Jambo muhimu katika maisha

12:13:00 PM Unknown 0 Comments

  JAMBO MUHIMU KATIKA MAISHA
Mafanikio katika jambo lolote kwenye maisha ya mtu si jambo la bahati nasibu; mafanikio huja kama matokeo ya kufuata au kutekeleza kanuni muhimu katika maisha ya mtu. Jambo moja wapo muhimu (kanuni) katika maisha ya mtu ili kufikia kilele cha mafanikio yake ni kujijengea tabia ya kujitathimini mara kwa mara ili kupata fursa ya kuona kama kile unachokifanya au kiwango cha maisha unayoishi ni sawa na kile ulichopanga au kutarajia.
Mwenyehekima mmoja amewahi kusema, maisha yasiyokuwa na kujitathimini ni maisha matupu (void). Si watu wengi wamejijengea tabia hii ambayo ni kanuni muhimu sana ili kufikia mafanikio halisi katika jambo lolote. Nioneshe mtu anayejitathimini mara kwa mara, nikuoneshe mtu anayefanikiwa katika njia zake.  Mfano mzuri wa kanuni hii muhimu katika maisha ni habari ya mwana mpotevu, ambaye aliishi maisha nje ya kile alichokusudiwa mpaka pale alipoamua kufanya jambo muhimu la kutathimini aina na kiwango cha maisha aliyokuwa anaisha. Kumbuka kila kitu huwa sawa mpaka pale umesimama na kujitathimini. (Luka 15)
Kujitathimni kunatoa fursa muhimu sana katika maisha katika maisha ya mtu. Kujitathimini kunaweza kufanyika wakati wowote ule, mwanzo wa mwaka au mwisho wa mwaka au katika ya mwaka au kila mwezi kulingana na malengo uliyojiwekea na mazingira uliyonayo. Kujitathimini kuna faida nyingi ikiwemo faida saba (7)zifuatazo:
i. Kujitathimini kunakupa fursa na kuamsha (renew or rejuvenate) hamasa (passion) na kukupa nguvu katika kile ulichokuwa unafanya au kuchukua hatua katika kile unachotakiwa kukifanya ili kufikia kilele cha mafanikio katika jambo husika.
ii. Kujitathimini kunakupa fursa na nafasi ya kuangalia malengo na vipaumbele vyako ili kuona kama vinaendana au vitakufikisha katika mafanikio unayoyatazamia.
iii. Wakati mwingine kujitathimini kunakupa fursa ya kujitambua zaidi na kuanza upya ili kujinasua mahali ulipokuwa umekwama.
iv. Kujitathimini kunakupa nafasi ya kuona rasilimali na fursa (opportunities) zinazokuzunguka ili upate  kuzitumia na kukufikisha katika malengo makuu.
v. Kujitathimini kunakupa nafasi ya kuziona fursa badala ya vikwazo katika changamoto au mazingira uliyonayo.
vi. Kujitathimini kunakupa fursa ya kutambua ni maeneo gani unayohitaji msaada (assistance) na mahali pa kupata msaada huo ili kukuwezesha kufikia malengo yako.
vii. Kupata fursa ya kuona kama kile unachokifanya au kiwango cha maisha unayoishi ni sawa na kile ulichopanga au kutarajia
Njia thabiti ya kujitathimini katika jambo lolote ni kwa kujiuliza maswali muhimu. Hii itakupa fursa ya kuona aina na kiwango ulichopo au mwenendo wa jambo husika; yafuatayo ni baadhi ya maswali muhimu unapojitathimini hasa katika kuangali aina na kiwango cha maisha uliyonayo sasa (Kiroho, kibiashara, kifamilia,kiuchumi,  kiofisi n.k):
i. Hivi ni kwanini naishi maisha ya namna hii kwa sasa? Je ningependa kuendelea na maisha haya hadi nitakapozeeka ama nataka kubadilika? (kutoka kitabu cha Timiza Malengo yako, Joel Nanauka)
ii. Je hivi aina na kiwango cha maisha ninayoishi ni sawa na kile nilichopanga au kutarajia (plan)
iii. Je hiki ninachokifanya kinachangia katika kufikia malengo yangu ya kimaisha?
iv. Je ni jambo gani naweza kufanya ili kuongeza ufanisi na ubora katika kile ninachokifanya? Kitu gani naweza kuboresha zaidi ili kutoa huduma au bidhaa bora zaidi ya sasa?
v. je, kwa sasa nikichukua maamuzi gani yatakuwa ni mwanzo wa mabadiliko  katika maisha yangu? Mfano: kutoka katika mahusiano, kuomba msamaha, kutafuta kazi nyingine, kujiunga na shule/kozi n.k (kutoka kitabu cha Timiza Malengo yako, Joel Nanauka)
“There’s a place for you at the top”

0 comments :