu zilizokubaliwa na jamii ambayo msingi wake ni familia. Wakristo ni lazima wamiliki vyombo vya habari ama wawe watangazaji ili watangaze tunu za Kimungu. Kilichopo sasa ni vikaptura na miziki ya hovyo.
  3. Elimu - Hurithisha tunu na maarifa yaliyokubaliwa na jamii hiyo kutoka kizazi hadi kizazi. Mchungaji Oyadepo na Mesa Otabil wamefanya vizuri kwa kufungua vyuo vikuu ili maadili ya kikristo yajulikane kwa wanafunzi.
  4. Ulinzi na Usalama -Hulinda taifa na mifumo yake, mara nyingine majeshi yamewasaidia waovu kumiliki na kutawala. Ni kutokana na watu wa Mungu kutokuwepo katika nyanja hiyo.
  5. Dini - Kila taifa linafanya ibada. Wakristo wanamwakilisha Mungu wa kweli katika mataifa yao hivyo ni lazima Mungu wetu aheshimiwe kupitia sisi kama nyakati za Eliya. Gidioni alivunja sanamu za baba yake na Nabii Eliya aliwachinja manabii wa baali na baali hakuweza kuwatetea. Mungu wetu ni Mkuu kupita miungu yote.
  6. Bunge - Si tu kwamba bunge hutunga sheria bali wabunge pia hutunga yale wanayopendeza mbele za Mungu wao. Mfano mzuri ni suala la mahakama ya kadhi nchini Tanzania, kama idadi ya wabunge wakristo ingekuwa ndogo leo tungeongea lugha nyingine. Kuna umuhimu wa wakristo kuwa wabunge.
  7. Mahakama - Huhusika na utoaji wa haki. Katika ulimwengu huu wenye vitisho, rushwa na uchawi ni watoto wa Mungu tu ndio huweza kusimamia haki. Wana sheria wadhalximu ni wengi, vijana tusome sheria tukamtetee Yesu kisheria na kuwapa watu haki zao bila ya kuwabagua.
  8. Kazi na Biashara - Ndiyo siri ya utajiri ilipo. Watu hawaheshimiwi kwa upako tu, bali kazi pia huleta heshima. Hekima ya masikini hudharauliwa, wakristo wafanye kazi (halali); wawe matajiri, wakitumia mali zao kusukuma gurudumu la injili. Luka 8:3
  9. Sayansi na Teknolojia - Ndiyo uwanja au jukwaa la kisasa. Zamani tulikutana uwanjani leo hii mamilioni ya watu wanakutana katika mitandao ya kijamii. Huwezi kuinjilisha kwa ufanisi wa juu kabisa ikiwa unachukia facebook na twitter. Kanisa linatakiwa liende ulimwengu uliko, leo hii vijana wengi wako mixtandaoni, kanisa halinabudi kuwafuata huko na kuwasaidia. Kanisa linapaswa liwe la kisasa ili liwainjilishe watu wa sasa kwa njia za sasa.  
WITO:
Wakristo wakikaa katika Nyanja hizo tisa utamaduni wa dunia hii utapotea na ule wa mbinguni utachukua nafasi. Ukiwa ni mkristo na uko katika vyombo hivi ujue cha kwanza kwako si mshahara bali ni ufalme wa Mungu na haki yake. Wakristo mjitokeze katika kuanzisha na kumiliki vyuo vya elimu na vyombo vya habari.
Life Minus Regret team inakutakia mwaka wenye Baraka zote kutoka kwa BWANA 2017.

0 comments :

Tunaishi mara moja tu!

12:10:00 PM Unknown 0 Comments


TUNAISHI MARA MOJA TU.
(Tumia vizuri awamu yako ya maisha)
“tena alikufa kwa ajili ya wote, ili walio hai wasiwe hai tena kwa ajili ya nafsi zao wenyewe, bali kwa ajili yake yeye aliyekufa akafufuka kwa ajili yao.” 2 Kor 5:14
Tungelikuwa tunaishi mara mbili angalau mtu angeweza kutumia awamu ya kwanza kuishi kwa ajili yake mwenyewe na awamu ya pili kuishi kwa ajili ya Yesu Kristo. Kizuri zaidi ni kwamba, tunaishi mara moja, hakuna mtu mwenye awamu mbili za maisha. We live only once!
Katika kuishi kwetu mara moja ni lazima mtu aamue kuishi kwa ajili yake mwenyewe au kuishi kwa ajili ya Kristo. Wewe unaishi kwa ajili ya nani? Wako wanaoishi kwa ajili ya kazi zao, wako wanaoishi kwa ajili ya michezo, wako wanaoishi kwa ajili ya burudani na wako wenye hekima wachache wanaoishi kwa ajili ya Kristo.
Oswald J Smith mwandishi wa kitabu nilicho kisoma na kukirudia zaidi ya mara mbili, “The Consuming Fire” anasema, “I have only one life to live and I want to invest it for Thee” kwa tafsiri yangu, “Nina maisha haya tu, ninataka niwekeze kwa ajili yako BWANA”
Katika mstari unaotuongoza pale juu 2 Kor 5:14 Paulo Mtume anasema wazi Yesu anatutaka tusiishi kwa ajili ya nafsi zetu wenyewe bali kwa ajili yake. Jiulize, unaishi kwa ajili ya Kristo au kwa ajili yako mwenyewe?
Asubuhi mpaka jioni unafanya nini? Wanaoishi kwa ajili ya Kristo huomba kwa saa moja na kusoma neno kwa angalau saa moja. Pesa zako zinatumikaje? Wanaoishi kwa ajili ya Kristo hutumia pesa zao kwa uinjilishaji. Luka 8:3
Nakualika ujitoe kwa Yesu na kuishi kwa ajili yake kuanzia leo: Sema sala hii, “Ee BWANA YESU mimi ni mwenye dhambi na wewe ni mwokozi wangu. Naomba unisaidie kuanzia leo niyatoe maisha yangu kwako, wala nisiishi tena kwa ajili yangu na kwa ajili ya Dunia badala yake nikufuate wewe milele. Amina.”
Nakutakia msimu mwema wa sikukuu, Shalomu….
>

0 comments :

Uaminifu! Tabia gani bora kama hii?

11:37:00 AM Unknown 0 Comments


UAMINIFU! TABIA GANI BORA KAMA HII?
(Si vema kufanana na watu wa dunia hii)

