Chagua Heshima

4:07:00 PM Unknown 0 Comments


CHAGUA HESHIMA

Jitahidi uwe chombo cha dhahabu

Watu wengi wanapata heshima katika jamiii kwa sababu mbalimbali ambazo huhusisha pia mafanikio yao. Lakini si wote wanaoheshimiwa na wanadamu huheshimiwa na Mungu pia. Watu wengi tunapata heshima ya wanadamu huku tukikosa heshima mbele za Mungu. Basi katika nyumba kubwa havimo vyombo vya dhahabu na fedha tu, bali na vya mti, na vya udongo; vingine vina heshima, vingine havina. Basi ikiwa mtu amejitakasa kwa kujitenga na hao, atakuwa chombo cha kupata heshima, kilichosafishwa, kimfaacho Bwana, kimetengenezwa kwa kila kazi iliyo njema.”  2Timotheo 2:20-21
Mungu akikuheshimu atakutumia. Atakutumia kuleta mapinduzi, atakutumia katika vita, atakutumia katika injili, atakutumia katika uamsho, atakutumia katika uimbaji hata katika biashara. Si wote wafanyao hayo hutumiwa na Mungu, ila wako ambao Mungu huwatuma na kuwatumia katika hayo.
Aliwatumia Yefta na Daudi katika vita, alimtumia Yeremia katika unabii, alimtumia Sauli katika ufalme na Musa na Haruni katika Ukuhani. Alimtumia Mariamu katika kumleta mkombozi Yesu na Elizabeth katika kumleta mwijilisti Yohana mbatizaji. Atakutumia pia.
Lakini Mungu ana kanuni moja, anamtaka mtu ajitenge na uovu. Kama unataka heshima mbele zake basi ni lazima ujitenge na ouvu. Ukikimbia dhambi atakuheshimu, ukishinda vishawishi atakuheshimu pia. Heshima si neema, ni jambo la kuamua. Heshima huleta na mafanikio, na mafanikio anayotaka Mungu kuyaona kwetu ni ushindi dhidi ya dhambi.
Katika nyumba kuna vyombo vyenye heshima na visivyo na heshima. Vya dhahabu hupata heshima kubwa kuliko vya udongo na vya mbao au miti. Ni wewe ndiye mwenye jukumu la kuchagua uwe chombo cha dhahabu, chombo cha udongo au cha miti. Njia ni moja kujitenga na uovu. Basi katika nyumba kubwa havimo vyombo vya dhahabu na fedha tu, bali na vya mti, na vya udongo; vingine vina heshima, vingine havina. Basi ikiwa mtu amejitakasa kwa kujitenga na hao, atakuwa chombo cha kupata heshima, kilichosafishwa, kimfaacho Bwana, kimetengenezwa kwa kila kazi iliyo njema.” 2Timotheo 2:21
Mtu aliyejitakasa, anaheshima mbele za Mungu kuliko wapigania uhuru waovu, kuliko mastaa wazinzi, kuliko matajiri watoa kafara, naam kuliko watumishi wa Mungu wasiohubiri kweli ya Kristo ili kujipatia faida.
Tukijitenga na uovu Mungu atatuheshimu. Tutakua lulu kwake na dhahabu. Atatutumia sana kwa ngazi nyingine na kwa viwango vya juu. Kila siku nimekuwa nikimshukuru Mungu kwa kutupa upendeleo wa kuwa watangazaji wa injili. Ndiyo angeweza kuchagua wachina tu kwani wako zaidi ya bilioni moja, akikuchagua amekupendelea. Tafadhali jitakase.
“Oh! Choose to be a gold vessel”

