Kupatwa kwa jua

3:08:00 PM Unknown 0 Comments

KUPATWA KWA JUA.
(Wafu hawawezi kumchagua Yesu wala kumkataa shetani)
Alhamisi, Septemba Mosi ilikuwa siku ya kupatwa kwa jua. Maeneo mengi ya mkoa wa Mbeya hususani Rujewa yalishuhudia kufifia kwa mwanga na giza kutokea kwa masaa kadhaa. Naamini ilikuwa hivyo kwa maeneo mengi ya Tanzania na Afrika Mashariki kwa ujumla.
Kituo cha habari cha BBC kilifanya mahojiano na Mheshimiwa Ghalib Bilal kuhusu kupatwa kwa jua na hapo nikataka kusikia machache kuhusu jambo hilo. Katika mahojiano hayo dondoo kubwa niliyopata ni kwamba, “kupatwa kamili hutokea mara moja katika eneo fulani kila baada ya miaka 300.” Kupatwa kamili kwa jua kutatokea tena hapa nchini kwetu miaka 360 ijayo. (At any place on Earth, a Total Solar Eclipse can be seen on average once every 360 years.). Only my grave will witness that.
Miaka mia tatu ijayo mimi wala wewe hatutakuwepo. Kumbe hatuna nafasi ya kuona tena kupatwa kamili kwa jua tukiwa Tanzania. Tunachoweza kukiona tena ni kupatwa kwa kawaida tu ambako hutokea mara kwa mara na si kupatwa kamili. Je, utakuwa wapi miaka mia tatu ijayo? Je, ratiba yako ya siku inakupa kujiandaa na maisha hayo ya umilele?
Ni vema kujiandaa! Ni ukweli ulio wazi, dhambi ni kikwazo cha maandalizi yetu. Kama ilivyokuwa kwa Adamu watu hawatendi dhambi kwa bahati mbaya au kwa kudanganywa, bali hutenda kwa kuchagua. Yesu alikuwa kijana na alijaribiwa kama sisi na hakutenda dhambi. Dhambi ni uchaguzi. Tunatenda kwa sababu tumeamua kumkana na tumechagua kutenda. We sin not because we have to, but it is because we want to.
Kila siku watu zaidi ya mia moja hamsini hufariki, magaidi nao wanasababisha vifo katika halaiki za watu. Kuuawa na gaidi hakukufanyi uokoke, unamuhitaji Yesu kwa umilele wako. Mamia ya wanachuo wa Garisa huko Kenya waliuawa na magaidi wa alshababu; tukio hilo haliwapi marehemu hao kumwona Mungu ikiwa hawakumchagua Yesu wakati wa uhai wao.
Ukimkataa Yesu ukiwa hai huwezi kumkubali ukiwa kaburini, ndio maana hakuna nchi duniani ambayo marehemu wanapiga kura. Wafu hawawezi kumchagua Yesu wala kumkataa shetani. Ni walio hai tu ndio wana uwezo huo. Dereva mmoja akielezea uzoefu wake wa kesi za ajali za barabarani alisema, “Marehemu hashindi kesi.”
Ukikosa kufika mbinguni huwezi kukosa kufika motoni. Wasio kwenda mbinguni huenda motoni. Watu wengi hawavutiwi sana na kwenda mbinguni kwa sababu hakuna walichowekeza huko. Hawajawekeza tumaini, imani, upendo, fedha wala matendo mema; hakuna wanachotazamia kukiona wakifika huko, ndio maana hawana fikra za kwenda huko.
Donald Trump anapokwenda Uingereza anakwenda kuona alichowekeza, Dangote anapokuja Tanzania (Mtwara) ni kutazama alichowekeza huko. Tukiweka pesa zetu mbinguni, tukikataa mambo ya dunia basi bila shaka shauku yetu ya kwenda mbinguni itaongezeka mara dufu maana tumewekeza huko. Hakuna mfanyabiashara anayeridhika kwa kupata taarifa za simu tu bila ya kufika eneo ilipo biashara yake ilikujiona kwa macho kinachoendelea, vivyo hivyo haitoshi kusikia tu simulizi za mbinguni ni lazima siku moja tufike huko.
Yesu alikuja kwa sababu ya walio wake, na sisi hatuna budi kumfuata aliko kwa sababu Yesu ni wetu. Tukiwekeza hazina yetu mbinguni tutatamani kwenda kwa sababu hazina ya mtu ilipo na moyo wake upo. Jifunze huduma kama hawa wa Luka 8:3 ambao waliamua kuhubiri na Yesu kwa fedha zao: “na Yoana mkewe Kuza, wakili wake Herode, na Susana, na wengine wengi, waliokuwa wakimhudumia kwa mali zao.
BWANA AKUBARIKI