Ilikuwa mchana wakati wa chakula na nilikuwa nikibadilishana mawazo na wafanyakazi wenzangu kutoka taasisi mbalimbali za Serikali. Mkononi mwangu kama ilivyoada nilikuwa na kitabu kizuri, “Money won’t Make You Rich” kilichoandikwa na mchungaji Sunday Adelaja.
Na mara rafiki mmoja akaniambia nimweleze kanuni za kumsaidia kufanikiwa kiuchumi, na mimi kwa haraka kama daktari fedha vile nikaanza kumweleza. Kanuni zote nilizomweleza zilikuwa zikikubaliana na neno Mungu. Mwishowe akazikataa kanuni zangu na akazitaja za kwake za kufanikiwa haraka ambazo ni, kuuza dawa za kulevya, meno ya tembo na ufisadi. Akasisitiza bila magendo huwezi kuwa tajiri.
Ndivyo walivyo watu wa ulimwengu, wanadai bila kuiba hakuna mafanikio, bila uasherati kabla ya ndoa hakuna ndoa wanasisitiza bila uchafu hakuna usafi. Ibrahimu, Ayubu na Daudi wote walikuwa matajiri katika Biblia na maandiko hayatuoneshi wizi au udanganyifu katika maisha yao, badala yake neno la Mungu linaonesha jinsi walivyokuwa waaminifu.
Mali ya mtu au ya serikali ni kipimo chako cha kuona kama unaweza kuaminiwa na kupewa mali yako mwenyewe. Siku za karibuni nimekuwa katika nafasi mbalimbali za kijamii na kikazi zinazoniwezesha kushika pesa za watu na za Serikali. Na kwa kweli nimekuwa mwaminifu, na Roho wa Mungu amekuwa akinitia moyo kwamba, ukiwa mwaminifu kwa mali ya mtu Mungu atakupa ya kwako mwenyewe, ukiwa mwaminifu katika pesa kidogo Mungu atakupa nyingi. Hujawahi  kuona wauzaji waaminifu huishia kumiliki mali na amana zao wenyewe. Mara nyingi imetokea sawa sawa na neno la Bwana. “Aliye mwaminifu katika lililo dogo sana, huwa mwaminifu katika lililo kubwa pia; na aliye dhalimu katika lililo dogo, huwa dhalimu katika lililo kubwa pia. Basi, kama ninyi hamkuwa waaminifu katika mali ya udhalimu, ni nani atakayewapa amana mali ya kweli” Luka 16:10-11
Kwa lugha nyingine kila unapoiba huwa unamwambia Mungu siko tayari kumiliki mali yangu mwenyewe. Vivyo hivyo kila unapozini na kusema uongo huwa unamwambia Mungu kwamba, “sifai kuwa tajiri.” Ni ukweli uliowazi maana kilichozungumzwa ni uaminifu ambao ni zaidi ya kutokuiba. Yusufu alipimwa uaminifu wake kwa kutaka kubakwa na mke wa Potifa. Kitendo cha Yusufu kukimbia na kukataa uovu huo kilituma ujumbe kwa Mungu kama huu, “Yusufu yuko tayari kuwa tajiri mpatie.”
Matajiri wengi wanafanikiwa kama kuku. Kuku akilishwa vizuri na kunawiri ni ili achinjwe. Matajiri wengi wako tayari kwa kuchinjwa. Utasikia amejinyonga, utasikia amechomwa kisu, utasikia amekufa kwa sababu ya kansa ya koo iletwayo kwa kupitia kuvuta sigara. They get rich only to die young!
Ni heri maskini mwaminifu kama Lazaro kuliko tajiri mwizi na fisadi. Dunia inadanganya inasema kipagani eti, ni sawasawa kuiba ili kuendelea, “The pagan society says,’ its okay, to lie, steal and cheat to get ahead’.” Uaminifu unazawadi yake, raha yake na fahari yake. Watu dhaifu na legelege hawawezi kuwa waaminifu, uaminifu ni haiba ya juu kabisa si rahisi kuipata kwa watu ambao hawajaunganika na Mungu.
Nakutakia msimu mzuri wa Krismas na mwaka mpya 2017, barikiwa tena Mungu na akuhifadhi daima.

0 comments :

Wote wametenda dhambi

6:17:00 PM Unknown 0 Comments


WOTE WAMETENDA DHAMBI
(“kwa sababu wote wamefanya dhambi, na kupungukiwa na utukufu wa Mungu;” Rum 3:23)
Biblia inasema, wote, haisemi kabila fulani au nchi fulani tu ndiyo imetenda dhambi. Hakuna kabila wala nchi ya wenye dhambi, sote tumetenda dhambi. Kupitia dhambi ya Adam makabila yote, wanadamu wote na nchi zote ziliingizwa katika hali ya dhambi. Hapa hakuna wa kumbagua mwingine.
Nimewahi kusikia watu wakibaguana kikabila wakisema usioe kule na wengine wakidai usiolewe katika kabila lile. Kigezo chao ni dhambi ambazo hata wao na nchi zao, na jamaa zao wanatenda. Katika agano jipya tunapata makundi mawili tu ya watu, waaminio na wasio amini. Biblia inasema, waaminio wataokoka na wasio amini wamekwisha hukumiwa. Imani ndiyo kigezo cha kuungana na mtu fulani au kutokuungana naye.
Nadhani mstari huu ni mstari ambao haujaeleweka miongoni mwa wengi. Sote tuliumbwa kwa sura na mfano wa Mungu ambao kwangu mimi nasema sura hiyo ni utukufu. Biblia inasema, wametenda dhambi na kupungukiwa na utukufu; kwa hiyo sura ya Mungu ambayo ni utukufu wake katika maisha yetu ilipungua kwa sababu ya dhambi. Rum 3:23
Kuna mtazamo wa kuitazama nchi ya Israeli kama bora kuliko nyingine, na wengine hudhani kwamba, ni Baraka kwenda Israel jambo ambalo si kweli kabisa. Wakristo hatuna hija ya kusafiri bali ya imani katika Yesu Kristo. Israel kama taifa hawakumkubali Yesu na ndio sababu iliyomfanya Mungu aachane na wito wa ngazi ya taifa na kuelekea kwa ngazi ya mtu binafsi kama yanenavyo maandiko, “bali wote waliompokea…” Yohane 1:12
Je, unataka kuungane na mtu? Je, unataka kuwa na uhusiano na mtu kibiashara? Unataka kumdhamini mtu? Kigezo si kabila ya au rangi yake, bali unapaswa kuangalia kama ni mmoja kati ya wale wamwaminio Yesu Kristo au lah! Biblia inasema, “Tusifungiwe nira isivyosawasawa na mtu asiye amini.” Inakataza kuunganishwa au kuungana isivyo faa na mtu asiye amini.
Badala ya kunyoosheana vidole ni vema wote tungefika alipofika John Newton yule mwandishi wa wimbo wa, ‘amazing grace’ aliyesema, “Ninachojua mimi ni mwenye dhambi mkuu, Na Yesu Kristo ni mwokozi mkuu.”
Kama unaamini Yesu alikufa kwa ajili yako basi ni muhimu pia uamini ulikuwa uu, mwenye dhambi, kama usingelikuwa na dhambi asingekufa kwa ajili yako. Nina amini hakuna aliyezaidi ya mwingine kikabila, kimataifa wala kiukoo, sote tumetenda dhambi na kupoungukiwa na utukufu na hivyo tunamuhitaji Yesu Kristo, Great Saviour!  Mpaka wiki ijayo shallomu.

0 comments :

