Uzuri unadanganya

10:08:00 AM Unknown 0 Comments

UZURI  UNADANGANYA.
(Beauty is fleeting)
Nimewahi kupewa ushauri kutoka kwa watu mbalimbali kuhusu masuala ya mahusiano na ndoa. Nimejitahidi pia kusoma walau vitabu kadhaa. Yote kwa yote kuhusu ndoa na mahusiano sitasahau ushauri huu, “uzuri/urembo unadanganya.” Kwa nini unadanganya? Kwa sababu si wa kudumu, na si kitu utakachokihitaji kila siku.
Si vema kumpuuza mtu mwenye hekima anapofumbua kinywa chake kusema kitu. Solomon mtu mwenye hekima sana ndiye aliyesema katika Mithali 31:30, “uzuri si wa kudumu” Yaani sura, mpangilio wa meno, rangi na umbo zuri havisemi kweli maana baada ya muda mtu huzeeka na ngozi hukunjamana, na mara urembo wote hutoweka. Maana yake uonavyo leo sivyo itakavyokuwa milele. Kwa lugha nyingi si mambo utakayoyahitaji baadaye. Baada ya muda kupita utagundua haukuhitaji sura bali ulihitaji, upendo, ushirika, amani na uaminifu. Kwa nyakati tofauti wachungaji na wenye hekima wameonya kwamba,kufanya uamuzi kwa kujali mwonekano wa nje ni hatari.
Amesema mwenye hekima huyu, “Mwanamke aliye na umbo zuri na sura nzuri pasina maarifa kichwani afaa kwa usiku mmoja, lakini yule mwenye ufahamu na maarifa afaa kwa maisha yote.” Ndoa ni agano la maisha si la usiku mmoja. Mwonekano wa nje hautoshi kutoa taswira ya ndani ya utu, uchapakazi, uaminifu na upendo.
Urembo ukisimama peke yake hautoshi, utanashati peke yake hausaidii. Haipasi kuwa urembo na utanashati, badala yake inafaa kuwa urembo na akili, urembo na uchapakazi, urembo na ibada, urembo na upendo, urembo na uaminifu.
Ili urembo usikudanganye basi ni lazima uwe umeujua ukweli. Tafuta watu wanaoheshimika utagundua si kwa rangi zao wali si kwa urembo na utanishati wao bali ni kwa kujitoa sadaka, kuishi maisha ya heshima, uaminifu na utu wema.
Wewe si Mr. Tanzania unaanzaje kuoa Miss Tanzania? Urembo unadanganya. 
Tukutane kileleni………

0 comments :