Mpaka umevuka, hakuna kusogea..!

10:14:00 AM Unknown 0 Comments

 

MPAKA UMEVUKA HAPA, HAKUNA KUSOGEA...!
Wakati yupo shule (akiwa mdogo), aliyewahi kuwa kiongozi mashuhuri Dr. Myle Munroe; alikuwa mwanafunzi wa mwisho darasani katika kila matokeo. Kwa wakati ule hakuna aliyefikiri angeweza kufanya jambo lolote la maana; si tu ulimwenguni lakini hata katika maisha yake binafsi. Anasema siku moja wakati anasoma biblia alikutana na na sehemu inayosema, “Nayaweza mambo yote katika Yeye (Kristo) anitiae nguvu”; na hapo ndipo ulipokuwa mwanzo wa maisha yake kubadilika pamoja na mabadiliko kimasomo; kwa wastani wa mwaka mmoja alitoka kuwa mwanafunzi wa mwisho darasani hadi kuwa mwanafunzi bora shule nzima, mpaka anamaliza.
Mpaka tumefikiri sawasawa, hatuwezi kuishi sawasawa. Mawazo yaliyopata nafasi ndani ya mtu juu ya jambo fulani au eneo fulani la kimaisha, ndiyo yatakayoamua hatima yake katika eneo hilo. Kama mtu hajaridhika na hali fulani katika maisha yake; njia ya pekee na ya kudumu ili kutoka mahali hapo, ni kwa kukutana na wazo mbadala litakalo zaa matumaini kwa kumpa kuona picha iliyobora zaidi anayopaswa kuifanyia kazi.  Mwanadamu atabaki katika hali hiyo hiyo aliyopo mpaka wazo mbadala limeingia na kutawala katika kichwa chake (Exposure).
Kama tunataka kuwa na matokeo tofauti na watu wa kawaida (average people) au tofauti na wakati uliopita katika eneo fulani; ni lazima tufikiri na kufanya tofauti. Kama haulidhishwi na kiwango cha kimaisha au kiroho ulichopo sasa; hali hiyo ya kutokuridhika unayoisikia ndani yako ni wito wa kukutaka ufikiri na kufanya tofauti na unavyofanya sasa.  Mwanasayansi Albert Einstein amewahi kusema, “Ni uendawazimu; kufanya kitu kile kile kwa namna ile ile, na kutegemea kupata matokeo tofauti” (Tafasiri isiyo rasmi)
Hakuna mtu anayeweza kwenda mbali zaidi ya mawazo yake aliyonayo sasa; mpaka umeelewa jambo hili, mambo hayawezi kusogea. Isaac Newton, “mwanafisikia” katika kanuni yake ya kwanza (Newton’s first law of motion) anasema, “Kitu kitabaki katika hali yake hiyo hiyo iliyopo, mpaka imekutana nguvu kutoka nje” (Tafasiri isiyo rasmi)
Mwandishi wa karne ya kwanza Paul katika kitabu chake kwa wafilipi anatoa vigezo vya kuzingatia unapochagua aina ya mawazo yanayopaswa kupata nafasi na kutawala ndani yako; akiwa na maana kwamba, endapo wazo halitakuwa na sifa au vigezo hivyo, usilipe nafasi ya kufanya makazi ya kudumu katika moyo [akili] wako.
Hatimaye, ndugu zangu, mambo yoyote yaliyo ya kweli, yoyote yaliyo ya staha, yoyote yaliyo ya haki, yoyote yaliyo safi, yoyote yenye kupendeza, yoyote yenye sifa njema; ukiwapo wema wowote, ikiwapo sifa nzuri yoyote. Yatafakarini hayo. Mambo mliyojifunza kwangu na kuyapokea, na kuyasikia na kuyaona kwangu, yatendeni hayo...” Wafilipi 4:8-9 (Msisitizo umeongezewa)

0 comments :