Usioneshe kama hutaki kuigwa

10:04:00 AM Unknown 0 Comments



USIONESHE KAMA HUTAKI KUIGWA
(Don’t show it if you don’t want to be imitated)
Watu wengi wanaonesha mambo ingawa nia yao ya ndani hawataki watu wengine wayaige mambo hayo. Katika mchezo wa mieleka (WWE) baada  ya kuonesha matangazo ambayo si salama kwa watoto eti wanasema, usijaribu nyumbani, “Don’t try this at home.” Ubongo wa mtu humuamuru kutenda na kutendea kazi kile akionacho.
Wale wa sigara nao baada ya kuandika mandishi makubwa yenye kusisitiza uongo, na kuweka vibwagizo vyenye kuonesha sigara ilivyotamu kama vile, “ni tamu, ni fresh, ni yako” ndipo wanaweka maandishi mengine madogo yasemayo, “uvutaji wa sigara ni hatari kwa maisha yako.” Wanasisitiza uongo kwa herufi kubwa na ukweli kwa herufi ndogo kabisa, mwandishi amefanya tofauti kidogo katika makala hii ili kukemea uvutaji wa sigari ambao kimsingi huleta saratani na magonjwa ya kifua.
Unadhani ni kwa nini makampuni yanawekeza mamilioni ya fedha katika matangazo? Fikiri ni kwa nini wasanii wanaofanya matangazo hayo hulipwa maradufu?  Hivi karibuni hapa Tanzania kampuni moja ya simu imeshindwa kuendelea kumlipa msaanii mmoja aliyedai kuongezewa pesa kwa ajili ya matangazo ya biashara anayoyafanya na kampuni hiyo. Jawabu ni moja makampuni yanaamini watu wakiona wanaamini, na huo ndio ukweli. Kampuni zinapata wateja lukuki kupitia matangazo kwa kuwa kile wateja waonacho huamini na kufanya.
Kila fainali za kombe la dunia zinapoisha vijana huanza tabia na mitindo mpya toka kwa wechezaji. Ukitazama mitindo yao ya kunyoa nywele na mavazi utajifunza kitu. Kuna nguvu katika kile walichokiona. Ukitambua hili utaona umuhimu wa kuonesha yale tu unayotaka yaigwe. Haijialishi ni mavazi, picha, matendo au maneno tusemayo. Ni vema tusema mambo ya kuigwa, tuishi kwa kuigwa na tuvae kwa kuigwa. Don’t show it if you don’t want to be imitated!
Si lazima watu waokolewe kwa kusoma neno na kuhubiriwa, wakati mwingine waokolewe kupitia mienendo yetu. Biblia inasema kuna nyakati unaweza kuoa au kuolewa na mtu asiye amini (mpagani) na kupitia wewe (matendo na maisha yako) atakayo tazama anaweza kuokoka. Kuna nguvu katika kile unachoona. No one in the bible had the bible.
Usitazame kile usichotaka kuwa. Nilimuulize mtoto mmoja anayetazama mieleka kwamba, unampango wa kupigana? Akasema, “Hapana, ila mtu akinichokoza nampiga za hivyo.” Somo hapa ni kwamba, ukitazama sana visivyofaa utatenda isivyofaa pia.
Rai yangu kwako, usione visivyofaa wala usioneshe usichotaka watu waige.

0 comments :