Watu wake ni akina nani?

6:44:00 PM Unknown 0 Comments

 
WATU WAKE NI AKINA NANI?
Basi, kabla ya sikukuu ya Pasaka, Yesu, hali akijua ya kuwa saa yake imefika, atakayotoka katika ulimwengu kwenda kwa Baba, naye ali amewapenda watu wake katika ulimwengu, aliwapenda upeo. Yohana 13:1

Unaposoma maandiko kwamba, Yesu aliwapenda watu wake swali unaloweza kujiuliza ni hili, watu wake ni akina nani hao? Ni kwa nini awapende kwa upendo wote. Neno aliwapenda upeo lina maana aliwapenda kwa upendo wote au kwa utimilifu wa upendo. Upendo huu Yesu alionesha wakati mauti yake imekaribia, alipata shida kuachana na wale aliowapenda na alitamani kuendelea kukaa  nao kwa kitambo kirefu. Ni kama mtu anapotoa wosia wa mwisho kwa watoto aliowapenda mno.

Katika tafakari yangu ninaamini walio wake ni hawa: 

  1. ~ Ni wale walioacha vyote wakamfuata [Mathayo 9:27].
  2. ~ Ni wale waliojikana na kuchukua msalaba [Marko 8:34-35].
  3. ~ Ni wale waliaminio jina lake [Yohana 1:12].
  4. ~ Ni wale waliokaa katika neno lake [Yohana 8:31-32].

Makundi hayo manne ni makundi ya watu ambao BWANA aliwapenda upeo wala hakupenda kuachana nao. Walikuwa watu waliochukua msalaba na kumfuata, walikuwa watu wenye kusikia neno lake na kulitenda.  Hawa ni watu walioacha mashamba, ndugu wa kike na kiume, ni ambao waliacha mambo mazuri wakaamua kumfuata BWANA.

Sharti la kuwa mwanafunzi wa Yesu si gumu wala huhitaji kuwa myahudi ili uwe mwanafunzi wake, unachohitaji kukifanya ni kukaa katika neno lake. Kulisoma kila siku na kulitenda. Ni vema kutenga muda ili kupata wasaa angalau nusu saa ya kusoma  neno na robo saa ya kutafakari.

Kama alivyowapenda waliomwamini nyakati zile, ndivyo anavyowapenda waamini wa leo, waliaminio Jina lake hata sasa. Anatupenda kwa upendo wote tena kwa upendo mtimilifu.

Mungu akubariki tukutane Boko Karmeli kwa masista kwa ajili ya programu ya Weekend of Purpose itakayofanyika Jumamosi na Jumapili, tarehe 15 na 16 mwezi wa kumi . Usikose

0 comments :