Umeitwa kuongoza

10:03:00 AM Unknown 0 Comments

UMEITWA KUONGOZA
Mtu hafanyiki kiongozi kwa cheo au nafasi aliyonayo katika Nyanja za siasa, taasisi, kanisa n.k; bali ni kusudi (purpose) linalozaa maono (vision) ndani yake. Sifa kuu ya kiongozi ni kuwa na maono chanya kwa mustakabali wa anachokiongoza. Mahali ambapo hakuna maono hakuwezi kuwa na uongozi, kunaweza kuwa na cheo lakini hakuna uongozi!.
Maono ndio hufanya kiongozi awe kiongozi. Siku zote watu hawafuati mtu, wanafuata maono yake. Mahali ambapo nguvu hutumika ili kufanya watu wafuate (follow) ni kwa sababu hakuna maono yanayoshawishi watu kufuata kwa utashi na hiari yao.
Ikiwa kila mtu ameumbwa kwa kusudi maalumu, basi ni ukweli uliowazi kuwa kila mtu ameitwa kuongoza katika eneo la kusudi lake; kumbuka maono ndio yanayotengeneza kiongozi na sio kinyume chake, na maono ni picha ya kusudi ndani ya mtu. Maono ndio yaliyotengeneza mtu anaitwa mama Theresa, Nelson Mandela, J. K. Nyerere, Martin Luther King Jr n.k. Maono ndio yanayotengeneza makampuni, mashirika, taasisi, ajira kwa watu, biashara, miradi (projects) na sio kinyume chake. 
Ninaposema kila mtu ameitwa kuongoza sina maana kila mtu ameitwa kuwa mwanasiasa (wapo waliokusudiwa hapa pia); na wala si swala la kuwa na cheo au kutokuwa nacho! Bali kwa kuwa umeumbwa kwa kusudi fulani, inatosha kujua mahali uongozi wako unahitajika. Uongozi wako unaweza hitajika kwenye eneo la biashara, eneo la tekinolojia, eneo la sanaa na michezo, eneo la siasa, jamii (social leader), afya, uchumi au madhabahu! (Your area of gifting and passions)
Kwanini nasema umeitwa kuongoza? Kwa sababu maono hutolewa kwa mtu mmoja kwanza kabla hayajapata wafuasi wengi; Na pia kila mtu ana eneo au nafasi yake kwa kadri ya kusudi la kuumbwa kwako sawasawa na maono aliyonayo; Ni kwa sababu ulichopewa si kwa ajili yako, ni kwa ajili ya wengine (japo na wewe utanufaika), mfano. Mwalimu hawi mwalimu kwa ajili yake, japo hupokea malipo ya kazi hio!  Kumbuka, hakuna mti unakula matunda yake wenyewe!!
There's a place for you at the top

0 comments :