Unatatua changamoto gani?

9:19:00 PM Unknown 0 Comments

 
UNATATUA CHANGAMOTO GANI?
Ili kuishi maisha yenye hamasa, swali muhimu unalotakiwa kujiuliza sio unataka kufanya nini katika maisha yako ya kuwa hapa duniani bali unatakiwa kujiuliza ni changamoto gani au tatizo gani unataka kulitatua katika kuishi kwako? Moja ya sifa kuu ya kufanana kwa watu wote waliofanikiwa ni utatuzi wa changamoto; nioneshe mtu aliyefanikiwa nikuoneshe changamoto anayotatua au aliyotatua katika kuishi kwake. Katika ulimwengu huu, usitafute jambo la kufanya; tafuta changamoto ya kutatua.
Kila aliyezaliwa na mwanadamu amebeba jawabu la changamoto fulani; kwa sababu mafanikio ya kweli yamebebwa katika kuleta majibu juu ya changamoto au upungufu uliopo mahali fulani. Watu hawatakufuata wala kukulipa kwa sababu una kipawa au ujuzi au uwezo fulani ndani yako, watu watakufuata na kuwa tayari kukulipa kwa sababu kipawa chako, ujuzi wako na uwezo wako unatatua changamoto walionayo. Thamani yako mbele ya watu inategemea kiwango chako cha utatuzi wa changamoto walizonazo watu hao.
Boresha uwezo wako wa kutatua changamoto.
Kila mara ni muhimu kuboresha uwezo wako wa kutatua changamoto, ndio maana hata watengenezaji wa simu kila mara huboresha simu wanazotengeneza kwa kuziongezea uwezo wa kutatua changamoto mbali mbali. Ndio maana utasikia iPhone 5 mara iPhone 6 mara “iPhone 6 plus”. Wanachofanya hapa si kutengeneza simu nyingine bali ni kuboresha simu iliyotengezwa hapo awali. Na kwa sababu hiyo thamani ya iPhone 6 plus ni kubwa kuliko thamani ya iPhone 6 ya kawaida. Na watu wako tayari kulipa zaidi kwa iPhone 6 plus kuliko iPhone 6 ya kawaida kwa sababu “iPhone 6 plus” imeboreshwa uwezo wake wa kutatua changamoto ya mawasiliano. 
Kuna namna nyingi za kuboresha uwezo wako wa kutatua changamoto katika eneo lako la huduma, biashara, tekinolojia, uongozi, elimu ulipata, uandishi, ofisini, kipawa, michezo (athletes); baadhi ni kwa kutafuta ujuzi zaidi, ‘kupractice’ zaidi, kujifunza kwa waliokutangulia, kujifunza kwa waliofanikiwa, kusoma vitabu vinavyohusiana na eneo umalotaka kulifanyia kazi n.k. Wazo kuu hapa ni kujitahidi kuwa bora zaidi ya jana, tafuta kuwa bora (excellent) katika kila ulichoweka nia ya kukifanya.
There’s a place for you at the top

0 comments :