Ni lazima kukua

5:46:00 PM Unknown 0 Comments

NI LAZIMA KUKUA.
Mwenyehekima mmoja amewahi kusema, ukuaji [wa mwili] ni jambo la asili; lakini maendeleo ni matokeo ya maamuzi ya mtu (Growth is natural but development has to be intentional). Hakuna mtu amewahi kuendelea kwa bahati mbaya [accidentally]; iwe ni kiroho, kiuchumi, kiuongozi n.k! Mpaka mtu ameamua [nuia] kuendelea katika eneo fulani, atabaki katika hali ile ile. Kanuni hii inafanya kazi kwa mtu mmoja mmoja, jamii hata taifa.
Nimewahi kusoma makala katika gazeti moja, ambapo mchambuzi alikuwa akieleza ni kwa namna gani bara la afrika linaweza kujifunza kutoka nchi ya China katika vita dhidi ya umasikini. Anasema mwaka 1966, China haikuwa na uwezo wa kuzalisha chakula cha kutosha watu wake lakini leo hii inauwezo wa kuzalisha chakula cha kutosha watu wake na kuuza nje ya nchi. Kumbe, kila mtu au jamii au taifa, lazima kwanza linuie kuendelea [Develop] katika eneo mahususi [specific] vinginevyo maendeleo hayawezi kutokea. Jambo kubwa tunalotaka uelewe hapo ni kwamba, kila mtu anawajibika binafsi katika kuhakikisha anapiga hatua kubwa ili leo iwe bora kuliko jana, na kesho iwe bora kuliko leo.
“Nilipokuwa mtoto mchanga, nalisema kama mtoto mchanga, nalifahamu kama mtoto mchanga, nalifikiri kama mtoto mchanga; tokea hapo nilipokuwa mtu mzima, nimeyabatilisha mambo ya kitoto” 1Kor 13: 11
Wataalamu wanasema, “kwa siku mwanadamu anafanya maamuzi karibu elfu kumi [10,000]” kwa mawazo ya haraka haraka unaweza ukaona kwamba chaguzi hizo {decisions} ni nyingi  kwa sababu tu tunapofanya maamuzi hayo hatufikiri sana. Si wengi wanaofikiri sana kwa nini hawakui, si wengi wanafikiri sana kwa nini ubora wao hauongezeki, si wengi wanaowaza kuhusu ubora wa afya zao. Kila kitu ni uchaguzi wako, hata wokovu ni matokeo ya uchaguzi na uamuzi wako. Aliandika Mt Agustino anaandika: “Mungu ambaye amekuumba bila kutaka, hawezi kukuokoa bila kutaka.”
Ili kukua ni lazima uchague maeneo ambayo unataka uone ukikua katika mwaka husika. Ukuaji lazima uzingatie muda, One day at a time! Maeneo yafuatayo ni muhimu kwa ukuaji wako:
  1. - Kitaaluma-Unaweza kusema mwaka huu lazima nisome shahada ya uzamili au ya uzamivu na ukatekeleza
  2. - Kiroho- Ni muhimu uwe na shauku ya kukua ili kufanana na Yesu. Yeye ni nuru hivyo ni lazima uwe nuru pia, yeye ni Mtakatifu na hivyo ni lazima uweke mkakati wa kuwa mtakatifu pia. 1 Yohana1:5-6
  3. - Kiuchumi- Mkakati wa kuongeza kipato na uwekezaji ni muhimu ufanyike kwa kuzingatia muda. Ni muhimu kuweka nia ya kuanzisha mradi au kuwekeza katika biashara ili kujiongezea kipato.
  4. - Sayansi na Teknohama- Ni lazima kila unachokifanya uchanganye na sayansi na teknolojia. Angalau ujue Microsoft Word, Power Point, Excel nakadhalika. Sayansi ya usindikaji ni muhimu ili kuongeza thamani ya bidhaa ghafi na mazao. Ukiipenda teknolojia utafanikiwa, mitandao ya kijamii pia ikitumika vizuri inaweza kukutangaza na kukupa fursa ya kipawa chako.
  5. - Kipaji chako- Kama unaimba basi ungalau jifunze pia kupiga hata chombo kimoja cha muziki, nenda chuo kinachokuza kipaji chako. Soma vitabu vinavyotoa mwongozo wa kipaji chako.
Mchakato wa ukuaji, unakutaka ukubali baadhi ya mambo, na ukatae baadhi ya mambo ili nguvu zako zielekee katika jambo moja. Ili kukua kwa haraka ni lazima ujifunze kuwa mtu wa jambo moja, bobea katika jambo moja, zamia kabisa katika fani yako. Hakikisha unakuwa na misuli katika kipaji chako hata watu wakutambue kama guru na kisha ujenge ufalme wa Mungu kwa kipaji hicho. Tukutana kileleni…..

0 comments :