Tunaishi mara moja tu!

12:10:00 PM Unknown 0 Comments


TUNAISHI MARA MOJA TU.
(Tumia vizuri awamu yako ya maisha)
“tena alikufa kwa ajili ya wote, ili walio hai wasiwe hai tena kwa ajili ya nafsi zao wenyewe, bali kwa ajili yake yeye aliyekufa akafufuka kwa ajili yao.” 2 Kor 5:14
Tungelikuwa tunaishi mara mbili angalau mtu angeweza kutumia awamu ya kwanza kuishi kwa ajili yake mwenyewe na awamu ya pili kuishi kwa ajili ya Yesu Kristo. Kizuri zaidi ni kwamba, tunaishi mara moja, hakuna mtu mwenye awamu mbili za maisha. We live only once!
Katika kuishi kwetu mara moja ni lazima mtu aamue kuishi kwa ajili yake mwenyewe au kuishi kwa ajili ya Kristo. Wewe unaishi kwa ajili ya nani? Wako wanaoishi kwa ajili ya kazi zao, wako wanaoishi kwa ajili ya michezo, wako wanaoishi kwa ajili ya burudani na wako wenye hekima wachache wanaoishi kwa ajili ya Kristo.
Oswald J Smith mwandishi wa kitabu nilicho kisoma na kukirudia zaidi ya mara mbili, “The Consuming Fire” anasema, “I have only one life to live and I want to invest it for Thee” kwa tafsiri yangu, “Nina maisha haya tu, ninataka niwekeze kwa ajili yako BWANA”
Katika mstari unaotuongoza pale juu 2 Kor 5:14 Paulo Mtume anasema wazi Yesu anatutaka tusiishi kwa ajili ya nafsi zetu wenyewe bali kwa ajili yake. Jiulize, unaishi kwa ajili ya Kristo au kwa ajili yako mwenyewe?
Asubuhi mpaka jioni unafanya nini? Wanaoishi kwa ajili ya Kristo huomba kwa saa moja na kusoma neno kwa angalau saa moja. Pesa zako zinatumikaje? Wanaoishi kwa ajili ya Kristo hutumia pesa zao kwa uinjilishaji. Luka 8:3
Nakualika ujitoe kwa Yesu na kuishi kwa ajili yake kuanzia leo: Sema sala hii, “Ee BWANA YESU mimi ni mwenye dhambi na wewe ni mwokozi wangu. Naomba unisaidie kuanzia leo niyatoe maisha yangu kwako, wala nisiishi tena kwa ajili yangu na kwa ajili ya Dunia badala yake nikufuate wewe milele. Amina.”
Nakutakia msimu mwema wa sikukuu, Shalomu….
>

0 comments :