Mtu mgumu kutawalika

2:17:00 PM Unknown 0 Comments

 
MTU MGUMU KUTAWALIKA
Ni rahisi sana kutazama wengine na sisi wenyewe tukasahau kujitazama na kujitathmini. Tunaweza tukayajua sana mapungufu ya wengine na tukasahau wapi tunapungua. Imenenwa, “Unakiona kibanzi kwenye jicho la nduguyo na unaacha kutazama boriti ndani ya jicho lako”.
Profesa na Mhadhiri wa chuo kikuu cha Havard cha Nchini Marekani bwana Bill George anaandika hivi katika moja ya vitabu vyake, “The hardest person you will ever have to lead is yourself”.
Wewe ndio mtu usiye tawalika, wewe ndio mtu mgumu kwa viongozi wako. Mara nyingi tumezoea kusema ni fulani na kujisahau kwamba, tunayo mapungufu makubwa. Kwangu mimi mtu mgumu kumtawala ni mimi, na wewe ni vema ujijue vema.
Miili yetu inaasili ya kutokutawalika. Ukipanga mpango wa kuacha michepuko unaweza kushuhudia vita dhahiri ambayo mwili unainua, hali kadhalika unapopanga kufunga. Biblia inasema, “Ifungeni dhabihu kwa kamba kando ya madhabahu”. Imenenwa pia, “Itoeni miili yenu kama dhabihu”. Kwa nini sadaka ifungwe kwa kamba? Isipofungwa itagoma au itakimbia. Isipofungwa haitawaliki.  Warumu 12:1-3
Kufungwa ni kulazimisha, kutia adabu, kufanya tena na tena mpaka maadili mema na utii uwe sehemu ya maisha yetu. Ni ngumu ni lazima ukaze. Wachichanji wanajua, ili uchinje nguruwe unahitaji kufanya kazi, ili utoe fungu la kumi unahitaji kujua kuacha matamanio binafsi na kuwa mtii kwa Bwana.
Tukutane juu.

0 comments :