0 comments :

Jitazame kama Mungu anavyokutazama

11:38:00 AM Unknown 0 Comments

JITAZAME KAMA MUNGU ANAVYOKUTAZAMA 
Sehemu kubwa ya maisha ya mtu huathiriwa (influenced) sana na namna anavyojitazama. Mara nyingi, mtazamo wa mtu juu ya maisha yake na nafsi yake huamua hatima yake. Mtu anayejitazama kama aliyeshindwa (failure) katika jambo fulani; hakuna namna ataweza kushinda au kufanikiwa katika jambo hilo. Hakuna mtu aliyeweza kwenda mbali zaidi ya mtizamo wake (jinsi aonavyo nafsini mwake). Kumbuka, Jinsi ujitazamavyo, ndio kikomo chako.
Suleimani, Mwenye hekima wa kale na kiongozi wa taifa la Israeli  amewahi kusema, “Maana aonavyo (mtu) nafsini mwake ndivyo alivyo”.  Akiwa na maana kwamba, kiwango na aina ya maisha anayoishi mtu ni matokeo ya namna mtu huyo anavyoona nafsini mwake. Kama mtu haridhishwi na aina ya maisha anayoishi au kiwango cha maisha anayoishi, hatua ya kwanza kabisa sio kubadili kazi au biashara; bali kuangalia na kubadili fikra na mtizamo wake uliomfikisha mahali alipo. Ndio maana wataalamu wa sayansi ya fedha wanasema, mtaji wa kwanza kwa mtu sio fedha bali wazo (mtizamo/fikra) jipya.
Tunaishi katika nyakati ambazo kila asubuhi unasikia na kusoma habari mbaya, kuyumba kwa uchumi, vita na majanga mbalimbali, ambayo kwa pamoja huleta hali ya kukata tamaa na kujiona hatuwezi, kana kwamba hakuna tumaini; Lakini habari njema ni kwamba, katikati ya vurugu za ulimwengu huu, unaweza kuchagua kuona tofauti; kujiona kama Mungu anavyokuona.
Wakati wa vita na tishio kwa taifa la Israeli kutoka kwa Goliati na majeshi ya Wafilisti, kila mtu alikuwa amekata tamaa na kukosa tumaini, lakini Daudi alichagua kujiona kama Mungu anavyomuona na mwisho wake ilikuwa ushindi mkuu kwake na kwa taifa lake. (1 Samweli 17:33, 37, 45-47)
Wakati wa tishio la Wamidiani, Gideoni alikuwa amejificha; Malaika akamtokea na kusema, “Bwana yu pamoja nawe ee shujaa”. Bwana alikuwa pamoja naye; na alikuwa anamuona na kumtambua Gideoni kama shujaa; Lakini Gideoni aliona Mungu hakuwa pamoja naye (amemuacha) yeye na taifa lake, hivyo  alijiona dhaifu na mtu asiye na msaada; ndio maana alikuwa amejificha. Lakini ukweli ni kwamba, changamoto alizokuwa nazo hazikuondoa ukweli na uhalisi wa kwamba Bwana yu pamoja naye na kuwa yeye ni Shujaa (Waamuzi 6:2, 11-14, 16). Changamoto zilizopo hazifuti wala kubadili msimamo na mtazamo wa Mungu juu ya maisha yako.
Gideoni hakufanywa shujaa wakati ule Malaika anamtokea, Malaika alimkuta Gideoni akiwa shujaa; ndio maana alimsalimia ee Shujaa; alichofanya malaika sio kuondoa changamoto za Wamidiani. Jambo la kwanza alihitaji kubadili namna ambavyo Gideoni anajitazama; ili aanze kujiona kama Mungu anavyomuona; ili aweze kuwa msaada kwa jamii yake pia. Naamini kabisa, kama asingebadili mtizamo wake na kuanza kujiona kama Mungu anavyomuona; Mungu angetafuta mtu mwingine wa kufanya naye kazi. Mpaka umejitazama kama Mungu anavyokutazama, kuna uwezekano mkubwa changamoto ulionayo ikaendelea kuwepo.
Kuna watu huomba na kusali kwa kushusha thamani yao kwa kujifananisha na vitu mbele za BWANA. Kuomba na kusali kwa namna hii si sawa mbele za Mungu. Mungu ametufanya kuwa watoto wake, warithi pamoja na Kristo Yesu (Joint heirs) na sisi ni matawi katika Mzabibu ambaye ni Yesu Kristo yaani tunauzima ule ule ndani yetu alionao Kristo (kumbuka uhai uliopo kwenye shina la mti ndio uhai huo huo ulipo kwenye matawi); Kwanini mtu ajione hana thamani mbele za Mungu aliyechagua kumvika taji ya utukufu na heshima namna hii? (Zaburi 8:4-6). Sala za namna hii hazioneshi kiwango cha mtu cha unyenyekevu mbele za Mungu, bali huoneshi kiwango cha ujinga (ukosefu wa maarifa) alicho nacho mtu.
Mwimbaji wa nyimbo za Injili, Sinach ameimba wimbo anasema “I know who I am (Ninajua/fahamu mimi ni nina)” swali langu kwako, je unajua wewe ni nani? Je unajiona kama Mungu anavyokuona; shujaa, mwana wa Mungu, mshindi, mwenye kuyaweza mambo yote katika Yeye, unajiona kama Mkono wa Mungu uko upande wako, mrithi pamoja na Kristo? Hakikisha unasikiliza vizuri wimbo wa mwanadada Sinach (unapatika youtube), itakuwa ni mahali pazuri pa kuanzia.
See you at the top

