Roho ya Batromayo Kipofu

10:25:00 PM Unknown 0 Comments

 
ROHO YA BATROMAYO KIPOFU
“ONA FURSA”
Batromayo aliona watu kama miti. Watu wengi wanasumbuliwa na roho hii hawaoni picha halisi, picha yao haijatulia. Ni kama vile ungo wao wa kudakia mawimbi haujatulia, hawapati picha halisi. Ni muhimu sana mwaka huu 2018 sote tumuombe Mungu afungue macho yetu tuweze kuona fursa!
Kwa uzoefu mdogo nathubutu kusema, “fursa haziwezekani bila imani”. Macho ya mwili hayotoshi, ile kwamba macho yetu yanaona taa za barabarani na tunavuka salama haina maana kama tunaona fursa pembezoni mwa barabara. Mtu anayeweza kufikiri kimkakati “strategic thinking” anaweza kuona fursa na kuzitumia. Kufikiri kimkakati kutakuwezesha uone miaka kumi ijayo na zaidi.
Kwa kukosa imani watu hauza mambo ambayo baadaye yangekuwa fursa kubwa, kwa uhaba wa imani watu huogopa kuanza jambo ambalo halijazoeleka. Anayewekeza miaka mia moja ijayo anaamini kwamba, Mungu atamlinda na kumpa uhai, ndani yake mtu huyo hamna hofu ya kifo. Fursa inataka imani katika sura tatu, kwanza mwamini Mungu muumba wako, jiamini na kisha amini wazo lako.  Adui mkubwa wa fursa ni hofu, uwekezaji unakwenda na ujasiri.
Zamani walituambia, “wasiwasi ndio akili” si kweli. Nenda msituni utagundua mnyama mfalme wa msitu ni simba ambaye ni mnyama jasiri. Njoo duniani utagundua mataifa makubwa yana ujasiri mkubwa pia. Alisema msemaji wa Marekani wa mambo ya nje wakati huo John carry, “Dola ya Washington haitatikisika” alisema hayo kwa ujasiri sana akionya taifa moja alilolitazama kama adui. Hatuna sababu ya kuogopa amesisitiza Shiv Khera katika kitabu cha, Unaweza Kushinda: “Losers want security, winners seek opportunity. Losers more afraid of life than death…”.
Tunawezaje kuona fursa? Maana kama hatukuijua fursa kabla ya kukutana nayo, siku ikitokea tutaiona kama mkosi. Lazima ujifunze kuhusu fursa na uzifahamu ili siku ukikutana nayo uitambue kirahisi. Wewe si tajiri ila jitahidi usome kuhusu utajiri. Leo wewe si mfanya biashara lakini jitahidi kusoma na kujifunza kuhusu biashara. Soma wasifu wa wafanya biashara kama; Mohamed Dewji, Warren Buffet, Reginard Mengi, Ratan Naval Tata, Alhaji Dangote, Said Bakhresa na wengine wenye ushawishi kwako.
Watu wengi wanapenda kushinda ila ni wachache tu ambao wanapenda maandalizi kwa ajili ya kushinda. Fursa zinakutaka ufanye maandalizi. Wewe ndiye unapaswa kuisubiri fursa kwani fursa haina nafasi ya kumsubiri mtu! Fursa huja kwa waliojiandaa. Preparation is the Key!
Sala: Ee Mungu Baba Muumbaji wetu, utufungue macho ili mwaka huu 2018 sote kwa umoja wetu tuweze kuona fursa. Katika Jina la Yesu Nimeomba. Amina.
Usisite kutuandikia kwa anuani yetu kwa maoni, ushauri na maombi. Barikiwa!

0 comments :