Mara nyingi sana

5:45:00 PM Unknown 0 Comments


MARA NYINGI SANA
(Saba mara sabini)
Wanaofuatilia huduma ya Uinjilisti watakuwa wanamfahamu au kumsikia ndugu Jimmy Swaggart, yeye hupenda kujiita brother Swaggart, ni mwinjilisti mwenye alama ya aina yake na mwenye kutembea mwendo mrefu kwa miaka kadhaa katika huduma aliyopewa. Ameonja kuanguka na kusimama na hapa anatoa funzo: “Msalaba wa Yesu kila siku unatenda kazi kamwe haushindwi, ni mimi na wewe tunaoweza kushindwa. Sisemi kama ikitokea ukianguka (maana utaanguka kweli) kama hautaacha kumwamini Yesu hata katika anguko lako, Yeye Bwana Yesu hatakuacha na mwishowe atakusimamisha maana hujaacha kumwamini hata katika kuanguka kwako.”
Kwa tafsiri yangu Jimmy anasema, kuanguka kupo, ndio maana haoni sababu ya kusema ikitokea ukianguka maana anajua itatokea. Katika huduma yake ameanguka na kusimama, anajua machungu ya kuanguka, anasisitiza tusikate tamaa maana msalaba wa Yesu unauweza wa kuokoa nyakati zote. Asubuhi moja nikiwa katika Studio za Ileje Fm radio msikilizaji aliniuliza kama, Mungu anaweza kusamehe dhambi kubwa. Nilimjibu, “Ndiyo anaweza, mara nyingi tu.” Si tu kwamba Mungu anasamehe bali anasamehe mara nyingi. Many times!
Baadaye nilimpa mfano tuliopewa na paroko kanisani kwetu, nanukuu: “mtu mmoja alimuuliza padre mmoja akisema, ‘padri nimemuua bosi wangu, Je! naweza kusamehewa? Padri akamjibu akasema, ‘unaweza kusamehewa bila shaka’ yule bwana akaendelea akasema, ‘wakati nikimuua bosi wangu dereva wake aliniona, ili kufuta ushahidi nikamuua na dereva je, naweza kusamehewa? Akamjibu ndiyo bila shaka. Akamwambia, ‘Padri niwie radhi kwani, nilipokuwa nikimuua dereva mke wa bosi aliniona ikabidi nimchinje na yeye pia. Vipi na hilo nalo Mungu anaweza kusamehe? Padri akajibu ndiyo bila shaka.’”
Usikate tamaa  Mungu anaweza kukusamehe haijalishi umefanya nini. Somo kuu la mfano hapo juu ni hili; Si kwamba Mungu anaweza kusamehe tu, bali anaweza kusamehe mara nyingi zaidi.
Mungu ni upendo. Maandiko yanasema upendo husitiri dhambi nyingi. Usipokata tamaa Mungu hatakuacha, na hata ukikata tamaa yeye ataendelea kukutafuta maana wokovu wako ni muhimu. Si sisi tuliomtuma mjumbe aende mbinguni kumshusha Yesu ili aje atuokoe bali ni Mungu aliyemtuma Yesu ashuke kutuletea wokovu.
Kila mtu anaweza kusamehe lakini si kila mtu anaweza kusamehe mara nyingi. Tabia kuu ya kimungu (great godly character) haiko katika kusamehe tu, bali iko katika kusamahe mara nyingi zaidi. Hata wapagani kuna nyakati husamehe, lakini hawawezi kufanya hivyo zaidi ya mara saba. Mitume walidhani, unaweza kusamehe mara saba tu, na kumbe ni zaidi ya hapo.
Msamaha unaponya mahusiano, unaponya ndoa, unaponya kanisa na nchi kwa ujumla. Asiye mfuasi wa msamaha ni mfuasi wa vita. Kuna wengine husema jino kwa jino, hili linawezekana ikiwa tu aliyekukosea ni mdogo. Ikiwa unapenda kulipiza kisasi badala ya kusamehe napenda kukuuliza, Je, utafanya nini ikiwa aliyekukosea anazo nguvu kuliko wewe? Je, utafanya nini ikiwa aliyekukosea ni mkuu sana? Naamini utamwachia Bwana maana, kisasi ni juu yake. Kama hatuwezi kusamehe hatuwezi kumwachia Mungu, kwani tutaona kama vile Mungu hawezi kumwadhibu vizuri mhusika.  Jifunze kusamehe mara nyingi zaidi, tamka msamaha sirini na hadharani pia, wewe uliyesamehewa makosa yako unawezaje kushindwa kusamehe wengine? Mathayo 6:14-15
Leo ninakuachia kazi ya nyumbani (home work) ifuatayo, piga simu, tuma meseji ya kusamehe na kama aliyekukosea yuko karibu mwambia nimekusamehe.
BARIKIWA

0 comments :

Mungu Anakutazama

10:05:00 AM Unknown 0 Comments

MUNGU ANAKUTAZAMA
(Maovu na mema yote hutendeka mbele ya macho ya Mungu)
Katika tasnia ya michezo, wengi wetu tumezoea kucheza vizuri mahali ambapo mashabiki au watazamaji ni wengi. Si wachezaji wengi wanaweza kujituma na kucheza kwa bidii sirini. Wengi hupenda kucheza vizuri wakiwa wanatazamwa na maelfu ya mashabiki jukwaani. Si ajabu ndio maana viwanja kama Old Trafford na Stanford Bridge (viwanja vya soka) huchukua mashabiki wengi, na wachezaji hujiona wabarikiwa wakisakata katika nyasi hizo.
Lakini ni lazima tujue wazi kwamba, Mungu ni mkuu kuliko watazamaji, anaona ndani ya mioyo yetu na hata nafsini mwetu. Ufanisi wake katika kuyatazama maisha yetu ni mkubwa kuliko mamilioni ya mashabiki wasioweza kutazama mpaka moyoni. Mwenye hekima mmoja anasema, “You’re for an audience of one: GOD ” akimaanisha, “Tunaishi kwa ajili ya kusanyiko la mtazamaji mmoja; MUNGU.” Tunapaswa kulenga kumpendeza yeye na kumtukuza yeye peke yake ambaye kwa nyakati zote hutuona.
Ikiwa kusanyiko unalolenga kulipendeza ni la watu, basi uwe na hakika mwenendo wako utakuwa mbaya katika nyakati ambazo hawakuoni, na ikiwa unalenga kumpendeza Mungu mwenendo wako utakuwa safi nyakati zote. Mungu akiwa ndio kusanyiko lako, basi utaishi vema maana yeye anapatikana mahali kote, si uwanjani wala ukumbini tu; bali yuko nasi gizani na nuruni, asubuhi, mchana jioni hata usiku.
Kitendo cha Adam na Eva (kabla ya anguko) kuishi bila nguo, tena bila ya kuona aibu kilikuwa ni alama ya uaminifu na hali ya kuwa bila hatia mbele za Mungu. Hawakuwa na kitu cha kuficha mbele za Mungu, hawakusongwa na jambo lolote ambalo lingewafanya waone aibu mbele za Mungu. Mwanzo 2:25
Kundi kubwa leo tumekuwa na sura tatu, ile ambayo jamii inaijua, ile ambayo sisi na Mungu tunaijua, na ile ambayo Mungu peke yake huijua. Ni muhimu kuwa na sura moja isiyobadilika, ni vema kutokuwa vuguvugu tena ni muhimu kukataa unafiki ambao tafrisiri yake rahisi ni kuwa na sura nyingi (many faces).
Mtu mmoja alisifika sana ofisini ilhali nyumbani kwake hawakuwa na furaha naye kabisa, alikuwa mwema kwa watu wasio wake na aliwatesa walio wake. Sura yake ya nyumbani ilikuwa tofauti na u-malaika aliouonesha ofisini. Ni msemo wa kutisha na usiotakiwa, “saint at abroad and devil at home.” Yaani, “Mtakatifu akiwa mbali, shetani nyumbani.” Ni muhimu kutafuta sura moja, nyumbani na ugenini, usiku na mchana, chumbani na nje ya chumba.
Dhambi zote hutendeka mbele ya macho ya Mungu. Tafakari hili neno, mbele ya macho yake. Kila dhambi tutendayo tunamkosea Mungu peke yake. Maumivu ya dhambi humwelekea Mungu ndio maana kuna nyakati hushindwa kuvumilia. Usije fikiri hata mara moja kwamba, unajikosea au unamkosea jirani, mara nyingi tunapokosa tunamkosea Mungu. Unapomtendea jirani yako uovu unamtendea Mungu. Inatisha kwani mabaya yote hutendeka mbele ya macho yake.
Tafakari na kuchukua hatua, Mungu yuko tayari kusamehe nyakati zote.

0 comments :