0 comments :

Mbona umeacha

12:28:00 PM Unknown 0 Comments

 
MBONA UMEACHA?
(Hakikisha unaanza tena)
Ulianza kusali vipi mbona umeacha? Ulianza biashara vipi mbona umeishia njiani? Ulianza kusoma kozi ile vipi mbona umekwama? Kwa nini umeacha kufanya mazoezi? Tatizo liko wapi? Hauoni kwamba, huu ni muda sahihi kwako kurejea kwa kishindo.
Katika siasa kuna neno maarufu liitwalo, “bouncebackability” ambalo linaelezea uwezo wa mwanasiasa kuinuka tena. Anaweza kuonekana ameishiwa sera au ameanguka kabisa, na ghafla anasimama na kushinda kwa kishindo. Ufufuko wa Yesu nao ulikuwa na sura hiyo. Kwa siku mbili na zaidi alizokuwa kaburini wengi walidhani ameshindwa kabisa, hata mitume wake walikata tamaa, siku ya tatu alifufuka na kutoka mzima.
Hii ni wiki yetu ya kusimama tena na kurejea katika nafasi zetu kwa kishindo.  Ni wiki ya kumwomba BWANA, afufue kazi zake ndani yetu. Inawezekana wewe ni mhubiri mfu, ni kiongozi mfu, ni mkristo mfu au ni mhandisi mfu. Lakini ni saa yako na yangu kumwambia, “EE BWANA FUFUA KAZI ZAKO NDANI YANGU”
Ni muhimu kumaliza ile kazi tuliyoianza, ni muhimu zaidi kuanza tena kutokea pale tulipoishia. Mwanariadha mmoja wa Tanzania akiwa katika mashindano ya Olimpiki aliendelea kukimbia na kumaliza mbio hizo ndefu licha ya kuumia. Napenda maneno ambayo mtangazaji alimpamba mwanariadha huyo aliyekuwa majeruhi alisema: “Sikutumwa na Nchi yangu kutoka mamilioni ya maili ili kuanza mbio, bali nimetumwa kumaliza mbio.”
Ni kweli kabisa hatukuitwa kuanza bali kumaliza, hatukuitwa kuwa washiriki tu wa maisha bali tumeitwa kuishi kama washindi. Je, Nguvu yetu inatoka wapi? Nguvu yetu si tu ile itokanayo na chakula tunachokula yaani, protini, vitamin, maji na vyakula vya nguvu. Nguvu yetu ni zaidi ya chakula tulacho, nguvu yetu yatoka kwa Bwana Mungu aliyeziumba mbingu na nchi. Kwa Yeye (Yesu Kristo) tunayaweza mambo yote na tunahakika tutamaliza.
Kwa kuwa bado tuko hai basi kila kitu kinawezekana. Napenda mchezo wa mieleka, somo kubwa katika mchezo huu ni kwamba, kuwekwa chini si kushindwa na kupigwa sana si kupoteza mchezo. Mara nyingi katika mchezo huu hata aliyechoka huweza kuibuka mshindi. Ni siku yako leo, toka kaburini, anza tena, maliza kazi yako, Mungu Baba na afufue kazi yake ndani yako katika jina la Yesu Kristo. Amen

