Changamoto kwa viongozi vijana

2:09:00 PM Unknown 0 Comments

 
CHANGAMOTO KWA VIONGOZI VIJANA
(Usimzuie mtu kufanya mabaya, ana uhuru)
Changamoto kubwa inayowasonga viongozi vijana ni kumilikiwa. Kuna hatari ya viongozi vijana kumilikiwa au kuongoza kwa akili za walioko nje ya ulingo. Kuna umuhimu wa viongozi vijana kuonesha umakini mkubwa na kipekee.
Ili kummiliki kiongozi kijana watu hutumia vitisho nini kitampata au nini hakitampata. Mara nyingi wenye roho hii (spirit of manipulation) husema, fanya hivi ili upendwe na watu au usifanye hivi watu watachukia. Watu wenye roho hii hutoa hakikisho feki, humwakikishia mtu usalama ambao kimsingi ni Mungu peke yake atupaye kukaa salama katika kazi, biashara na vyeo. Katika amani nitajilaza na kupata usingizi mara, Maana Wewe, Bwana, peke yako, Ndiwe unijaliaye kukaa salama.” Zaburi 4:8
Yesu alijua Petro anaroho hii ambayo hutoka kwa shetani. Petro alimwita Yesu Kristo pembeni akimwonya kwamba, mateso hayatampata. Mara nyingi wenye roho hii hupenda kumbana mtu pembeni, humwita kipekee bila ya watu, hutoa onyo hilo kwa siri.
Ingawa Yesu Kristo alikuwa kiongozi kijana hakusita kumkemea Petro kwamba, “rudi nyuma yangu shetani”. Nakusihi kijana usiruhusu kumilikiwa kinyume na kusudi la kuumbwa kwako, usizuiwe kutekeleza yale ambayo Mungu amekuitia kutekeleza. Mathayo 16:23
Nakumbuka nikiwa kiongozi kijana mtu mmoja aliniita akinikemea na kunieleza fanya hivi au vile, na mara moja nikawa mkali nikamwambia, “Mimi ni mtu wa kanuni, sipangiwi nifanye lipi na lipi nisifanye bali napanga mwenyewe.”
Yes, I am a man of Principle! Nilijibu hivyo waziwazi kwa sababu nilijua ubaya wa roho hii ya kumiliki watu, nilikuwa nimeitafakari usiku wa kabla ya tukio. Mtu anaruhusa ya kuchagua hata mabaya, uhuru wa kuchagua (freedom of choice) ni muhimu kwa kila jamii ya kistaarabu. “Because to take away a man’s freedom of choice, even his freedom to make the wrong choice, is to manipulate him as though he were a puppet and not a person” Madeleine L’Engle
Imani hufanya watu wamilikiwe lakini maarifa huwaweka huru. Hakuna anayeruhusiwa kumiliki utashi na dhamira ya mwanadamu. Hata viongozi wa dini hawaruhusiwi. Mwanadamu ni kiumbe huru, na anapaswa kuamua apendacho.
Endelea kutembea katika uhuru wako, Mungu alimtuma mwenaye kukuokoa na shetani ili uwe huru wala si ili uwe milki ya viongozi wa dini, siasa au serikali.  Kumiliki watu ndio uchawi wa kisasa ambapo mtu hafanyi kitu bila ya kupiga simu au kuomba kibali kwa wanadamu.
Amesema Joyce Meyer, Ukiwa na shida nenda kwenye kiti cha enzi cha Mungu, usikimbilie kupiga simu. (Go to throne not to the telephone) Mtegemee Mungu na yeye atakuwa ngome yako, ngao yako, na kigao wala hautaondoshwa. 
Barikiwa.

0 comments :