Ninapotoa dhabihu ya shukurani

2:29:00 PM Unknown 0 Comments

NINAPOTOA DHABIHU YA SHUKRANI “
“Atoaye dhabihu za kunishukuru, ndiye anayenitukuza (anayeniheshimu); anaanda njia ya Mimi kumuonesha wokovu wa Mungu” Zab 50:23 (NIV)
Ili uweza kutafakari mstari tajwa hapo juu ni vema uweke jina lako au ujitazame katika mstari huo. Ni wewe unayemtukuza? Je, ni wewe unayejiandalia njia ya wokovu wa Mungu? Mara nyingi watu hufanya jambo baada ya kutambua uzito au umuhimu wa jambo hilo. Si watu wengi sana wanaelewa umuhimu wa kuwa na moyo wa shukrani mbele za Mungu; hivyo ni rahisi sana kwa mtu kuomba akiwa na hitaji, lakini ni watu wachache sana wanaokumbuka kushukuru baada ya kujibiwa mahitaji yao.  Lakini pia, Mbali na kumshukuru Mungu baada ya kujibu maombi yako, unaweza kujizoeza au kujifunza kuwa na moyo wa shukrani mbele za Mungu kama tabia au mtindo wa maisha yako (A grateful heart).
Kuna tofauti kubwa kati ya kushukuru baada ya Mungu kujibu ombi la mahitaji yako na kuwa na moyo wa shukrani. Moyo wa shukrani ni zaidi ya kushukuru, ni mfumo au utaratibu wa maisha ya mtu. Kushukuru kunaweza kutokea mara moja au kwa msimu, lakini moyo wa shukrani ni tabia au mfumo wa kimaisha endelevu.
Ni mtu mwenye moyo wa shukrani pekee ndiye anayeweza kumshukuru Mungu katika kila jambo. Kumbuka kuna tofauti ya kumshukuru Mungu kwa kila jambo na kumshukuru Mungu katika kila jambo. Tafasiri ya kiingereza ya 1 Wathesalonike 5:17 inasema “toeni shukrani kwa Mungu katika kila hali/jambo kwa kuwa hayo ni mapenzi ya Mungu kwenu” (tafasiri isiyo rasmi). Kinachowafanya baadhi ya watu washindwe kumshukuru Mungu ni hali ya kutokuamini kwamba hayo ni mapenzi ya Mungu. Tukijua kwamba yatupatayo ni mapenzi yake, tutapenda kumshukuru hata kama mambo hayo yameleta simanzi.
Moyo wa shukrani unamfanya mtu ahesabu Baraka za Mungu katika maisha yake kuliko changamoto zake. Ni moyo wa shukrani pekee ndio unaoweza kumfanya mtu aone Mungu ni mkubwa kuliko hali yake. Moyo wa shurani humfanya mtu kuacha kulalamika juu ya kile ambacho Mungu hajajibu na kuanza kumshukuru Mungu juu ya kile ambacho amewahi kujibu.  Moyo wa shukrani hutafuta sababu ya kumshukuru Mungu katika kila jambo na kila hali. (Zab77:2, 6-10,11-19)
Mtume Paulo alipopelekwa gerezani naweza kusema bila shaka hakumshukuru Mungu kwa kutupwa gerezani lakini nina uhakika kuwepo kwake gerezani hakukumzuia kumshukuru na kumsifu Mungu. Hii inatupa kuona kuwa inawezekana kumshukuru Mungu katika kila jambo, na huu ndio moyo wa shukrani yaani mfumo wa Maisha.  (Matendo ya Mitume 16:25-26)
Moyo wa shukrani unatoa fursa kwa Mungu kudhihirisha wokovu wake. Kwa lugha rahisi, moyo wa shukrani hutoa fursa kwa nguvu za Mungu kuwa tayari muda wote (standby) ili kukusaidia utakapohitaji; ndio maana mstari wetu wa kutufungulia hapo juu unasema, “anaandaa njia ya Mimi kumuonesha wokovu wangu”. Moyo wa shukrani huvuta upendeleo (kibali) wa Ki-Mungu katika maisha ya mtu kuliko anavyoweza kufikiri. Ningeweza kusema, kushukuru kunavuta wingu la upendeleo wa Ki-Mungu (God’s favor); lakini Moyo wa shukrani hushikilia wingu la upendeleo wa Ki-Mungu ili kukaa katika maisha ya mtu (cause it to dwell).

0 comments :

Jina lako nani?

1:14:00 PM Unknown 0 Comments


JINA LAKO NANI?
( Unajionaje nafsini mwako )
Zamani tulifuga mbwa na tuliwita jina kaburu, tulitaka awe mkali kama wale makaburu wa Afrika ya kusini. Makaburu hawakuwa na sifa njema, waliwatesa sana watu weusi kule nchini Afrika kusini. Waliwatendea kwa ukali na kwa ukatili mkubwa na hata kuwaua.
Mbwa yule alikuwa mkali sawa sawa na jina lake, alipokwenda kung’ata hakupiga kelele aling’ata kimya kimya. Mbwa yule alituletea kesi kadhaa za kuuma watu nyakati za asubuhi. Iko nguvu ya ajabu katika jina na katika namna unavyojiona wewe mwenyewe. Mtu hufanana na namna anavyojitazama ndani yake.
Unapoitwa jina lenye kukupinga au lenye kuashiria ulegevu na laana unapaswa kulikataa, au kuwa na mtazamo mpya ndani yako ili maisha yako yafanane na jina lako. Ukiitwa jina Shida, Mwadawa, Maganga, Sikitu, Lameck na majina mengine yafananayo na hayo ni lazima uyakatae na kuchagua jina jema. Hata kama watu wasiojua wataendelea kukuita kwa majina mabaya lakini tayari ndani yako utakuwa unajua wewe ni mtu tofauti. Utakuwa unajua wewe ni hodari, wewe ni tariji, wewe ni taifa takatifu na tena ni mtu wa mafanikio.
Moja ya watu wanaofanikiwa sana katika utawala ni wale wenye majina ya Benjamini tafsiri ya hili jina ni, mtu wa mkono wa kuume au kwa lugha nyingine ni mtu mkubwa. Mimi nawafahamu Benjamin wachache tu ambao walifanikiwa kuwa watu wakuu, Benjamin Mkapa alikuwa Rais wa Tanzani, Benjamin Franklin aliongoza huko Marekani na hata sasa Benjamin Natanyahu anaongoza huko Israel.
Wakati wa kuzaa kwake Raheli mke wa Yakobo alishikwa na utungu mkuu, na katika kujifungua kwake huko alifariki. Ikawa wakati wa kutoa roho yake alimwita mtoto wake jina Benoni, maana yake mwana wa uchungu wangu lakini Yakobo babaye alikataa asiitwe Benoni akasema aitwe Benjamini maana yake, mtoto wa mkono wangu wa kuume (mtawala) na tazama Benjamin alikuwa mtu mkubwa. Mwanzo 34:18
Na Yakobo anapombariki Benjamin anamfananisha na mbwa mwitu, mtu imara na mwenye nguvu ya kutafuta asubuhi na usiku, mtu asiyeishiwa chakula. Ninaamini kama angeliitwa Benoni asingeliweza kuwa shupavu na mwenye akili kama namna alivyokuwa. Mwanzo 49:27
Kabila la Benjamin lilikuwa na heshima na umahiri mkubwa (brave and active) kwa kuwa liliambiwa litaketi mkono wa kuume ambao ni mkono wa heshima kuliko kushoto (Zaburi 80:17). Ni kabila lililopigana vita mara nyingi na kushinda na kujitwalia nyara kama mbwa mwitu anayejitajirisha kwa vitoweo. Kila kilichonenwa katika jina la Benjamini, kilitokea katika kabila la Benyamini. Watu wake walikuwa hodari na watawala wenye nguvu vitani. Sauli na Yonathani mwanaye moja ya viongozi na mashujaa kutoka katika kabila la Benjamin na wasomaji wa Biblia wanajua jinsi walivyokuwa watu hodari kwa vita na katika uongozi. {1Samweli 9:1, Waamuzi 20:21-25, 3:15, 5:14,}
Wewe ni mtu muhimu sana katika kujenga Ufalme wa Mungu hapa duniani. Jina lako linabeba lile kusudi (mission) ambalo Mungu alilokuumbia ulitekeleze. Chunguza maana ya jina lako.  Kataa maana mbaya zote za jina lako, litakase kwa damu ya Yesu na nenea mazuri jina lako.

0 comments :

Nani analeta maana...!

1:27:00 PM Unknown 0 Comments


NANI ANALETA MAANA KATIKA MAISHA YETU
(Mungu ndiye huleta maana katika maisha ya mwanadamu) 
Siku moja nilisoma mtandaoni mtu ameandika kiboko ya wachungaji wenye walinzi binafsi (board guards) ni hii Zaburi ya 127:1-2, nikacheka sana. Ninachoweza kuandika ni kwamba, hata kama wanadamu wanahusika Mungu lazima ahusishwe pia.  Imeandikwa, “1. Bwana asipoijenga nyumba Waijengao wafanya kazi bure. Bwana asipoulinda mji Yeye aulindaye akesha bure. 2. Kazi yenu ni bure, mnaoamka mapema, Na kukawia kwenda kulala, Na kula chakula cha taabu; Yeye humpa mpenzi wake usingizi.