0 comments :

Usioneshe kama hutaki kuigwa

10:04:00 AM Unknown 0 Comments



USIONESHE KAMA HUTAKI KUIGWA
(Don’t show it if you don’t want to be imitated)
Watu wengi wanaonesha mambo ingawa nia yao ya ndani hawataki watu wengine wayaige mambo hayo. Katika mchezo wa mieleka (WWE) baada  ya kuonesha matangazo ambayo si salama kwa watoto eti wanasema, usijaribu nyumbani, “Don’t try this at home.” Ubongo wa mtu humuamuru kutenda na kutendea kazi kile akionacho.
Wale wa sigara nao baada ya kuandika mandishi makubwa yenye kusisitiza uongo, na kuweka vibwagizo vyenye kuonesha sigara ilivyotamu kama vile, “ni tamu, ni fresh, ni yako” ndipo wanaweka maandishi mengine madogo yasemayo, “uvutaji wa sigara ni hatari kwa maisha yako.” Wanasisitiza uongo kwa herufi kubwa na ukweli kwa herufi ndogo kabisa, mwandishi amefanya tofauti kidogo katika makala hii ili kukemea uvutaji wa sigari ambao kimsingi huleta saratani na magonjwa ya kifua.
Unadhani ni kwa nini makampuni yanawekeza mamilioni ya fedha katika matangazo? Fikiri ni kwa nini wasanii wanaofanya matangazo hayo hulipwa maradufu?  Hivi karibuni hapa Tanzania kampuni moja ya simu imeshindwa kuendelea kumlipa msaanii mmoja aliyedai kuongezewa pesa kwa ajili ya matangazo ya biashara anayoyafanya na kampuni hiyo. Jawabu ni moja makampuni yanaamini watu wakiona wanaamini, na huo ndio ukweli. Kampuni zinapata wateja lukuki kupitia matangazo kwa kuwa kile wateja waonacho huamini na kufanya.
Kila fainali za kombe la dunia zinapoisha vijana huanza tabia na mitindo mpya toka kwa wechezaji. Ukitazama mitindo yao ya kunyoa nywele na mavazi utajifunza kitu. Kuna nguvu katika kile walichokiona. Ukitambua hili utaona umuhimu wa kuonesha yale tu unayotaka yaigwe. Haijialishi ni mavazi, picha, matendo au maneno tusemayo. Ni vema tusema mambo ya kuigwa, tuishi kwa kuigwa na tuvae kwa kuigwa. Don’t show it if you don’t want to be imitated!
Si lazima watu waokolewe kwa kusoma neno na kuhubiriwa, wakati mwingine waokolewe kupitia mienendo yetu. Biblia inasema kuna nyakati unaweza kuoa au kuolewa na mtu asiye amini (mpagani) na kupitia wewe (matendo na maisha yako) atakayo tazama anaweza kuokoka. Kuna nguvu katika kile unachoona. No one in the bible had the bible.
Usitazame kile usichotaka kuwa. Nilimuulize mtoto mmoja anayetazama mieleka kwamba, unampango wa kupigana? Akasema, “Hapana, ila mtu akinichokoza nampiga za hivyo.” Somo hapa ni kwamba, ukitazama sana visivyofaa utatenda isivyofaa pia.
Rai yangu kwako, usione visivyofaa wala usioneshe usichotaka watu waige.

0 comments :

