Kwa mara ya mwisho

12:22:00 PM Unknown 0 Comments

 
KWA MARA YA MWISHO
[USIPOZUIA LEO HUWEZI KUZUIA KESHO]

Inaweza ikawa ni ahadi ya uongo, kujiahidi kupita uwezo wetu wa utendaji. Ngoja nile kwa mara ya mwisho, ngoja ninywe kwa mara ya mwisho, ngoja niende kwa mara ya mwisho, ngoja nikakae naye kwa mara ya mwisho. Tunaweza kushinda jaribu la kesho leo, kamwe huwezi kushinda jaribu la kesho bila ya kushinda leo.
Inawezekana unajitahidi kupunguza ulaji wa sukari, inawezekana unajitahidi kuacha kilema fulani au unahitaji kupunguza kiasi cha unywaji wa soda. Unaweza tu kwa kuondoa urasimu wa mpaka kesho, mpaka mwezi ujao au mpaka juma lijalo. Usianguke leo ili usimame kesho, badala yake simama leo ili kesho usimama imara zaidi. Mwenye hekima mmoja anaandika: “Giving in even once weakens our ability to resist next time”
Hujachelewa bado, wala haujaharibika kabisa, you are not beyond repair! Usijikatie tamaa mabadiliko yanawezekana. Siku 365 za mwaka ni fursa 365 za kubadilika. Neema ipo kila asubuhi kwa hiyo unaweza kubadilika bila shaka. 
Kuna nyakati huwa najiona niko chini (very down) kwa sababu ya dhambi, makwazo, majaribu na pengine kiburi changu dhidi ya neno la Mungu. Lakini huwa najitia moyo nikiwa na hakika kwamba, Mungu hakuniumba ili anihukumu bali ili aniokoe na kunipa uzima wa milele katika YESU KRISTO. Nikikumbuka neno hili huwa nafarijika sana, Kwa kuwa Mungu hakutuweka kwa hasira yake, bali tupate wokovu, kwa Bwana wetu Yesu Kristo;” 1Wathesalonike5:9
Kuna mwingine anaweza akasema Mungu anajua tutakwenda jehanamu, kwa hiyo hakuna haja ya kufanya jitihada. Wazo hilo si la kweli, Mungu anajua utakwenda mbinguni kwa hiyo fanya jitihadi za kumtafuta.  1Watheselonike 4:9 inaweka wazi kwamba Mungu hakutuumba kwa ajili ya hukumu.
Yesu aliposema, haombi kwa Baba atutoe ulimwenguni bali atulinde na yule mwovu alimaanisha, Changamoto zipo, na hakuna aliyekingiwa changamoto (no one is immune to challenges) sote tunapaswa kupambana na kushinda. Unapotatua changamoto moja unatengeneza kinga ya kukusaidia kupambana na changamoto nyingine, ndivyo wasemavyo wenzetu kwamba; “bahari shwari haitoi wanamaji shupavu.” Utapitia mengi katika bahari ya maisha; ila uwe na hakika Mungu anakuwazia mema na mwisho wake utatoka katika bahari ya maisha ukiwa shupavu na hodari. Yako mateso na ziko changamoto, yote hayo yapo ili kufanya uwe bora zaidi na uwe shujaa zaidi.
Bila jangwa huwezi kuwa na Musa mpole na mtaratibu, bila ubaguzi wa rangi huwezi kuwa na Nelson Mandela mwenye kusamehe na mwenye heshima; bila ya kufeli au kuishia njiani ki-masomo tusingelipata watu bora kama Bill Gates ambao laiti wangefaulu masomo yao vizuri na kuhitimu wangekuwa waajiriwa wala wasingeliweza kujiajiri na kuajiri maelfu kama walivyo sasa.
Endelea mbele Yesu Kristo yu hai kwa ajili yako. Shallom……

0 comments :