Unataka kufanikiwa katika nini - II?

9:30:00 AM Unknown 0 Comments

UNATAKA KUFANIKIWA KATIKA NINI - II?
“Success is predictable, so is the failure”
Kiwango cha mafanikio ya mtu katike eneo lolote hutegemea kiwango chake cha maarifa sahihi, ufahamu na utendaji kazi wa kanuni zinazoleta mafanikio katika eneo hilo. Toleo la kwanza katika mfululizo huu tuliangalia kanuni/ mambo mawili; Na leo nataka tuangalie mambo mengine mawili:
a.    Je, unaona au unaliona (ndani yako) jambo hilo unalotaka kufanikiwa au kufanikisha (Do you see it)?
Mpaka umeliona jambo hilo waziwazi ndani yako, hautaweza kulimiliki/ kulifanya kuwa dhahiri. Kwa kadri unavyoona ndivyo unavyoongeza eneo la umiliki wako yaani uwezekano wa kulifanikisha jambo hilo au kufanikiwa katika eneo hilo. “Maana nchi hii yote uionayo, nitakupa wewe na uzao wako hata milele”. Kipimo cha Ibrahimu hakikuwa kwa Mungu aliyeahidi, kilikuwa katika uwezo wa macho yake kuona. Mungu hakumuwekea mipaka; mipaka iliwekwa na macho yake. “Inua macho yako ukatazame kutoka hapo ulipo”. (Mwanzo 13:14-15, 17)
Ukitazama kutoka hapo ulipo (ambapo unachotamani na kutaka kufanikisha kipo kama wazo tu kwenye maandishi/mchoro) unaiona hiyo nchi? Je unajua ya kuwa unajua ya kuwa unaweza kufanikiwa au kufanikisha jambo hilo uliloliandika? Kuandika ni jambo moja, na kujua ndani yako kuwa unaweza (confidence) kufanikiwa/kufanikisha ni jambo lingine. Kumbuka, tunapewa au tunapata kile tunachokiona. Habakuki aliambia, “Ukaifanye kuwa wazi sana…” Mpaka macho yako yameona (wazi wazi) kwanza, hautaweza kumiliki kikamilifu. Kwa kadri unavyoona vizuri ndivyo unavyoweza kutembea kwa kasi kufikia mafanikio yako (The more clearer you can see it, the greater the speed of delivery).
Warren Baffett, anasema kabla hajawa tajiri aliona (he saw it clearly) atakuwa tajiri, wala hakuwa na shaka hata dakika moja. “I always knew I was going to be rich. I don’t think I ever doubted it for a minute.” –(“Siku zote nilijua kuwa, nitakuwa tajiri. Sidhani kama nimewahi kuwa na mashaka juu ya hilo (ndani yangu) hata kwa dakika moja”: Tafasiri isiyo rasmi). Mwanadada Emma Wenani anasema, “Deep down, I always knew I would be successful” (“Ndani kabisa ya moyo wangu, nilikuwa najua nitafanikiwa”: Tafasiri isiyo rasmi). Ndani ya moyo wako unaona nini? Unachoona ni muhimu sana, kwa sababu kinaweza kukukwamisha au kukufanikisha.
b.   Tafuta maarifa, elimu na ufahamu wa ‘kutosha kuanza’ jambo hilo/ kuhusu eneo
Kabla ya kuanza jambo lolote lenye maana, ni muhimu kuwekeza katika kupata maarifa sahihi na ufahamu wa kutosha kukusaidia kuanza. Kiwango chako cha mafanikio katika eneo lolote hutegemea kiwango chako cha maarifa na ufahamu uliona nao kuhusu eneo/jambo hilo; iwe kiroho, kimwili, kifedha au kiuchumi, familia, huduma, mradi, uwekezaji n.k. Unapopata maarifa sahihi ya kukuwezesha kuanza matokeo huwa dhahiri. Mfano. Usianze mahusiano, au ndoa, biashara, kilimo, mradi au uwekezaji wowote ule kama huna maaarifa sahihi na ufahamu wa kukusaidia kuanza vyema; Don’t start blindly. Hili litakuepusha na  msongo wa mawazo (stresses and depressions) pamoja na gharama nyingine nyingi sana kama vile muda, fedha n.k. Ukianza bila kuwa na maarifa na ufahamu wa kutosha uwe na uhakika jambo hilo halifiki mbali au litakugharimu sana. Kumbuka, Mpaka akili imetoka jasho, hautaweza kuona wepesi (Until your brain sweat; you won’t experience swiftness).
Japo kujifunza ni jambo endelevu, lakini ni muhimu kuhakikisha kabla ya kuanza jambo lolote unapata maarifa yaliyo sahihi yatakayokusaidia kuanza vyema. Unataka kuona wepesi katika ndoa, uhusiano, huduma, biashara, kilimo, mradi au uwekezaji wowote ule? “Yale uliyoyaona kwa macho, usitoke nje kwa haraka ili kuyashindania; usije ukakosa kujua la kutenda hatimaye...” (Mithali 25:7c-8)
There’s a place for you at the top!

0 comments :