Tafsiri ya huo mstari ni kwamba, usiingie kwenye mradi (project) ambao Mungu haufanyi. Usiwekeze nguvu zako mahali ambapo Mungu hawekezi. Usilinde asipolinda, ukisikia analinda basi hapo na wewe kalinde. Kwa lugha nyingine ni kwamba, fanya pamoja na Mungu. Shirikiana na Mungu katika kazi zako, Do not try to work alone! Ukishaona Mungu hayumo katika mchakato fulani lazima ujue matokeo yatakuwa sifuri. Magumu na mabaya yaliyowapata Adamu na Eva yalitokana na kutengana na Mungu. Hata asingewalaani kwa kinywa chake bado matokeo ya kazi zao na maisha yao ingekuwa ni sifuri. Alama ya juu unayoweza kuipata unapotenda jambo bila ya Mungu ni sifuri (bure). Petro alionja sehemu ya laana ya  hawa wazazi wa kale yaani, Adamu na Eva baada ya kukesha usiku kucha katika uvuvi na kuambulia sifuri. We need Jesus! Luka 5:5

 Zamani niliona nembo (logo) ya shule moja imeandika, Life – Jesus = 0 yaani, maisha bila Yesu ni sifuri. BWANA Yesu ndiye anayeleta maana ya michakato yote ya maisha yetu. Mfumo wetu wa elimu bila Yesu ni bure, mfumo wetu wa ulinzi bila Yesu ni bure. Kazi bila Yesu ni sifuri, utajiri bila ya Mkono wa BWANA ni sifuri pia. Hakuna jambo ambalo linamuhusu mwanadamu ambalo Mungu hataki kushiriki. Kwa kuwa linamhusu mwanadamu linamhusu Mungu pia. Yesu alikwenda harusini kana ya Galilaya (Yohana 2), Yesu alikwenda msibani Lazaro alipokufa (Yohana 11), Yesu alikwenda kazini kwa Petro ambapo ni baharini kwa kuwa alikuwa mvuvi. Yesu alikwenda kushinda nyumbani kwa Zakayo na mara nyingine kwa Martha na Mariamu.

Ingawa kanisa lilikabidhiwa kwa Petro bado Kristo ndiye alikuwa mjenzi. Alimwambia, “Na juu ya mwamba huu nitalijenga kanisa langu” yaani, mjenzi ni Kristo (Mathayo16:18). Neno nitalijenga linaonesha wazi si Petro ambaye atajenga bali ni Yesu aliyemmiliki wa kanisa ndio atakayejenga; maana anasema, na juu ya mwamba huu (Petro) nitalijenga kanisa langu. Anahusika na furaha na huzuni zetu, anahusika na taaluma na siasa zetu. Ni BWANA wa watu wote tena ni BWANA  wa vitu vyote. Nadhani unafahamu mwenye nyumba anaweza hata asishike tofali lakini kwa kuwa ndiye aliyenunua kila kitu na ndiye anayetoa vitendea kazi huhesabika kuwa anajenga. Utasikia najenga huko mbezi au Madale. Anayetoa nguvu, vitendea kazi, ramani na maelekezo ndiyo mjenzi. Kristo ndiye mjenzi wa Kanisa wala si mtume, nabii, mchungaji wala kasisi.

Tunapotenda tukiwa na Mungu matokeo huwa makubwa na kazi huwa nyepesi kama usingizi. Tukiwa na Mungu tunaweza kupata matokeo makubwa (Big Results Now BRN); maandiko husema, “Yeye huwapa wapenzi wake usingizi.” Ni kama Petro alivyopata matokeo makubwa baada ya kutii, Utii wetu kwa Kristo ni mwisho wa laana. Hakuna hukumu wala laana kwa waliondani ya Kristo. Luka 5:5

Paulo anasema kuishi kwake ni Kristo, vipi wewe? Kuishi kwako ni anasa, ulevi au ni kazi yako?  Kuishi kwako ni mumeo au rafiki yako wa kiume au wa kike? Ni pale tu ambapo kuishi kwako ni Kristo ndipo uko salama. Ni rahisi kusema kuishi kwako ni Kristo kwa kuwa unalijua andika, lakini je, Kristo ndio maisha yako?  Mpaka umekubali kuishi kwako kuwe Kristo, maisha yako hayataleta maana. Kuishi kwetu ni bure ikiwa tuko nje ya Kristo. Flp 1:21

Tafakari na acha maisha yako yalete maana kwa kujitoa kwa Yesu.

0 comments :

Ni lazima kukua

5:46:00 PM Unknown 0 Comments

NI LAZIMA KUKUA.
Mwenyehekima mmoja amewahi kusema, ukuaji [wa mwili] ni jambo la asili; lakini maendeleo ni matokeo ya maamuzi ya mtu (Growth is natural but development has to be intentional). Hakuna mtu amewahi kuendelea kwa bahati mbaya [accidentally]; iwe ni kiroho, kiuchumi, kiuongozi n.k! Mpaka mtu ameamua [nuia] kuendelea katika eneo fulani, atabaki katika hali ile ile. Kanuni hii inafanya kazi kwa mtu mmoja mmoja, jamii hata taifa.
Nimewahi kusoma makala katika gazeti moja, ambapo mchambuzi alikuwa akieleza ni kwa namna gani bara la afrika linaweza kujifunza kutoka nchi ya China katika vita dhidi ya umasikini. Anasema mwaka 1966, China haikuwa na uwezo wa kuzalisha chakula cha kutosha watu wake lakini leo hii inauwezo wa kuzalisha chakula cha kutosha watu wake na kuuza nje ya nchi. Kumbe, kila mtu au jamii au taifa, lazima kwanza linuie kuendelea [Develop] katika eneo mahususi [specific] vinginevyo maendeleo hayawezi kutokea. Jambo kubwa tunalotaka uelewe hapo ni kwamba, kila mtu anawajibika binafsi katika kuhakikisha anapiga hatua kubwa ili leo iwe bora kuliko jana, na kesho iwe bora kuliko leo.
“Nilipokuwa mtoto mchanga, nalisema kama mtoto mchanga, nalifahamu kama mtoto mchanga, nalifikiri kama mtoto mchanga; tokea hapo nilipokuwa mtu mzima, nimeyabatilisha mambo ya kitoto” 1Kor 13: 11
Wataalamu wanasema, “kwa siku mwanadamu anafanya maamuzi karibu elfu kumi [10,000]” kwa mawazo ya haraka haraka unaweza ukaona kwamba chaguzi hizo {decisions} ni nyingi  kwa sababu tu tunapofanya maamuzi hayo hatufikiri sana. Si wengi wanaofikiri sana kwa nini hawakui, si wengi wanafikiri sana kwa nini ubora wao hauongezeki, si wengi wanaowaza kuhusu ubora wa afya zao. Kila kitu ni uchaguzi wako, hata wokovu ni matokeo ya uchaguzi na uamuzi wako. Aliandika Mt Agustino anaandika: “Mungu ambaye amekuumba bila kutaka, hawezi kukuokoa bila kutaka.”
Ili kukua ni lazima uchague maeneo ambayo unataka uone ukikua katika mwaka husika. Ukuaji lazima uzingatie muda, One day at a time! Maeneo yafuatayo ni muhimu kwa ukuaji wako:
  1. - Kitaaluma-Unaweza kusema mwaka huu lazima nisome shahada ya uzamili au ya uzamivu na ukatekeleza
  2. - Kiroho- Ni muhimu uwe na shauku ya kukua ili kufanana na Yesu. Yeye ni nuru hivyo ni lazima uwe nuru pia, yeye ni Mtakatifu na hivyo ni lazima uweke mkakati wa kuwa mtakatifu pia. 1 Yohana1:5-6
  3. - Kiuchumi- Mkakati wa kuongeza kipato na uwekezaji ni muhimu ufanyike kwa kuzingatia muda. Ni muhimu kuweka nia ya kuanzisha mradi au kuwekeza katika biashara ili kujiongezea kipato.
  4. - Sayansi na Teknohama- Ni lazima kila unachokifanya uchanganye na sayansi na teknolojia. Angalau ujue Microsoft Word, Power Point, Excel nakadhalika. Sayansi ya usindikaji ni muhimu ili kuongeza thamani ya bidhaa ghafi na mazao. Ukiipenda teknolojia utafanikiwa, mitandao ya kijamii pia ikitumika vizuri inaweza kukutangaza na kukupa fursa ya kipawa chako.
  5. - Kipaji chako- Kama unaimba basi ungalau jifunze pia kupiga hata chombo kimoja cha muziki, nenda chuo kinachokuza kipaji chako. Soma vitabu vinavyotoa mwongozo wa kipaji chako.
Mchakato wa ukuaji, unakutaka ukubali baadhi ya mambo, na ukatae baadhi ya mambo ili nguvu zako zielekee katika jambo moja. Ili kukua kwa haraka ni lazima ujifunze kuwa mtu wa jambo moja, bobea katika jambo moja, zamia kabisa katika fani yako. Hakikisha unakuwa na misuli katika kipaji chako hata watu wakutambue kama guru na kisha ujenge ufalme wa Mungu kwa kipaji hicho. Tukutana kileleni…..