Ni atakayevumilia

10:07:00 AM Unknown 0 Comments

 
NI ATAKAYEVUMILIA MPAKA MWISHO
(Endelea kufanya, anzia ulipoishia)
Taasisi ya taarifa za takwimu za kazi nchini Marekani (US Bureau of Labor Statistics Information) inaripoti hivi, “katika nyanja zote za biashara, asilimia arobaini na nne (44%) ya makampuni mapya hutoweka ndani ya miaka miwili na asilimia sitini na sita (66%) hutoweka ndani ya miaka minne ya uhai wa makampuni hayo.”
Mwisho wa siku si yule aliyeanza safari, wala si yule mwenye nguvu, bali ni yule aliyevumilia na kufika kileleni. Biblia haisemi ajuaye sana ataokoka, wala haisemi anayekaa karibu na kanisa ndiye atakaye okoka, badala yake imenena, “atakaye vumilia mpaka mwisho.” Kuanzia katika mafunzo ya kawaida kabisa ya maisha mpaka kwenye neno la Mungu ni mvumilivu ndiye aliyetabiriwa kushinda.
Kwenye ujasiliamali watu huambiwa, “winners never quit, quitters never win.” Uzoefu wa maisha unampa nafasi kubwa mvumilivu kuliko mtu mwenye akili kubwa lakini ana tabia ya kukata tamaa. Kaka mmoja alikuwa na nia ya kuwa daktari (medical doctor) na aliendelea na nia hiyo licha ya vikwazo vingi. Kikwazo kikubwa kilikuwa ni kupata sifuri (division zero) kidato cha sita. Lakini ilikuwa ni habari njema kwangu kusikia kwamba, mwakani atamaliza miaka yake mitano na kupata alichotamani maishani mwake kwa siku nyingi, udaktari. Daraja la mwisho limeshindwa kumkwamisha kwa sababu ya uvumilivu wake.
Rafiki yangu aliandika, “ukichoka usiache, jifunze kupumzika.” UKiwa kwenye uhusiano jifunze kutafuta njia ya kuendelea na si ya kutokea. Ukishindwa kupambana na changamoto katika uhusiano omba kupumzika ili upate muda wa tafakari na maombi. Moja ya changamoto ni tamaa isiyozuilika, ukikaa pembeni utakumbuka kwamba, kuna faida katika kumtii Mungu na raha ya ajabu hutokea ikiwa miili yetu itatumika kama mahekalu ya Mungu. Dakika moja ya tafakari ina maana zaida kuliko masaa mengi ya majibizano.
Mchana mmoja Dominick Mzonya, aliniomba nimsindikize ili akazungumze na kuwatia moyo wanafunzi. Katika moja ya mambo aliyowasisimua kwayo ni kumbukumbu ya tafiti ya makundi matatu ya watu. Makundi hayo matatu yalihusisha watu wenye uwezo wa juu (akili sana), wenye uwezo wa kati (kawaida), na wale wenye uwezo wa chini. Mwisho wa siku katika kutazama maisha ya watu hawa mafanikio yao hayakutokana na akili au uwezo wao bali yalitokana na uvumilivu wao. Wa kundi la mwisho alipovumilia alifanikiwa, wa kundi la kwanza alipovumilia alifanikiwa hatimaye hata wa kundi la katikati alipovumilia bila ya kukata tamaa alifanikiwa. Nguvu haipo katika akili kubwa (High IQ) bali katika kufanyia kazi upendacho, kujitoa, na kudumu bila ya kukata tamaa. Christiano Ronaldo anaonekana kusifiwa sana katika soka moja ya siri ya mafanikio yake ni hii, “Ni wa kwanza kuingia uwanjani kwa mazoezi kabla mchezaji mwingine awaye yote hajaingia na ni wa mwisho kutoka wakati wote wameshamaliza mazoezi.”
Washindi ni wavumilivu, sifa nyingine wanazopewa na watu ni urembo tu. Washindi hufanya mazoezi kila siku kwa uaminifu mkubwa. Mwanafunzi hawezi kufaulu mtihani kwa kusoma siku moja nzima yenye saa 24. Bali mwanafunzi atakayesoma kwa saa moja kila siku ndani ya siku 24 atakuwa bora kupita yule aliyesoma usiku na mchana. Ingawa wote watatumia saa ishirini na nne lakini yule wa kila siku saa moja anaonesha kudumu na kujizatiti katika maandalizi kwa siku ishirini na nne, wakati yule aliyekesha usiku na mchana anaonekana kudumu kwa siku moja tu.
Kila mtu ni mvumilivu lakini si mpaka mwisho, wengi ni mpaka katikati. Kila kitu ni kigumu ila ni lazima tudumu katika kukifanya. Usikate tamaa endelea kuomba kazi, endelea na kipaji chako, wekeza muda mwingi katika kazi zako. Hakuna kuchoka, hakuna kuzimia mpaka tumefika kileleni. Ili timu yetu, “Life minus regret program” iweze kutoa makala hizi kila wiki inatulazimu kusoma kila siku, kusali na kuandika kila wiki. Usisahau tuna majukumu yote kama wewe. Usiache, usirudi nyuma, na Mungu atakusaidia na kukusimamisha. Mapambona yanaendelea, well done is waiting for you.

0 comments :