UTAJIRI WETU KATIKA KRISTO YESU-II

8:25:00 PM Unknown 0 Comments


UTAJIRI WETU KATIKA KRISTO YESU-II
Njia kuu ya kutambua mapenzi ya Mungu juu ya maisha yetu, ni kwa kulisoma Neno lake. Neno la Mungu linatupa fursa ya kuyajua mawazo ya Mungu na mipango yake juu yetu katika siku zetu za kukaa hapa duniani. Neno la Mungu ni kama kioo, tunachopaswa kijitizama ili kuona kama maisha yetu yanaendana na mpango wake uliowekwa wazi katika Neno hilo.
Mpenzi naomba ufanikiwe katika mambo yote na kuwa na afya yao, kama vile roho yako ifanikiwavyo”3Yohana1:2
Jambo moja wapo tunalopaswa kutambua ni utajiri wetu tulionao katika Kristo juu ya afya. Ni mpango wa Mungu ulio kamili kwa watu wake kutembea katika afya njema siku zote za maisha yao. Si mapenzi ya Mungu usumbuliwe na magonjwa. Ukombozi wa mwanadamu hakuishia tu katika kukomboa roho yake, bali pia ulihusu ukombozi kwa nafsi, mwili na mazingira yake pia.
“Yeye mwenyewe alizichukua dhambi zetu katika mwili wake juu ya mti….; na kwa kupigwa kwake mliponya
1Petro 2:24
Biblia inasema kwa kupigwa kwake mliponywa, haisemi mtaponywa; hii inatupa kujua kuwa uponyaji wetu umekwisha kutolewa tayari, yaani gharama imekwisha kulipwa, hivyo magonjwa ya aina yoyote ile hayana uhalali wa kuwepo katika maisha yetu. Yesu Kristo alichukua madhaifu yetu [Math 8:17] hakuchukua udhaifu wetu ili aturudishie baada ya muda, alichukua ili kutupa fursa ya kufurahia uzima wa Mungu katika maisha yetu kwani alikufa mara moja na yupo hai kwa ajili yetu.
Ikiwa Yesu allichukua magonjwa na madhaifu yetu, sisi tulioitwa kwa Neema yake tumebakiwa na jambo moja tu nalo ni Afya, mahali ambapo ugonjwa au udhaifu umeondolewa ni jambo moja tu ambalo hubaki kutawala, nalo ni Afya dhabiti. Kumbuka, Yesu hakufa msalabani ili tu aokoe roho zetu, kifo chake kimelipia afya ya miili yetu pia ili ipate kutumika kama Hekalu la Roho wake Mtakatifu kueneza Ufalme wa Mungu hapa duniani. Kuishi bila ya kusumbuliwa na magonjwa au madhaifu katika maisha yetu hapa duniani inawezekana, shetani hakuna anachodai.
Ni kweli shetani ni mungu wa ulimwengu huu [2Kor10:4], lakini Neno la Mungu liko wazo kuwa, wewe si wa ulimwengu huu; hivyo basi shetani hana mamlaka juu yako wala juu ya afya yako. Una uhalali wa kutembea kifua mbele kwa kuwa upo katika ulimwengu ambao Yesu Kristo ndiye Mungu anayetawala, na katika Yeye hakuna magonjwa [Kolosai 1:13].
