Nuia Kuacha Alama

6:53:00 PM Unknown 0 Comments

 
NUIA KUACHA ALAMA
(Tumia uwezo ulio ndani yako) 
Mwandishi wa vitabu na kiongozi maarufu Dr. Myles Munroe, amewai kuandika, “The greatest tragedy in your life will not be your death but what dies with you at death. What a shame to waste what God gave you to use” yaani Jambo baya kabisa katika maisha yako halitakuwa kifo chako, bali ni kifo cha kile ulichokufa nacho. Ni fedheha kiasi gani kufa bila kutumia uwezo uliopewa na Mungu ili uutumie (Tafasiri isiyo rasmi).
Mara nyigi mtu anapofikiri juu ya kifo chake, ghafla anapata hekima na nidhamu juu ya aina na mfumo wa maisha anaoishi sasa; na kuanza kuishi kwa kuzingatia vipaumbele muhimu katika maisha yake. Watu wote walioacha alama (legacy) duniani, walifikiri juu ya vifo vyao kwanza; walijua wao si wa kudumu hapa duniani; na kuna siku hawatakuwepo, hivyo walifanya bidii kuishi na kutumia uwezo [potentials] waliokuwa nao kwa namna iliyowapasa ili muda wao utakapoisha wasiwe watu wa kujuta.
“Basi, utujulishe kuzihesabu siku zetu, Tujipatie moyo wa hekima” Zaburi 90:12
Ili kuacha alama inatupasa kuishi kwa ufanisi kwanza, kutumia kile tulijaliwa na Mungu kwa ajili ya sifa na utukufu wake na kwa kuwafaidia wengine. Hapa nataka nikushirikishe hatua tatu muhimu zitakazokusaidia;
Hatua ya kwanza, ni kutambua uwezo ulionao. Kila mtu anao uwezo ndani yake, hakuna mtu alikuja duniani bila kupewa uwezo fulani utakaompa Mungu utukufu na kuwafaidia watu wengine. Inaweza kuwa ni kuongea, kuandika, michezo (athletes), kuimba, ‘uwezo wa biashara’, kusimamia na kuongoza, Mawazo ya kuanzisha kampuni, kufundisha, kuhubiri, kupika, kufurahisha wengine  n.k
Hatua ya pili, ni kuufanya uwezo huo kuwa bora kila siku (Improve) ili makusudi utakapokuwa unautumia, uwe katika kiwango cha ubora na ufanisi zaidi. Kama ni kazi au huduma unafanya leo, uifanye katika ubora kuliko ulivyofanya jana. Nuia kufanya kitu bora kila siku kuliko ulivyofanya jana. Hii itakulazimu kujifunza na kupata maarifa zaidi ili kuboresha uwezo huo.

Mfano. Unaweza kuwa na uwezo wa kuimba lakini haujui kuimba, yaani hauna maarifa ya kukusaidia kuimba katika ubora. Mwenyehekima mmoja amewahi kusema, “Watu hawavutwi na uwezo ulionao, bali wanavutwa na ujuzi ulionao”.

Kuwa na uwezo tu haitoshi, unahitaji maarifa yatakayo kusaidia kutumia uwezo huo. Ujuzi ni tofauti na uwezo hauji kwa kuwekewa mikono, unakuja kwa kujifunza[1Tim4:13, 14], yaani kama wewe haujajifunza sheria; utawekewa mikono na Mwanasheria mkuu wa serikali mpaka upate upara, na bado utatoka haujui
Hatua ya tatu, usisubiri uwe kila kitu ili ufanye kitu; usipate shida kuanza na biashara ndogo, ikiwa ndani yako unaona kampuni. Biblia inasisitiza kuwa, mtu asidharau mwanzo mdogo [Zekaria 4:10, NKJV]. Mwal. Christopher Mwakasege amewahi kushuhudia kwamba alianza kuhubiria watu wanne, leo hii anahudumia maelfu; Mwandishi wa kitabu cha The Leader who had no title, Robin Sharma anasema katika mkutano wake wa kwanza ukumbi mzima ulikuwa na watu wapatao ishirini na wanne, kati ya hao ishirini na mmoja ni ndugu zake.
Mama Teresa wa Calcutta hakuwa na fedha alipoanza kuwasaidia masikini kule India; alijua kamwe hawezi kuwafikia masikini wote na kuwapatia huduma muhimu; hii haikumkatisha tamaa, alianza na mmoja. Kumbuka jambo hili: Usiniambie unachoweza kufanya, nioneshe.

0 comments :