Kama si Kompyuta Basi ni Roboti

9:56:00 PM Unknown 0 Comments

 
KAMA SI KOMPYUTA BASI NI ROBOTI
(Tumia akili yako kufikiri vema)
Dunia iko kwenye kasi kubwa ya mabadiliko ya sayansi na teknolojia. Mabadiliko haya ni muhimu sana, nchi ambazo ziko mbele katika mabadiliko haya watu wake huishi maisha marefu. Si ajabu kwa Japan, Korea kusini na Kaskazini raia wake kuwa na wastani wa umri mrefu wa kuishi. Mabadiliko haya humpa mwanadamu muda wa kupumzika kwa kuwa humwondoa kwenye majukumu ya kutumia nguvu na kumwachia jukumu zito la kufikiri. Sayansi na teknolojia ni muhimu katika afya ya binadamu, usindikaji na ujenzi wa miundombinu.
Kazi kubwa ambayo mwanadamu anapaswa kubaki nayo ni kufikiri. Mabadiliko na mapinduzi hayawezi kutokea ikiwa hatukupindua sehemu iliyoko katikati ya sikio la kulia na sikio la kushoto yaani, ubongo. Kazi za mazoea kama vile kubeba mizigo, kubaki mizigo, kuandika hati, kusikiliza na nyinginezo zifananazo na hizi zinaweza kufanywa vizuri kama sina kompyuta basi ni roboti.
Hivi karibuni Japan wamezindua roboti ambaye huangalia watoto nyakati za usiku. Bila shaka roboti huyu akifika Afrika atanyang’anya kazi za watu wengi katika shule na maeneo ya malezi ya watoto. Kupitia masomo ya walimu wabobezi yaliyoko mitandaoni, “you tube” na katika maeneo mengine ya kuhifadhia itafika mahali hatutahitaji tena kukutana na mwalimu ana kwa ana. Mungu alitaka tuishi kwa kufikiri, tutumie utashi wetu. Kufikiri hakupitwi na wakati, mwenye fikra njema anaweza kushinda kipimo cha muda (time test).
Tabia za mazoea na kazi za mazoea ni rahisi kufanya kwa kutumia teknolojia pasipo kumhitaji mtu awaye yote. Tabia hizi za mazoea huua ubunifu na uwezo wetu wa kufikiri. Wastaafu wengi wanaotoka kwenye kazi zisizosumbua ubongo hushindwa kumudu maisha mapya ambayo huhitaji fikra mpya na mawazo mkakati. Fedha yao ya kustaafu huwa kama magurudumu mapya katika injini iliyoharibika kabisa. Ni wazi Teknolojia inawafukuza watu wengi kazini kuliko tumbua tumbua ya vyeti feki. Uzuri wake ni kwamba inarahisisha utendaji na ina ajiri watu wengi zaidi wanaoifahamu zaidi ya wale inaowafukuza.
Ni muhimu tuusukume ubongo na ufahamu wetu ili tupate mawazo na fikra endelevu za kutuwezesha kwenda sambamba na sayansi na teknolojia. Ni muhimu kukumbatia teknohama kuliko shahada za vyuo vikuu. Nchi za wenzetu zinapunguza udahiri vyuo na zinahimiza ufundi ili tu zikuze ujuzi na matumizi ya sayansi na teknolojia katika maisha ya kila siku.
Ile kwamba, mtakula kwa jasho haikuzuii kufunga kiyoyozi na kula kwa damu ya Yesu iliyovunja laana zote. Jasho ni matokeo ya ugumu wa kazi ni muhimu fikra zetu zituletee njia rahisi, zenye kugharimu muda mchache, rasilimali chache na ubora wa juu. Tukutane katika msimu mpya wa Weekend of Purpose. Barikiwa!!  

0 comments :