Utamaduni wa Yesu

11:35:00 AM Unknown 0 Comments


 
UTAMADUNI WA YESU
(JESUS CULTURE OF WORSHIP)
Utamaduni wa Yesu Kristo ni kuabudu. Katika siku zake hapa Duniani Yesu alijijengea kasumba ya kuabudu mara kwa mara. Wanaoabudu sanamu wanafanana na sanamu, na wanao mwabudu Mungu hufanana na Mungu. Kwa jinsi tunavyomwabudu Mungu zaidi ndivyo tunavyofanana naye zaidi.  Si ajabu ndio maana Yesu alifanana na Baba yake wa mbinguni. Nawaonea huruma wanaoabudu sanamu; fedha, muda, watu au vinyago kwa kuwa mwisho wa siku watafanana na sanamu zao, “Wazifanyao watafanana nazo, Kila mmoja anayezitumainia.”  Zaburi 115:8
Ni saa kumi na mbili jioni namaliza kutafakari. Mawingu ni ya bluu kidogo na hali ya hewa ni tulivu. Jua linaanza kuzama na mwangaza wake unafifia. Japokuwa kule kwetu Mpanda ni joto, lakini wakati jioni hali huwa ni rafiki. Na mara namwita kwa sauti mpwa wangu, “Benjamini, Benjamin, twende.” Tabiri, tunataka kwenda wapi na Benjamini? Tunakwenda mlimani mahali ambapo watu ni wachache, huko tutamwabudu Mungu na kumshukuru. Tunadumisha utamaduni wa Yesu ambao ni kuabudu. It was His dominant culture to worship God.
Zamani za kuhani Eli, Elkana wa Rama alikuwa akienda kuabudu kila mwaka. Alikwenda kila mwaka kwa kuwa zama zile watu walikwea kwenda mbali sana kuabudu. Walikuwa wakiabudu milimani tu ama Yerusalemu tu na hivyo ililazimu safari ndefu. Lakini sasa tunamwabudu Mungu katika roho na kweli, tunamwabudu mahali popote na muda wowote.Na mtu huyo alikuwa akikwea kutoka mjini kwake mwaka kwa mwaka, ili kuabudu, na kumtolea Bwana wa majeshi dhabihu katika Shilo. Na wale wana wawili wa Eli, Hofni na Finehasi, makuhani wa Bwana, walikuwako huko.”  1Samweli 1:3
Leo hii hatuendi mlimani wala Yerusalemu. Tunamwabudu Mungu barabarani, chumbani, kanisani, ofisini hata vitandani mwetu. Tunapofanya kwa utukufu wake maana yake tunamwabudu Mungu. Unaweza kumwabudu Mungu wakati wowote iwe ni katika kusoma au wakati unakula chakula. [1Kor 10:31]
Je, unataka kufanana na Mungu? Hakikisha unamwabudu na unamshukuru. Je, unatabia ya kuabudu? Unaweza kuamua kujijengea tabia ya kuabudu; na ni rahisi, tabia ni mazoea, mazoea hujengwa kwa kutenda jambo kwa kurudia rudia. Unamshukuru Mungu asubuhi, mchana jioni hata usiku.
Kwa kuwa Mungu ni mkuu ni vema ukapiga magoti na kumwangukia, ukijua wazi kwa njia hiyo unafanana naye. Ametutaka tumwabudu akijua kwa njia hiyo atatuinua.  Tafadhali mwabudu leo.  Amani ikae na waabuduo halisi na watu wote waseme Amina!


0 comments :