0 comments :

Laiti kila mwenye dhambi angalitambua hili

9:44:00 PM Unknown 0 Comments

LAITI KILA MWENYE DHAMBI ANGELITAMBUA HILI!
[Wana ujumbe nusu na hivyo hauleti maana kamili]
Kila mwenye dhambi anajua fika kwamba yeye ni mwenye dhambi.  Kujua kwamba tuna dhambi haitoshi, lazima tujue kwamba, Mungu yuko tayari kutusamehe. Kujua kwamba, unadhambi kunaleta uchungu lakini kujua kwamba, Mungu yuko tayari kusamehe kunaleta amani ikiwa utalifanyia kazi wazo hilo. Kama kila mdhambi angelijua hilo angeliomba toba mapema.
Mungu hafanyi maandalizi ili ajiweke tayari kusamehe bali yuko tayari hata sasa kusamehe. Laiti kama kila mwenye dhambi angelijua hili, wengi wangetubu, shida yao wana ujumbe nusu, wanajua wazi ni wenye dhambi, bali hawajui  kama Mungu yuko tayari kusamehe.
Yohana 8:1-8 inaeleza, nyakati zile Mafarisayo walipomkamata [mfumania] yule mwanamke katika zinaa walimpeleka mbele za Yesu wakiwa na wazo la kumpiga kwa mawe mpaka kufa kama ilivyokuwa katika sheria ya Musa. Lakini Yesu aliposema, “asiye na dhambi na awe wa kwanza kumtupia jiwe”, biblia inasema, wote waliokuwa pale kuanzia watoto wadogo mpaka wazee walishtakiwa mioyoni mwao, ikiwa na maana mioyoni mwao walishuhudiwa kwamba, wao pia ni wenye dhambi. Hakuna mwenye dhambi asiyejua kwamba yeye ni mwenye dhambi. {Yohana 8:7-8}
John Newton mtunzi wa wimbo maarufu duniani, ‘amazing grace’ anasema, “nijualo mimi ni hili, mimi ni mwenye dhambi mkuu, na Yesu Kristo ni Mwokozi mkuu”. Anajua yeye ni mwenye dhambi na anaifahamu na tiba pia.  Hakuna mwenye dhambi asiyejijua wala asiyeijua hukumu yake. Imeandikwa:  Maana neno hili mnalijua hakika, ya kwamba hakuna mwasherati wala mchafu wala mwenye tamaa, ndiye mwabudu sanamu, aliye na urithi katika ufalme wa Kristo na Mungu.” Waefeso 5:5
Paulo anasema, neno hilo tunalijua hakika, tunafanya tunachokijua, tunajua madhara yake na hasara zake tunazijua pia. Je, ni nani hajui kama Mungu anachukia wizi, udhalimu, uchafu na ubaya wote? Bila shaka sote tunajua.
Yesu aliposema asiye na dhambi na awe wa kwanza kumtupia mwanamke huyu jiwe, biblia inasema wote walisutwa nafsini mwao yaani, hakusalia hata mmoja asiyekuwa na dhambi wala ambaye hakujua kwamba anadhambi. Kumbe kila mwenye dhambi anajua anazo lakini hataki kuzipeleke kwa Yesu, maana hata hawa baada ya kushtakiwa mioyoni mwao hawakumwendea Yesu, badala yake waliondoka zao wakamwacha Yesu na yule mwanamke.
Ni muda muafaka sasa tumejua kwamba tunadhambi na tunachukua uamuzi wa busara wa kuzipeleka mbele za BWANA badala kukimbia au kuendelea kukaa nazo kama walivyofanya wayahudi hawa. Mungu yuko tayari kusamehe muda wote ungalipo hai, Mungu ni wa rehema na ni mwenye huruma nyingi; hatamdharau mtu mwenye dhambi atubuye, wala hawezi kumwacha aliyeumizwa katika ukosaji. Napenda kukualika leo mwendee kwa kusema maneno haya: “Ee BWANA uniwie radhi mimi mwenye dhambi, nimejua makosa yangu na nimejua wokovu wako. Unioshe kwa damu yako na unioneshe na wokovu wako leo. Amina”
Aksante kwa kuja na kushiriki katika msimu wa nne [4] wa weekend of purpose, makala zijazo tutakujuza  mafundisho yatokanayo na weekend of purpose kwa uchache.

0 comments :

Watu wake ni akina nani?

6:44:00 PM Unknown 0 Comments

 
WATU WAKE NI AKINA NANI?
Basi, kabla ya sikukuu ya Pasaka, Yesu, hali akijua ya kuwa saa yake imefika, atakayotoka katika ulimwengu kwenda kwa Baba, naye ali amewapenda watu wake katika ulimwengu, aliwapenda upeo. Yohana 13:1

Unaposoma maandiko kwamba, Yesu aliwapenda watu wake swali unaloweza kujiuliza ni hili, watu wake ni akina nani hao? Ni kwa nini awapende kwa upendo wote. Neno aliwapenda upeo lina maana aliwapenda kwa upendo wote au kwa utimilifu wa upendo. Upendo huu Yesu alionesha wakati mauti yake imekaribia, alipata shida kuachana na wale aliowapenda na alitamani kuendelea kukaa  nao kwa kitambo kirefu. Ni kama mtu anapotoa wosia wa mwisho kwa watoto aliowapenda mno.

Katika tafakari yangu ninaamini walio wake ni hawa: 

  1. ~ Ni wale walioacha vyote wakamfuata [Mathayo 9:27].
  2. ~ Ni wale waliojikana na kuchukua msalaba [Marko 8:34-35].
  3. ~ Ni wale waliaminio jina lake [Yohana 1:12].
  4. ~ Ni wale waliokaa katika neno lake [Yohana 8:31-32].

Makundi hayo manne ni makundi ya watu ambao BWANA aliwapenda upeo wala hakupenda kuachana nao. Walikuwa watu waliochukua msalaba na kumfuata, walikuwa watu wenye kusikia neno lake na kulitenda.  Hawa ni watu walioacha mashamba, ndugu wa kike na kiume, ni ambao waliacha mambo mazuri wakaamua kumfuata BWANA.

Sharti la kuwa mwanafunzi wa Yesu si gumu wala huhitaji kuwa myahudi ili uwe mwanafunzi wake, unachohitaji kukifanya ni kukaa katika neno lake. Kulisoma kila siku na kulitenda. Ni vema kutenga muda ili kupata wasaa angalau nusu saa ya kusoma  neno na robo saa ya kutafakari.

