Ndio maana haukuweza

11:45:00 AM Unknown 0 Comments

 
NDIO MAANA HAUKUWEZA
Zingatia Uhalisia Gal 6:7
Imewatokea wengi kushindwa kufikia malengo, ni jambo la kawaida kwa wengi kushindwa kupungua uzito, si ajabu kwa wanafunzi kufeli mtihani. Kila unaposhindwa jitahidi kurudi kwenye misingi. Wakristo wengi wameanguka katika dhambi na kwao ni muhimu kurejea katika misingi.
Mambo hayatokei yenyewe tu, na kama wakristo tunahitaji miujiza na si maajabu. We need miracles not magic! Maajabu yako hata kwa waganga wa kienyeji, maajabu ni kupata pesa bila kufanya kazi, kufaulu bila kusoma, kahaba kuolewa au asiyehaki kuinuliwa. Ni ajabu kwa anayekula kupita kiasi kupungua uzito.
Miujiza ni tofauti na maajabu. Miujiza inakutaka ushirikiane na Mungu, miujiza inatualika tuungane na Mungu. Miujiza ni mchanganyiko wa sala na kazi, pia miujiza ni mchanganyiko wa imani na matendo. Miujiza hutokea pale watu wanapoamua itokee. Amesema Joel Osteen “Ni imani yetu ndiyo huamsha nguvu ya Mungu”.
Ili muujiza utokee lazima pawepo na imani, sala, mafungo, bidii ya kazi upendo na amani. Upendo unachagiza sana uwepo wa muujiza. Ofisi ambayo upendo umetawala watu watamaliza kazi kwa wakati (finishing before deadline). Maajabu hutokea tu bila sababu, lakini miujiza inahitaji muda, uwekezaji, bidii na upendo. Mungu wetu ni mtenda miujiza (miracles) si maajabu (magic). Kama hauna muda na mpenzi wako usitarajie muujiza wa amani na upendo bali tarajia maajabu ya amani na upendo. Galatia 6:7
Maajabu yanafanya muuzaji mwenye lugha mbaya apate wateja, muujiza hutokea pale muuzaji mwenye busara na kauli nzuri anapopata wateja wengi na kuuza sana sana. Waganga wa kienyeji (chief magic promiser) hawakufundishi huduma nzuri kwa wateja bali wanawahadaa wateja na kufanya upate usichostahili. Usiende kwao, wala kwa wasoma nyota. Wagalatia 6:7
Hata biblia imekataa, kuvuna usipopanda, kupewa usichoomba, kupata usichostahili. Wengi tunao ujuzi wa kutufikisha kileleni, lakini hatuna maarifa ya kutufanya tudumu hapo. Haifai kupenda kuona maajabu. Maajabu hayawezi kudumu maana hata hatujui kwa nini hutokea. Lakini muujiza wa Yesu ukitokea na sisi tunajua tukitimiza yanayotakiwa utatokea tena. Siku moja mpwa wangu alimuona Pastor Chris akiwapuliza watu wanaanguka baadaye na yeye akafanya na akapata matokeo yale yale. Siku za mbeleni nami pia katika kuombea watu nikafanya nikapata matokeo yale yale.
Ushindi ni tabia, mafanikio ni tabia pia. Soma biblia na tazama tabia za waliotendewa miujiza utakuta zinafanana. Si rahisi kuushinda ulimwengu kama bado haujajishinda mwenyewe, si rahisi kuaminiwa na watu ikiwa bado haujimini wewe mwenyewe. Madhara ya kutokujiamini ni sawa sawa na kutokumwamini Mungu.
Batromayo kipofu alihakikisha anapaza sauti na Yesu akamsikia licha ya kelele za umati mkubwa, Zakayo alipanda juu ya mti ili amwone Yesu, mama aliyetokwa na damu alipenya katika ya kundi la watu maana haikuwa rahisi kumgusa Yesu. Muujiza unataka ujipange, uwe juu ya viwango vya watu, muujiza utataka upige kelele mpaka Yesu asikie, muujiza unataka upenye katikati ya watu katika usaili.
Mara ya kwanza ulipoimba vizuri Mungu alitaka ujue kipaji chako, pale ulipohubiri vizuri Mungu alitaka ujue wito wako, pale ulipotengeneza bidhaa nzuri Mungu alitaka ujue kazi yako lakini utambulisho huo haukusaidii kama hautendi hivyo mara kwa mara. Kwa mshindi kushinda ni mazoea, kipaji chako kikiwa tabia yako hapo utadumu. 
Wiki hii ikawe mwanzo wa miujiza katika maisha yako katika jina la Yesu Kristo. Amen

0 comments :