Bado hujawa tayari kuoa

10:57:00 AM Unknown 0 Comments

 
BADO HUJAWA TAYARI KUOA.
(MANENO YAKO YANAAMUA HATMA YAKO)
Si rahisi kufahamu mtazamo wa mtu kama hajatamka chochote, si rahisi kujua mawazo ya mtu asipoyaweka katika maneno. Maneno yetu huonesha hatma yetu. Your words determine your reach!
Maneno yetu huelezea msimamo na uelekeo wetu juu ya jambo fulani. Kuna baadhi ya maneno mtu akitamka unaweza kujua hali inayojiri moyoni mwake. Yafuatayo ni baadhi tu ya maneno yanayooenesha kwamba mtu hayuko tayari kwa kuolewa au kuoa.
Wanawake wote ni sawa. Kitendo cha kusema wanawake wote ni sawa ni hatua inayo onesha mtazamo mbaya dhidi yao. Kwambo wote ni waovu, au wote hawafai. Mtu mwenye mtazamo huu hafai kwa kuoa. Hata biblia imetanganisha wako iliyowaita mke mwema na kuna wengine imewaita kahaba. Wako wazuri na wema kama Abigaili, na unapaswa kumwomba BWANA ili upewe mke mwema. “Moyo wa mumewe humwamini, Wala hatakosa kupata mapato. Humtendea mema wala si mabaya, Siku zote za maisha yake.” Mithali 31:11-12
Mwanamke atanisaidia nini? Mtu anayefikiri anajitosheleza mwenyewe (self centered and self consumed) na asingehitaji msaada wa mwingine hafai kwa kuungana naye. Kama hauoni umuhimu wa nafasi ya mke katika kukusaidia kibiblia na kijamii basi usioe. Ni yule anajua umuhimu wa nafasi fulani ndiye anayeweza kuipigania hata nyakati za changamoto kali. Ni Mungu aliyesema, Si vema mwanaume awe peke yake, wala si mwanadamu aliyenena hayo. Kama haikuwa vema pale Edeni basi ujue si vema hata sasa uwe peke yako. Mwanzo 2:18
Wanawake hawaokoki. Hili nalo si jambo jema. Nimewahi kumsikia rafiki yangu mmoja akilisema na akinukuliwa na rafiki yangu mwingine. Rafiki yangu huyu ameoa mwaka jana,sasa sijui kwa nini kaoa. Katika ndoa mwanamke ni kama udongo ambao mwanaume anapanda maisha yake (Sow your life) na kinyume chake kwa wanawake. Asiyeokoka maana yake asiye zaliwa mara ya pili au asiyeamini, Sasa kwa nini upande maisha yako kwa mtu asiye amini? Ingawa wanaume huwa na msimamo imara sana katika imani na maamuzi lakini bado wokovu si swala la kijinsia bali ni swala la imani. Luka 8:4
Ataniharibia huduma? Naamini uharibifu katika muungano unaweza kufanywa na mtu yeyote aliyesehemu ya muungano huo. Kusema ni upande fulani tu si sawasawa, kwani kwa kufanya hivyo upande mwingine unakuwa ni kama upande wa Malaika. Ni jambo jema kama pande zote zitalenga na kujizatiti kusaidia mafanikio ya kiroho ya upande mwingine kiroho. Mithali 31:11-12
Tunakuwa salama sana pale ambapo fikra zetu zinakuwa sawasawa na neno la BWANA. Pale tunapowaona wengine ni bora kuliko sisi tunaonesha ukomovu wa akili na imani. Tunakuwa wenye hekima sana tunapoacha kuwahukumu watu kwa rangi zao, jinsia zao, kabila lao na nchi zao. Imeandikwa “wote” yaani nchi zote, makabila yote na lugha zote. Warumi 3:23 “Kwa sababu wote, wamefanya dhambi na kupungukiwa na utukufu”
Tukutane katika msimu wa tano wa “weekend of purpose” hapo mwezi May jitahidi ufike, yako mengi mazuri yanaandaliwa kwa ajili yako mteule wa BWANA. Barikiwa.

0 comments :