Kwa nini ulianza?

4:03:00 PM Unknown 0 Comments

 
KWA NINI ULIANZA?
Michael Jordan aliwahi kuambiwa na kocha wake akiwa shule, kuwa hana uwezo wa kuwa mchezaji wa “basketball”; leo hii anajulikana kama shujaa katika mpira wa kikapu ulimwenguni. Dr. Myles Munroe aliwahi kuambiwa na mwalimu wake kuwa yeye si binadamu kamili, akili zake ziko nusu, hivyo hawezi kuelewa kama wanafunzi wengine; lakini leo anatajwa kama mwandishi bora aliyewahi kuishi katika nyakati zetu; ambaye  asilimia 80 ya vitabu vyake vimevunja rekodi ya mauzo na kuandikwa katika lugha zaidi ya 60.
Watu hawa walipokutana na hali ya kukatishwa tamaa katika kufikia malengo, ndoto na maono yaliyokuwa ndani yao, hawakurudi nyuma na kujikunyata; ndani yao walijua kwanini walianza safari katika kufikia malengo na ndoto zao. Sababu ya wao kuanza ilikuwa na nguvu, kuliko nguvu ya kukatisha tamaa kutoka katika mazingira yaliyowazunguka. Wewe pia jiulize ni mangapi ungefanya kama tu, ungekuwa na uhakika wa ushindi wakati wa kuanza? Tafakari kwa jinsi ya mshairi huyu anavyouliza. “How many things would you attempt if you know you could not fail” Robert Frost
Watu wakuu hawakuangalia changamoto za fedha au rasilimali zao; hawakuangalia ubaya wa maisha yao ya nyuma; hawakuangalia nani anayewaamini au asiyewaamini; hawakuangalia mazingira magumu waliyokuwa nayo, bali waliutizama uaminifu wa Mungu na uwezo [potentials] uliowekwa ndani yao. Hawakuwa tayari kwa mazingira yao kuamua hatima ya maisha yao.
Na tena, walijua sababu iliyowasukumu kuanza walichoanza. Kumbuka, Unapotambua kwanini ulianza jambo, utapata nguvu na ujasiri wa kusonga mbele [katikati ya changamoto] ili kufikia malengo makuu ulikuwa nayo tangu awali.
Unaposikia hali ya kukata tamaa katika kuelelekea jambo au “project” fulani katika maisha yako; kitu kimoja unaposwa kujiuliza ni je “Kwanini ulianza? Sababu ya kuanza ndiyo sababu ya kuendelea, inakupa nguvu na ujasiri wa kusonga mbele mpaka utakapotimiza ndoto na maono yaliyowekwa ndani yako.
Kumbuka jambo hili, unapokutana na changamoto fulani katika kufikia lengo lilopo mbele yako; endelea kufanya unachotakiwa kufanya, endelea kufanya unachotarajiwa kufanya; hata kama mazingira yanakushawishi kufanya tofauti [1Samweli30:3-4,6,8].
Bwana atanitimilizia mambo yangu…” Zaburi 138:8a


0 comments :