Chagua kuendelea mbele

12:52:00 PM Unknown 0 Comments

 
Chagua Kuendelea Mbele
Mara nyingi tunapokutana na changamoto katika kufikia yale tuliyopanga au kutazamia; tunaweza kuchagua mambo mawili tu, kusonga mbele au kukata tamaa na kutafuta sababu ya kulaumu na kughairi kuendelea mbele! Kile utakacho kiamua baada ya kukutana na changamoto ndicho utakachokipata baada ya changamoto hiyo kupita.
"Ukifikiri kama unaweza au hauwezi, upo sahihi "
Yaani ukifikiri na kuona kama jambo fulani unaliweza au utaweza basi ujue upo sahihi; na ukiona au kufikiri jambo fulani hauliwezi au hautaliweza basi ujue upo sahihi pia!  Na hii ndio sababu inayofanya wengine waendelee mbele na wengine kuishia kulalamika na kughairi kuendelea 'utukufu' ulio mbele yao
" Bwana akamwambia Musa, Mbona unanililia mimi? Waambie wana wa Israeli waendelee mbele" Kutoka 14 :15
Siri ya kufanikiwa wakati wa changamoto sio kurudi nyuma au kukata tamaa, siri ya mafanikio ya kweli ipo katika kuendelea mbele. Thomas Edison, mwanasayasi na mgunduzi amewahi kusema "Our greatest weakness lies in giving up. The most certain way to succeed is always to try his one more time " (Udhaifu wetu mkubwa upo katika kukata tamaa; njia ya uhakika kufikia mafanikio ni kujaribu mara nyingine: Tafsiri isiyo rasmi)
Kumbuka jambo hili, Haukuanza ili uishie njiani! Ndio, narudia tena haukuanza ili uishie njiani hivyo chagua kuendelea mbele. Mwenye hekima mmoja amewahi kusema, unapochoka usiache (usikate tama); jifunze kupumzika (ili upate nguvu ya kuendelea). Don't stop because you're tired, stop when it's done!
There's a place for you at the top

0 comments :