Je hamkusoma?

2:24:00 PM Unknown 0 Comments

 
JE, HAMKUSOMA?
(Mathayo 19:4-6)
Matatizo mengi katika maisha ya mwanadamu ni matokeo ya semina alizokataa kwenda na vitabu alivyokataa kusoma. Askofu David Oyadepo anasema, “Kabla hujaoa au kuolewa jitahidi angalau (at least) usome vitabu (50) hamsini kuhusu mambo ya mahusiano na ndoa”. Ni wachungaji wachache wako tayari kuusema ukweli huu mchungu, matatizo ya ndoa ni matatizo ya maarifa.
Kuna nyakati mchungaji wetu mkuu yaani, Yesu Kristo alihojiwa kuhusu matatizo ya ndoa, naye bila kumumunya maneno alisema, ni matatizo ya kutokusoma. Aliwajibu akawaambia, “….Hamkusoma ya kwamba….” Mathayo 19:4
Wangesoma wangejua. Atakachofanya shetani si kukuzuia usiolewe, bali atakuzuia usisome. Mafundisho ya wiki mbili, mwezi mmoja au mwaka mmoja hayawezi kusaidia, ni lazima usome. Talaka, ugomvi, watoto wa mtaani na jamii zisizo na maadili zote zinasababishwa na jambo moja, ukosefu wa maarifa. Nikiwa chuo kikuu mzumbe nilimweleza rafiki mmoja, kama hauko tayari kusoma hauko tayari kuishi.
Sasa unaweza ukaelewa kwa nini watu wana wake wengi, sasa unaweza ukaelewa kwa nini watu wana waume wengi, sasa unaweza ukaelewa kwa nini makanisa ya leo yameanza kuongeza muda wa mafundisho. Ni kwa sababu ya ukosefu wa maarifa, hawakusoma!
Hakuna familia bila msamaha, hakuna ustawi kama familia itakuwa kipaumbele cha pili. Kuna ndoa za kibudha, ziko za ki-mila, na ziko za kiserikali. Kila hiyo inakanuni na taratibu zake, lakini ni zile zinazofungwa kwa mtazamo wa falsafa ya Yesu Kristo ndizo zitakazo weza kuleta maana kwa dunia hii. Ni familia hizo ndizo zitaleta ufalme, watoto watakao mtisha shetani badala ya kumwogopa, watoto watakao tumia ustadi na akili zao kwa maendeleo ya kudumu ya jamii zao. Si tu kwamba umezaa mtoto bali umemzalia nani, Mungu au shetani, mbingu au Jehanamu?
Bila ya mama, ni bila ya upendo; na bila ya baba, ni bila ya ulinzi, vyote havikuachi salama. Nimewasikiliza wachungaji zaidi ya 8 katika jambo hilo wote wanasema mambo haya kwa pamoja; 1. Uzuri au utanashati unadanganya bali chagua mtu amchaye BWANA, 2. Usioe kabla hujajua makusudi ya kuumbwa kwako, 3. Kazi kwanza ndoa baadaye yaani, usiolewe na mtu asiyejituma kufanya kazi hata ndogo ndogo, 4. Usioe nje ya kanisa, zamani watu walirudi kwao sasa hivi ni kanisani yaani, mtu aliyemwamini Kristo na kuokoka, 5. Usiwe na haraka, “don’t rush”, 6. Usipuuze ushauri wa jamii kuhusa ushuhuda wa huyo mtu, 7. Fuata sifa ulizojiwekea na si umbo na muonekano, review your checklist, 8. Oa chagua la Mungu na si chagua lako.
Nilisikia kwa Benny Hinn na Sunday Adelaja wakisema, “Mary God’s choice and not your choice” yaani “uungane na mtu ambaye Mungu amekuchagulia na si ambaye wewe umemchagua”. Hii hupelekea mtu kuomba sana na kusoma sana. Katika maombi Mungu atakuongoza, na katika neno Mungu atakuangazia, kwa kuwa neno ni taa. Taa ikiangaza ni rahisi kuona na kuwa na hakika na salama.
Kwa muhtasari, soma kabla ya kuingia katika uhusiano, lijue kusudi la kuumbwa kwako kabla ya kuingia kwenye uhusiano. Unaweza pia kuagiza kitabu cha, “Si kwa tamaa, bali kwa upendo” ni kizuri na kinapatikana kwa namba zetu. Barikiwa….

0 comments :