Kumbuka jambo hili, Ikiwa Yesu Kristo ndiye aliyekuweka huru, hakuna anayeweza kukuweka katika utumwa tena. Ikiwa ni Kristo ndiye aliyekubariki, hakika hakuna anayeweza kukulaani, ikiwa ni Yesu Kristo aliyechukua magonjwa na madhaifu yetu, je ni nani anayeweza kutuzuia kuwa na afya dhabiti? Tukiijua kweli, kweli itatuweka huru na hakuna atakayeweza kuchukua uhuru wetu.
Sawasawa na imani yako unapokea
.
Tunapokosa kujua utajiri tulionao ndani ya Yesu Kristo katika eneo fulani la maisha yetu, tunakuwa watumwa katika eneo hilo. Ndio maana Mungu hulituma Neno lake ili kuokoa. Biblia inasema watu “wanaangamizwa” kwa kukosa maarifa; maana yake ni kwamba “huyo” anayewaangamiza anatumia ujinga [ukosefu wa maarifa] wa hao watu wa Mungu kama mtaji wa kuwaangamizia. Watu wamechukuliwa mateka si kwa sababu ni wanyonge hawana nguvu bali wamechukuliwa mateka kwa sababu ya kukosa maarifa.   
“Kwa sababu hiyo watu wangu wamechukuliwa mateka, kwa kukosa kuwa na maarifa; na watu wao wenye cheo wana njaa, na wengi wao waona kiu sana”
Isaya 5:13
Nabii Isaya anasema, “Ni nani aliyesadiki habari tuliyoileta? Na mkono wa BWANA amefunuliwa nani?... (Isaya 53:1-8)! Mkono wa Mungu hufunuliwa kwake yeye anayesadiki habari iliyotolewa juu ya kile ambacho Mungu amesema. Uweza wa Mungu hufunuliwa na kuwekwa dhahiri kwetu ili kutusaidia na kutuokoa, pale tunapoamini ujumbe wa Neno lake. Mpaka tumejua na kukubali mioyoni mwetu kuwa kazi moja wapo ya msalaba ni kutupatia afya dhabiti, hatutaweza kufurahia afya ya Ki-Mungu katika maisha yetu.
Naye heri aliyesadiki, kwa maaana yatatimizwa aliyoambiwa na Bwana” Luka 1:45
Jambo kubwa ambalo tunataka ulipate siku hii ya leo ni kwamba, Mungu anajali mafanikio ya roho yako, nafsi yako, mwili wako na mambo yako YOTE [3Yoh1:2]. Kwa kifo na ufufuko wake, una uhalali wa kuwa mzima na kuanza kufurahia uponyaji na afya kamili juu ya jambo lolote lililokuwa likikusumbua. Katika Jina la Yesu Kristo, kama ulikuwa mgonjwa uwe mzima, kwa imani pokea Afya tele tangu leo; kwa kuwa Damu ya Yesu imeshakwisha kumwagika, na gharama imeshalipwa kwa ajili yako; Na sasa ni wakati wa kuishi maisha ya Ushindi katika Kristo Yesu kama ulivyokuwa umekusudiwa tangu awali.