Kama alivyowapenda waliomwamini nyakati zile, ndivyo anavyowapenda waamini wa leo, waliaminio Jina lake hata sasa. Anatupenda kwa upendo wote tena kwa upendo mtimilifu.

Mungu akubariki tukutane Boko Karmeli kwa masista kwa ajili ya programu ya Weekend of Purpose itakayofanyika Jumamosi na Jumapili, tarehe 15 na 16 mwezi wa kumi . Usikose

0 comments :

Tazama zaidi ya uonanyo

11:14:00 AM Unknown 0 Comments


TAZAMA ZAIDI YA UONAVYO

Watu wanapokutana na ukinzani/changamoto  katika jambo, mambo mawili huweza kutokea; kukosa nguvu na  ujasiri wa kuendelea mbele hadi kupata mpenyo,  au kukosa  uvumili na hivyo kutafuta njia mbadala hata kama si salama ili kufikia tamanio lake. Mtu wa namna hii huona changamoto kama mwisho au kikwazo cha kufikia mafanikio yake. Mfalme Sauli alipokutana na Goliath, yeye na Israeli yote isipokuwa Daudi walikosa nguvu na ujasiri wa kuendelea mbele [1Sam 17:11]; wakati Ibrahimu alipokutana na changamoto ya kupata mtoto, aliingia kwa mfanyakazi wake kama njia mbadala ili kufikia matamanio yake, na gharama yake ilikuwa kubwa. 

Robert H. Schuller, mwandishi wa kitabu cha “Tough times never last but tough people do”, anasema “Tofauti ya mtu anayeshinda na mtu anaishindwa katika changamoto [hiyo hiyo] wanayokutana nayo wote wawili au mazingira hayo hayo, ni namna ambavyo watu hao wamechagua kulitazama jambo hilo [Tafasiri ya mwandishi]”. Hivyo kumbe, namna ambavyo mtu anatazama au kuchagua kuona jambo au changamoto iliyopo mbele yake ndio huamua hatima ya mtu huyo katika jambo hilo; yaani kushinda au kushindwa kwake. [The ability to see beyond the situation is the key to overcome the challenge/crisis].

Musa alipokuta na vikwazo katika kuwakomboa wana wa Israeli kutoka katika utumwa wa Misri; hakuona kama tatizo la kumrudisha nyumba, bali aliona nafasi kwa yeye kuona Nguvu na Udhihirisho wa Mungu katika maisha yake na wana wa Israeli. Ndio maana kila alipokutana na tatizo au changamoto alikimbilia mbele za Mungu, kwa kuwa alijua ilikuwa ni fursa kwake ya kuona Ukuu wa Mungu; na kupitia ugumu wa Farao, Mungu atukuzwe na watu wote wapate kujua kuwa Mungu Anaishi.  Leo hii anajulikana kama mshindi [Kutoka 9:11, 29].

Wakati kila mtu anamuona Goliath kama tatizo katika Israeli, Daudi alimuona Goliath kama fursa ya kudhiirisha Ukuu na uweza wa Mungu; na ili dunia wapate kujua yuko Mungu katika Israeli. Lakini pia kwake, aliona kama fursa kwa yeye kuoa mtoto wa Mfalme bila kutoa mahari na mwanzo wa kuishi maisha bora, pia fursa kwa yeye pamoja na familia yake kuishi huru [1Sam 17:25, 46-47]. Leo hii anajulikana kama mshindi.

Mama Teresa wa Calcutta, mshindi wa tuzo ya amani ya Nobel alipoona maskini na watu wasio na msaada kule India; hakuona kama tatizo la kumkatisha tamaa, bali aliona fursa ya kumtumikia Mungu kwa kugusa maisha ya watu. Leo hii anajulikana kama mshindi.

Nimewahi kusikia habari za mama mmoja ambaye alikuwa amempa Yesu maisha yake; na alikuwa anafanyakazi katika kampuni fulani, lakini baada ya muda aliachishwa kazi; akaenda kwa mchungaji wake analia, mchugaji wake akamuuliza kwanini alikuwa analia!!!? Akamuuliza, “Je una kitu gani ambacho unaweza kufanya?” Yule mama akamjibu kuwa anaweza kutengeneza keki tu. Baada ya mazungumzo na mchungaji wake; akamuambia aende akatengeneze keki kisha apelekee pale alipoachishwa na kuwagawia wafanyakazi wenzie bure kama sehemu ya kuagana nao; mara ya kwanza hilo wazo halikuingia akilini mwa yule mama lakini akafanya kama alivyoambia na mchungaji wake. Alipomaliza, wakati anarudi nyumbani, watu mbalimbali pale ofisini wakamtafuta na kumuuliza kama anaweza kuwatengenezea keki kwa “oda” maalumu, kwa kuwa keki zake ni nzuri. Baada ya muda kidogo yule mama alikuwa na ofisi yake, akanunua mashine kubwa zaidi na kuajiri watu wengine katika ofisi yake.

Mara kadhaa tumesikia watu wakisema, “Tatizo sio tatizo bali tatizo ni namna ambavyo mtu analitazama tatizo”; ukitafakari usemi huu utagundua kuna ukweli ndani yake. Kumbe, hatua ya kwanza kwa mtu ili aweze kuvuka katika changamoto fulani, ni kuangalia namna ambavyo analitazama jambo hilo vinginevyo mtu anaweza kufanya kosa kama la Ibrahimu au kukubali kuwa dhaifu mbele ya changamoto kama mfalme Sauli na wana Israeli . Wiki ijayo tutangalia mambo kadhaa ya kumsaidia mtu aweze kuona zaidi ya anachoona ili kupata matokeo bora zaidi….

See you at the Top

0 comments :

