Sitaki kukosa baraka hizi

12:28:00 PM Unknown 0 Comments

 
SITAKI KUKOSA BARAKA HIZI
Ilikuwa mwezi Desemba 2015 nikiwa katika basi la Mbeya Express kuelekea Mpanda huko Katavi. Kama ilivyoada nilikuwa na kitabu changu mkononi ili kurahisisha safari yangu. Na katika mapumziko hayo mafupi ya siku kuu ya Chrismas niliamua kuchochea uinjilishaji kwa kusoma kitabu hicho cha mwandishi Marc Cahil, “One Thing You Cannot Do In Heaven”
Kitabu kinahusu uinjilishaji tena si rahisi kukutana na ujumbe mwingine katika kitabu hicho ambacho nilikuwa nakisoma kwa mara ya pili. Wakati huo hali yangu ya uchumi ilikuwa si nzuri, ingawa nilikuwa nakwenda likizo nilikuwa nakwenda nikiwa na wazo la kupunguza matumizi. Nilikuwa natembea nikiwa na tahadhari kichwani, ya kupunguza matumizi hususani ya fungu la kumi. Ghafla ndani ya kitabu nikakutana na onyo, “Unapotaka kupunguza matumizi usipunguze pesa ya sadaka au fungu la kumi”
Yaani, unaweza kupunguza matumizi ya nguo; chakula, vinywaji, safari na mengine lakini si matumizi ya sadaka na zaka. Niliposoma ujumbe huo nikaweka azimio moyoni kwamba sitapunguza matumizi ya zaka badala yake nitatoa kama ilivyokawaida 10%. Ilinisumbua kidogo kwani nilikuwa nimepanga tayari kupunguza matumizi ya sadaka ili kumudu mambo mengine.
Mwandishi alinukuu maandiko kutoka katika Biblia jinsi Mungu atakavyo fungua madirisha ya mbinguni na kunibariki hata isibaki nafasi, nilisoma pia namna atakavyo nilinda na kuondoa hali ya kuvuja kiuchumi. Baada ya kuzisoma ahadi hizo niliandika pembeni ya kitabu maneno haya, “siko tayari kukosa Baraka hizi” yaani, “I am not ready to forfeit these blessings.”
Nilipofika nyumbani niliamua kumtolea Mungu bila kupunguza kiwango licha ya changamoto iliyokuwapo. Nilipomtolea Mungu alinibariki mno tena kwa haraka akinipa zaidi ya mara tano ya sehemu niliyotoa zaka ndani ya siku saba. Kila ninapotoa fungu la kumi ninamwona Mungu. Mara nyingine umeme uliachiliwa pasipo kupoozwa vema na watu wengi walishuhudia uharibifu wa mali, jirani yangu pia alishuhudia vitu vyake vikiungua. Asubuhi wakati ananipatia taarifa ya kilicho tokea ndipo nilisikia ndani yangu Roho akinikumbusha lile neno kwamba, tukitoa zaka kamili Mungu atamharibu yeye aharibuye. Nami nikajua wazi ni Mungu aliyeokoa vitu vyangu kutoka katika uharibifu wa umeme. Asubuhi hiyo niltamani niwashuhudie jirani zangu kwa nini Mungu amelinda vitu vyangu lakini sikupata kibali kwani wangeweza kutafsiri kama majigambo ilhali ni shauku yangu kuona wengi wanakata bima kutoka mbinguni kwa njia ya fungu la kumi.
Mtu pekee ambaye anachukia kutoa fungu la kumi ni yule ambaye hawajawahi kutoa na hivyo hajaonja baraka za kutoa zaka. Kwa sisi tulio onja kwa kweli, hatuwezi acha tabia hiyo. Anthony Robbins anashauri watu kuweka akiba moja kwa moja lakini mimi nashauri tutoe zaka moja kwa moja.
Hata kama matumizi yako yameongozeka epuka kuacha kutoa fungu la kumi kwa sabau tu eti matumizi yameongezeka. Toa hata katika hali ya shida. Tahadhari! Wengi wametoa na huenda hawajaona Mungu akitenda kama nilivyoshuhudia. swali langu kwao, walikwenda kutoa sehemu gani? Nimewahi kuulizwa, “Ni wapi nikatoe fungu la kumi?”
Katoe mahali unapolishwa kiroho, toa mahali wanapoliheshimu neno la Mungu, toa kwa wale wanaotaabika kwa ajili ya kuwalisha watu chakula cha roho yaani neno. Chunguza udongo na kisha toa kwa watumishi waadilifu. Mkulima anapaswa kuchagua udongo, hali kadhalika tunapotoa zaka, sadaka na dhabihu lazima tuchague udongo. Eneo unalopeleka zaka litakupatia neno kwa wingi, ukichunguza utaona maeneo mengi ambayo watu hawatoi zaka hakuna neno. Mungu alisema tutoe zake ili chakula (neno lake) liwe kwa wingi ghalani (Kanisani/fellowship/huduma na nk).

0 comments :