Mtizamo wako juu ya changamoto

3:15:00 PM Unknown 0 Comments


MTIZAMO WAKO JUU YA CHANGAMOTO
Jambo kubwa linalokwamisha watu wengi kufikia kilele cha mfanikio katika mambo mengi ni mtizamo wanaokuwa nao hasa wanapokutana na changamoto kadhaa katika maisha yao ili kufikia mafanikio hayo. Hakuna mtu anayeweza kwenda mbali zaidi ya mawazo yake na mtizamo wake [Your attitude determines your altitude].
Watu wa Israeli wakasema, Je! Mmemwona mtu aliyepanda huko? Hakika ametoka ili awatukane Israeli; basi, itakuwa, mtu Yule atakayemwua, mfalme atamtajirisha kwa utajiri mwingi, naye atamwoa binti yake, na kuifanya mbari ya baba yake kuwa huru katika Israeli” 1 Sam 17:25
Kila mtu alimuona Goliath kama kikwazo cha mafanikio katika taifa la Israeli, kwa upande wa Daudi, Goliath alikuwa njia kuelekea na kufikia  maendeleo na mafanikio yake binafsi, mafanikio ya familia yake na taifa kwa ujumla, hakumuona kama kikwazo cha mafanikio bali njia ya mafanikio. 1Sam17:25-26, 48!
Wakati kila mtu alikuwa akiogopa kuingia Kaanani wa kuhofia majitu, Joshua na Caleb waliwaambia wana wa Israeli kuwa hawa ni chakula chetu, na Mungu alimpa kuona mafanikio ya nchi ya Kaanani (Hesabu14:9). Je una mtizamo gani juu ya changamoto iliyoko mbele yako au inayohusu familia au taifa lako? Je unaona ni kikwazo cha mafanikio yako au unaona ni mlango na njia ya kuelekea mafanikio yako.
Unaona nini?
Changamoto katika ulimwengu huu si jambo la kuepukika. Mara nyingi tunapotatua changamoto moja huibuka nyingine; kuna changamoto mbalimbali katika maisha ya mtu.  Wakati mwingine tunapokutana na changamoto mtu huweza kujihisi hana msaada; na tena hakuna namna anavyoweza kutoka salama katika changamoto hiyo. Mtu anapopitia wakati mgumu, huweza kufikiri ndio mwisho wa maisha yake, au mwisho wa ndoto na mipango yake. Ukweli ni kwamba hakuna changamoto itakayo dumu milele, kila jambo ni kwa wakati tu.
Mpaka tumechagua kuona kama Mungu anavyoona, changamoto hazitakuwa njia ya kuelekea mafanikio yetu bali vikwazo. Mpaka tumechagua kuona kama Mungu anavyoona hatutaweza kusema kama Daudi, “Nijapopita katika bonde la uvuli wa mauiti sitaogopa mabaya…!” BWANA alimuuliza Yeremia anaona nini, Yeremia aliona ufito lakini Mungu alilitazama Neno lake alilosema juu ya Yeremia ya kwamba atakuwa kiongozi wa mataifa na hakuna jambo litakaloweza kumzuia kufikia mafanikio hayo. [Yeremia 1:4-12]
“Kama sisi hatuamini,  yeye hudumu wa kuaminiwa. Kwamaana hawezi kujikana mwenyewe”2Timotheo2:13
Hii inatupa kujua kuwa haijalisha ni jambo gani linatokea, endapo mtu atachagua kuamini Neno la Mungu juu ya Maisha yake, hakika litatimizwa. Mungu analo Neno juu ya Afya yako, familia, biashara, ndoa, masomo n.k. Ni jukumu letu kujua Mungu anasema nini katika Neno lake juu ya maisha yetu. Hakuna upande salama isipokuwa upande wa Neno la Mungu. Katika Israeli wafalme walienda vitani baada ya kujua Neno la Bwana linasema nini juu yao kwa wakati wao, Mungu aliposema waende walienda hata walipokuwa wachache kwa kuwa walikuwa na Uhakika ya kuwa Mungu atafanya yale yote aliyoyaahidi.
Daudi akauliza kwa Bwana, akasema, Je! Nikiwafuata jeshi hili, nitawapata? Naye akamjibu, Fuata; kwa kuwa hakika utawapata, nawe hukosi utawapokonya wote. Basi Daudi akaenda…” 1Sam 30:1-9
Uweza wa Mungu unafunuliwa na kuwekwa dhahiri kwetu ili kutusaidi na kutuokoa pale tunapoamini Neno la Kinywa chake. Mt. Luka anaandika, “Heri aliyesadiki, kwa maaana yatatimizwa aliyoambiwa na Bwana”

Si kwa kazi wala si kwa matendo mema

2:28:00 PM Unknown 0 Comments



SI KWA KAZI WALA SI KWA MATENDO MEMA
Tumeokolewa bure

Biblia inanena wazi wazi kwamba, tumeokolewa kwa Neema kwa njia ya imani katika Yesu Kristo. Hakuna kazi inayoweza kutosha kumwokoa mwanadamu isipokuwa kazi ya msalaba tu, ni ile ambayo Kristo aliitenda. Kazi ya msalaba ni kazi timilifu hatuwezi kuchangia kitu. Iliyo kamili haihitaji kusaidiwa, Yesu alishasema imekwisha. Hakuna namna unavyoweza kuikamilisha iliyo kamili badala yake unapaswa kuamini tu. Kwa maana mmeokolewa kwa neema, kwa njia ya imani; ambayo hiyo haikutokana na nafsi zenu, ni kipawa cha Mungu; wala si kwa matendo, mtu awaye yote asije akajisifu.” Waefeso 2:8-9

Ongeza ufanisi ......

11:27:00 AM Unknown 0 Comments



ONGEZA UFANISI WAKO KUPITIA VIPAUMBELE
Uwezo wa mwanadamu unakikomo chake katika kila afanyalo. Ndio maana kuweka vipaumbele ni jambo la msingi. Nguvu za mwanadamu ni kidogo, hawezi kufanya vizuri kila kitu kwa wakati mmoja. Hawezi kuwekeza katika kila mradi. Hawezi kumfikia kila mtu. Kwa kuwa pesa tulizonazo ni kidogo, muda nao hautoshi na watu tulionao wanamajukumu mengi ndio maana tunahitaji kuweka vipaumbele.