Kupatwa kwa jua

3:08:00 PM Unknown 0 Comments

KUPATWA KWA JUA.
(Wafu hawawezi kumchagua Yesu wala kumkataa shetani)
Alhamisi, Septemba Mosi ilikuwa siku ya kupatwa kwa jua. Maeneo mengi ya mkoa wa Mbeya hususani Rujewa yalishuhudia kufifia kwa mwanga na giza kutokea kwa masaa kadhaa. Naamini ilikuwa hivyo kwa maeneo mengi ya Tanzania na Afrika Mashariki kwa ujumla.
Kituo cha habari cha BBC kilifanya mahojiano na Mheshimiwa Ghalib Bilal kuhusu kupatwa kwa jua na hapo nikataka kusikia machache kuhusu jambo hilo. Katika mahojiano hayo dondoo kubwa niliyopata ni kwamba, “kupatwa kamili hutokea mara moja katika eneo fulani kila baada ya miaka 300.” Kupatwa kamili kwa jua kutatokea tena hapa nchini kwetu miaka 360 ijayo. (At any place on Earth, a Total Solar Eclipse can be seen on average once every 360 years.). Only my grave will witness that.
Miaka mia tatu ijayo mimi wala wewe hatutakuwepo. Kumbe hatuna nafasi ya kuona tena kupatwa kamili kwa jua tukiwa Tanzania. Tunachoweza kukiona tena ni kupatwa kwa kawaida tu ambako hutokea mara kwa mara na si kupatwa kamili. Je, utakuwa wapi miaka mia tatu ijayo? Je, ratiba yako ya siku inakupa kujiandaa na maisha hayo ya umilele?
Ni vema kujiandaa! Ni ukweli ulio wazi, dhambi ni kikwazo cha maandalizi yetu. Kama ilivyokuwa kwa Adamu watu hawatendi dhambi kwa bahati mbaya au kwa kudanganywa, bali hutenda kwa kuchagua. Yesu alikuwa kijana na alijaribiwa kama sisi na hakutenda dhambi. Dhambi ni uchaguzi. Tunatenda kwa sababu tumeamua kumkana na tumechagua kutenda. We sin not because we have to, but it is because we want to.
Kila siku watu zaidi ya mia moja hamsini hufariki, magaidi nao wanasababisha vifo katika halaiki za watu. Kuuawa na gaidi hakukufanyi uokoke, unamuhitaji Yesu kwa umilele wako. Mamia ya wanachuo wa Garisa huko Kenya waliuawa na magaidi wa alshababu; tukio hilo haliwapi marehemu hao kumwona Mungu ikiwa hawakumchagua Yesu wakati wa uhai wao.
Ukimkataa Yesu ukiwa hai huwezi kumkubali ukiwa kaburini, ndio maana hakuna nchi duniani ambayo marehemu wanapiga kura. Wafu hawawezi kumchagua Yesu wala kumkataa shetani. Ni walio hai tu ndio wana uwezo huo. Dereva mmoja akielezea uzoefu wake wa kesi za ajali za barabarani alisema, “Marehemu hashindi kesi.”
Ukikosa kufika mbinguni huwezi kukosa kufika motoni. Wasio kwenda mbinguni huenda motoni. Watu wengi hawavutiwi sana na kwenda mbinguni kwa sababu hakuna walichowekeza huko. Hawajawekeza tumaini, imani, upendo, fedha wala matendo mema; hakuna wanachotazamia kukiona wakifika huko, ndio maana hawana fikra za kwenda huko.
Donald Trump anapokwenda Uingereza anakwenda kuona alichowekeza, Dangote anapokuja Tanzania (Mtwara) ni kutazama alichowekeza huko. Tukiweka pesa zetu mbinguni, tukikataa mambo ya dunia basi bila shaka shauku yetu ya kwenda mbinguni itaongezeka mara dufu maana tumewekeza huko. Hakuna mfanyabiashara anayeridhika kwa kupata taarifa za simu tu bila ya kufika eneo ilipo biashara yake ilikujiona kwa macho kinachoendelea, vivyo hivyo haitoshi kusikia tu simulizi za mbinguni ni lazima siku moja tufike huko.
Yesu alikuja kwa sababu ya walio wake, na sisi hatuna budi kumfuata aliko kwa sababu Yesu ni wetu. Tukiwekeza hazina yetu mbinguni tutatamani kwenda kwa sababu hazina ya mtu ilipo na moyo wake upo. Jifunze huduma kama hawa wa Luka 8:3 ambao waliamua kuhubiri na Yesu kwa fedha zao: “na Yoana mkewe Kuza, wakili wake Herode, na Susana, na wengine wengi, waliokuwa wakimhudumia kwa mali zao.
BWANA AKUBARIKI

0 comments :

Jitazame kama Mungu anavyokutazama

11:38:00 AM Unknown 0 Comments

JITAZAME KAMA MUNGU ANAVYOKUTAZAMA 
Sehemu kubwa ya maisha ya mtu huathiriwa (influenced) sana na namna anavyojitazama. Mara nyingi, mtazamo wa mtu juu ya maisha yake na nafsi yake huamua hatima yake. Mtu anayejitazama kama aliyeshindwa (failure) katika jambo fulani; hakuna namna ataweza kushinda au kufanikiwa katika jambo hilo. Hakuna mtu aliyeweza kwenda mbali zaidi ya mtizamo wake (jinsi aonavyo nafsini mwake). Kumbuka, Jinsi ujitazamavyo, ndio kikomo chako.
Suleimani, Mwenye hekima wa kale na kiongozi wa taifa la Israeli  amewahi kusema, “Maana aonavyo (mtu) nafsini mwake ndivyo alivyo”.  Akiwa na maana kwamba, kiwango na aina ya maisha anayoishi mtu ni matokeo ya namna mtu huyo anavyoona nafsini mwake. Kama mtu haridhishwi na aina ya maisha anayoishi au kiwango cha maisha anayoishi, hatua ya kwanza kabisa sio kubadili kazi au biashara; bali kuangalia na kubadili fikra na mtizamo wake uliomfikisha mahali alipo. Ndio maana wataalamu wa sayansi ya fedha wanasema, mtaji wa kwanza kwa mtu sio fedha bali wazo (mtizamo/fikra) jipya.
Tunaishi katika nyakati ambazo kila asubuhi unasikia na kusoma habari mbaya, kuyumba kwa uchumi, vita na majanga mbalimbali, ambayo kwa pamoja huleta hali ya kukata tamaa na kujiona hatuwezi, kana kwamba hakuna tumaini; Lakini habari njema ni kwamba, katikati ya vurugu za ulimwengu huu, unaweza kuchagua kuona tofauti; kujiona kama Mungu anavyokuona.
Wakati wa vita na tishio kwa taifa la Israeli kutoka kwa Goliati na majeshi ya Wafilisti, kila mtu alikuwa amekata tamaa na kukosa tumaini, lakini Daudi alichagua kujiona kama Mungu anavyomuona na mwisho wake ilikuwa ushindi mkuu kwake na kwa taifa lake. (1 Samweli 17:33, 37, 45-47)
Wakati wa tishio la Wamidiani, Gideoni alikuwa amejificha; Malaika akamtokea na kusema, “Bwana yu pamoja nawe ee shujaa”. Bwana alikuwa pamoja naye; na alikuwa anamuona na kumtambua Gideoni kama shujaa; Lakini Gideoni aliona Mungu hakuwa pamoja naye (amemuacha) yeye na taifa lake, hivyo  alijiona dhaifu na mtu asiye na msaada; ndio maana alikuwa amejificha. Lakini ukweli ni kwamba, changamoto alizokuwa nazo hazikuondoa ukweli na uhalisi wa kwamba Bwana yu pamoja naye na kuwa yeye ni Shujaa (Waamuzi 6:2, 11-14, 16). Changamoto zilizopo hazifuti wala kubadili msimamo na mtazamo wa Mungu juu ya maisha yako.
Gideoni hakufanywa shujaa wakati ule Malaika anamtokea, Malaika alimkuta Gideoni akiwa shujaa; ndio maana alimsalimia ee Shujaa; alichofanya malaika sio kuondoa changamoto za Wamidiani. Jambo la kwanza alihitaji kubadili namna ambavyo Gideoni anajitazama; ili aanze kujiona kama Mungu anavyomuona; ili aweze kuwa msaada kwa jamii yake pia. Naamini kabisa, kama asingebadili mtizamo wake na kuanza kujiona kama Mungu anavyomuona; Mungu angetafuta mtu mwingine wa kufanya naye kazi. Mpaka umejitazama kama Mungu anavyokutazama, kuna uwezekano mkubwa changamoto ulionayo ikaendelea kuwepo.
Kuna watu huomba na kusali kwa kushusha thamani yao kwa kujifananisha na vitu mbele za BWANA. Kuomba na kusali kwa namna hii si sawa mbele za Mungu. Mungu ametufanya kuwa watoto wake, warithi pamoja na Kristo Yesu (Joint heirs) na sisi ni matawi katika Mzabibu ambaye ni Yesu Kristo yaani tunauzima ule ule ndani yetu alionao Kristo (kumbuka uhai uliopo kwenye shina la mti ndio uhai huo huo ulipo kwenye matawi); Kwanini mtu ajione hana thamani mbele za Mungu aliyechagua kumvika taji ya utukufu na heshima namna hii? (Zaburi 8:4-6). Sala za namna hii hazioneshi kiwango cha mtu cha unyenyekevu mbele za Mungu, bali huoneshi kiwango cha ujinga (ukosefu wa maarifa) alicho nacho mtu.
Mwimbaji wa nyimbo za Injili, Sinach ameimba wimbo anasema “I know who I am (Ninajua/fahamu mimi ni nina)” swali langu kwako, je unajua wewe ni nani? Je unajiona kama Mungu anavyokuona; shujaa, mwana wa Mungu, mshindi, mwenye kuyaweza mambo yote katika Yeye, unajiona kama Mkono wa Mungu uko upande wako, mrithi pamoja na Kristo? Hakikisha unasikiliza vizuri wimbo wa mwanadada Sinach (unapatika youtube), itakuwa ni mahali pazuri pa kuanzia.
See you at the top

0 comments :