Sala ya mwaka mpya

12:03:00 PM Unknown 0 Comments


SALA YA MWAKA MPYA 2017
(EE, BWANA UNIUMBIE MOYO SAFI)
Mipango ya mwaka mpya 2017 bila badiliko la moyo na mtazamo ni kazi bure, ni sawa na kufukuza upepo. Sasa ni mwanzo wa mwaka ambapo kila mtu ana mipango lukuki. Iko ya kitabia, maana tungependa kuwa watakatifu Zaidi 2017, iko ya kiuchumi, maana hutupendi umasikini, iko ya kijamii maana tungependa kuwa na Amani na watu wote na kusaidia jamii zetu mwaka huu.
Katika kuanza mwaka nilipenda kuwasikia watumishi wengi wa Mungu wanasema nini kuhusu mwaka mpya 2017. Lakini katika wote na yote mimi nimeguswa na badiliko la moyo ambalo amelisema Billy Graham ambaye ni mhubiri mashuhuri tena mwenye alama. Kwamba, kama BWANA hakuniumbia moyo safi basi sitaonja badiliko lolote mwaka huu. Lakini kama mioyo yetu na mitazamo yetu kama haikubadilika basi mipango hiyo yote itakuwa ni bure. Ni lazima kufanywa upya nia zetu. [Warumi 12:1-2]
Moyo wako ndio kitovu cha mabadiliko yote. Moyo hutoa badiliko la kudumu, na ili badiliko liwe la kudumu lazima litoke katika msukumo wa ndani na si kutoka nje. Mimi pia nina mipango mingi mwaka huu lakini huu ni kipaumbele, ninataka badiliko la moyo, niwe safi zaidi na nifanane na Yesu. Ni muhimu tumwambia BWANA abadilishe mioyo yetu. Oh Lord Jesus, change my heart!
Unaweza ukajipinga mwenyewe, ikiwa mtindo wako wa maisha hauna uhusiano chanya na malengo yako basi tegemea 2017 kukuonesha mabadiliko kidogo sana. Ni vigumu kukua kiuchumi bila kupunguza matumizi ya anasa, wako wanaotaka kubadilika bila kumwomba Yesu abadilishe mioyo yao. Daudi alijua hawezi kujibadilisha wala hawezi kubadilika ikiwa Mungu si chanzo na egemeo la mabadiliko hayo. Haya ni maneno yake Daudi akihitaji badiliko kutoka dhambini mpaka katika utakatifu tena, Ee, Mungu uniumbie moyo safi…” Zaburi 51:10
Katika orodha ya mipango yako ya mwaka huu, ongeza mmoja, ongeza badiliko la moyo, fanya jambo hilo kuwa mpango mkuu.
Kila la kheri katika 2017.

0 comments :