Ongeza maarifa katika eneo maalum

5:37:00 PM Unknown 0 Comments

ONGEZA MAARIFA KATIKA ENEO MAALUMU
Kama ilivyo kawaida, mwanzoni mwa mwaka kila mtu anaweka malengo yake au mambo anayotaka afanikiwe au afanikishe katika kipindi cha mwaka huo. Pamoja na kwamba si kila mtu ana utaratibu wa kuandika malengo yake ya mwaka, lakini karibu kila mtu huwa na malengo au mambo analiyopanga kufanikisha katika mwaka.  Nafahamu baadhi yetu tumeweka malengo ya kusoma vitabu katika mwaka huu mpya (kama hujaweka lengo la kusoma vitabu, basi hujachelewa kufanya hivyo), hili ni jambo jema kwa kila mwenye uwezo wa kusoma.
Pamoja na mipango na malengo yako mengi uliyojiwekea kwa mwaka huu mpya, leo nataka nikupe hamasa juu ya jambo moja, nalo ni kuweka nia au malengo ya kuongeza maarifa/ujuzi na ufahamu katika eneo mahususi au maalumu katika maisha yako. Yaani badala ya kuweka lengo la kusoma tu, weka pia ni eneo gani unalotaka kuongeza ujuzi au maarifa ili kuliboresha.
Mwenyehekima mmoja amewahi kusema "Usishibishe njaa yako, shibisha maono yako [don’t feed your hunger, feed your vision]"; huu ni ushauri mmoja wa hekima ambao nimewahi kuupata kuhusu usomaji katika kuishi kwangu. Lengo hapa ni kukuepusha na tabia ya kusoma kila kinachokuja mbele yako bila malengo mahususi wala mpangilio utakao kusaidia kupiga hatua zaidi katika maisha ya kila siku. Mtu anaweza kupanga mwaka huu nataka nisome vitabu 30 au 20, lakini ukimuuliza unataka kusoma kuhusu nini au kuhusu eneo gani, ni wachache sana wanamajibu yanayoeleweka (concrete answer)
Ili kusoma kwetu kulete badiliko katika maisha yetu na mazingira tuliyopo ni muhimu ukachagua cha kusoma ukilenga kuboresha eneo mahususi katika maisha yako. Na hapa utapata fursa ya kufanya tathmini kuona kama unasogea, na kama kusoma kwako kuna kuletea faida inayoweza kupimwa [measurable results].
Kumbuka, huwezi kusoma vitabu vyote vilivyoandikwa, hivyo basi lazima ujue nini cha kusoma na nini cha kuacha hata kama kina sura nzuri, ili mwisho wa mwaka useme kwa kusoma vitabu au kwa kujifunza ujuzi fulani nimepiga hatua hii; kiuchumi, kiroho, mahusiano, ufanisi kazi, huduma, ubora wa kazi zangu n.k
There’s a place for you at the Top

0 comments :