Furahia Maisha Yako

11:09:00 AM Unknown 0 Comments

 
FURAHIA MAISHA YAKO!!
Mungu ametuumba si tu kwa ajili ya ibada na kazi, bali hata kwa ajili ya kufurahia maisha haya. Kutembelea fukwe, kula vizuri, kusafiri, kushiriki matukio ya furaha na pengine hata kuwa na mitoko ya hapa na pale kwa wale wapendanao. Alisema Ratan Tata yule mmiliki wa kiwanda cha kutengeneza magari ya TATA, “Hakuna faida yoyote ikiwa utapanda cheo siku ambayo mnatengana na mpenzi wako…maisha hayahitaji uwe shupavu na makini kiasi hicho” alimaanisha mafanikio ya kazini yaende sambamba na furaha ya nyumbani, tukichukulia maisha kuwa magumu sana kila siku itakuwa ni mapambano bila ya pumziko.
Biblia inaweka wazi katika kitabu cha Mhubiri 3:13, “tena ni karama ya Mungu kila mtu apate kula na kunywa, na kujiburudisha kwa mema katika kazi yake yote.” Napenda mstari ulivyotafisiriwa kwa lugha nyingine, “It is a gift of God to enjoy the good of all his labor”.
Mungu anapenda kila mtu apate muda wa kufurahia matokeo ya kazi zake. Baada ya kazi nzito ni furaha, partying and enjoying!!! Hatuna maana kwamba mioyo yetu izame katika anasa la hasha! Bali kuwe na muda wa kupumzika na kufurahia maisha ambayo ni zawadi kutoka kwa Mungu.
Maneno ya Reba Mc Entire huwa ni ya kuchekesha lakini yana maana alisema, “to succeed in life you just need a wishbone, backbone and a funny bone”. Ni kweli kabisa kila siku ni lazima tuwe na msingi wa kutumaini na kutamani yajayo lakini ni lazima ucheshi na furaha viwe kama uti wa mgongo wa mafanikio yetu.
Namna rahisi ya kufurahia haya maisha ni kuwa sababu ya wengine kufurahi. Katika mchakato wa kufanya watoto, majirani, mke, mume, binti wa kazi, au mfanyakazi mwenzio afurahi utajikuta wewe mwenyewe unafurahi. Furaha inatabia ya kurudi kwenye chanzo chake, hakikisha unakuwa chanzo cha furaha.
Maisha haya si marefu kiasi kwamba tukumbatie huzuni, ukiishi miaka 50 unamapumziko ya Jumamosi na Jumapili 2500 tu na inawezekana zimeshapungua, kama una mika 25 umeshatumia nusu ya majuma hayo. Jipange.
Enjoy…………
Kwa makala nyingine nyingi kama hizi tembelea; www.lifeminusregeret.blogspot.com

0 comments :