UNATAKA KUFANIKIWA KATIKA NINI?- IV

10:10:00 PM Unknown 0 Comments

UNATAKA KUFANIKIWA KATIKA NINI?-IV
(Amua kuthubutu)
Mtu mmoja amewahi kusema, “Maisha hayatupi tunachokitaka, bali hutupa kile ambacho tupo tayari kukifanyia kazi”. Kile ambacho unatamani kitokee katika maisha yako au katika eneo lolote la maisha yako ni lazima uwe tayari kufanyia kazi ili kiwe halisi. Nioneshe mtu mwenye udhubutu katika yale anayoyatamani, nikuoneshe mtu mwenye matokeo katika maisha yake.
Kuhamasika (motivated) pekee katika jambo fulani hakutaleta matokeo katika maisha kama hakuna udhubutu wa kufanyia kazi jambo hilo. Wako wengi waliopita semina au kusikia mafanikio ya watu wengine, na wakahamasika kweli kufikia malengo waliyojiwekea lakini baada ya muda hakuna wanachoweza kuonesha kama matokeo ya kuhamasika kwao. Na hii ni kwa sababu walihamasika lakini hawakuchukua hatua ya kufanyia kazi matamanio yao.
Mwenyehekima mmoja amewahi kusema, baada ya mwaka kupita au mwezi au muda fulani, tutabaki tukijilaumu na kutamani kama tungedhubutu kuyafanya yale tuliyoyahairisha. Do it today or regret tomorrow. Kumbuka: hakuna jambo lolote lenye thamani ambalo huja kirahisi, ni matokeo ya kazi (nothing worth comes easy, it takes work).
Mtu mvivu husema,Simba yuko nje; nitauawa katika njia kuu” Mithali 22: 13
Adui mkubwa katika eneo la udhubutu ni visingizio; unaweza kuwa katika kundi la watu wanaoeleza kwa nini hawakuweza kufikia malengo yao, au ukawa katika kundi la wachache wanaoleza namna gani wameweza kufikia mafanikio yao katikati ya changamoto nyingi. Kumbuka, ulimwengu hautoi heshima kwa wanaoeleza kwanini haiwezekani, au kwanini hawakuweza au wanaoeleza namna ambavyo watu waliwakatisha tama walipotaka kuanza. Usijipe majibu ya kushindwa au kwamba haiwezekani kabla haujadhubutu. “Maisha hayatupi tunachokitaka, bali hutupa kile ambacho tupo tayari kukifanyia kazi”.

There’s a place for you at the top

0 comments :