Ububu wa Zakaria

11:39:00 AM Unknown 0 Comments


UBUBU WA ZAKARIA.
(Bora asiyesema, kuliko anenaye yasiyostahili)
Kuzaliwa kwa Yohana mbatizaji kulikuwa kwa muujiza, maana wazazi wake walikuwa wazee sana na wenye kukoma katika kawaida za wanadamu. Zakaria aliposhindwa kuamini aliyoambiwa na BWANA alifanyika bubu. Kumwacha mwenye imani ndogo azungumze kunaweza kuharibu ushuhuda, hivyo ni bora afanyike bubu. Talk Faith! Luka 1:20
Biblia inasema Zakaria alifanywa bubu kwa sababu hakusadiki neno la Mungu (Luka 1:20). Asiye na imani hutamka mashaka wala hakuna uhai na uwezo wa kujenga katika maneno yake. Tumepewa vinywa kwa ajili ya kujibariki na kuwabariki wengine. Tumepewa vinywa kwa ajili ya kumkiri Mwokozi wetu na kuwajenga wanaotusikia. Kwa nini kuongea jambo ambalo ndani yake hamna tumaini, kwa nini kuzungumza jambo ambalo ndani yake imani tena ya nini tutamke lile ambalo si faraja.
Akiwajenga watoto wake mchungaji mmoja alisema, “Talk love, talk faith, talk hope and edify others” yaani, zungumzeni upendo, imani, tumaini na kuwajenga wengine. Ni afadhali ukae kimya kuliko kujilaani au kujiita mdhambi. Tunahesabiwa haki kwa maneno yetu, hatusaidii sana kujiita wenye dhambi, na kujiona watu duni.
Kristo alitimiza amri kumi hivyo kupitia Kristo kila aaminiye ametimiza amri kumi ndani ya Kristo. Hivyo basi si mara zote unapojiita mdhambi unapata rehema, kuna mara nyingine unajihukumu kwa sababu tu hauna imani ya kujiita mwenye haki.
John F Kennedy aliyepata kuwa Rais mwenye upekee wake nchini Marekani alisema, “The only reason to give a speech is to change the world” yaani “sababu pekee ya kutoa hotuba ni ili kuubalisha ulimwengu wetu” yaani kuufanya uwe bora zaidi na uwe mahala salama zaidi.
Hatuongei ili kufanya watu wapigane, hatuongei kuleta uchochozi. Yesu alipotukanwa hakujibu chochote badala yake alijikabidhi kwa Mungu. Aliamini Mungu anaweza kujibu mashambulizi hayo vizuri kuliko yeye. Tatizo wengi wetu hatumwamini tunaona tunaweza kujibu na kulipiza vizuri kuliko Yeye. Tunasahau kisasi ni juu ya BWANA na kwamba BWANA ni hodari wa vita.
Wako wale wasemao jino kwa jino au jicho kwa jicho, lakini sheria hii haiwezi kutekelezeka ikiwa aliyekutendea yu na nguvu kuliko wewe. Waefeso sita imeiita imani yetu silaha, imeiita pia maombi yetu silaha, kwayo tunaweza kushindana vema kuliko kwa matusi, dharau na majigambo.
Mungu akubariki sana!
Usikose msimu wa tano wa Weekend Purpose.

0 comments :