Kuelekea Uhuru wa Kifedha

12:43:00 PM Unknown 0 Comments

 
KUELEKEA UHURU WA KIFEDHA
(THE BIBLICAL LAWS OF MONEY)
Tafiti mbalimbali zinaeleza kwamba, moja ya changamoto kubwa ulimwenguni hasa bara la Afrika ni umasikini mkubwa wa kipato. Ni ukweli unaosikitisha, na eneo hili ni moja ya maeneo ambayo hayana msisitizo mkubwa ndani ya mwili wa Kristo (kanisa). Eneo la maarifa kuhusu fedha au uchumi ili kumkomboa mtu kiuchumi ni kama limeachwa; Na kwa sehemu kubwa ukiona mahali fedha inatajwa kanisani au kikundi cha sala basi ujue ni sadaka inayozungumziwa. Ni watu wachache sana wanaozungumzia au kuhubiri au kufundisha maarifa kuhusu fedha na uchumi ili kumuwezesha mtu kupiga hatua katika eneo hilo kwenye maisha yake na jamii yake.
Jambo moja ambalo ni halisi na halikwepeki ni kwamba, ili kuishi katika ulimwengu huu wa sasa kila mtu anahitaji fedha za kutosha kumuweza kukidhi mahitaji yake na mahitaji ya wale wanaomzunguka. Kumbuka fedha haina dini, haijali kabila wala rangi yako; haiwezi kuja kwako kwa sababu wewe ni wa dini au dhehebu au rangi au kabila fulani (it is neutral). Na kwa sehemu kubwa, kiwango cha fedha au mafanikio ya kiuchumi ya mtu yanategemea kiwango cha maarifa na ufahamu sahihi alionao juu ya kanuni za fedha (The laws of money).
Nakumbuka siku moja wakati nipo sekondari niliwahi kuhudhuria kikundi cha sala mahali  fulani, na siku hiyo tukafundishwa kuwa ili kufanikiwa kifedha basi ni lazima tutoe sadaka ya kupanda ili makusudi tuvune mara mia kwa kigezo kwamba ukitoa utapokea mara mia ya ulichotoa (bila shaka unakumbuka hilo andiko). Na tena nikakumbuka lile andiko la kila apandacho mtu ndicho atakachovuna, basi nikapiga hesabu zangu pale, kwamba endapo nitatoa elfu moja basi nitarajie kupokea laki moja (bila shaka sijakuacha hata kama ulikimbia hesabu, elfu moja mara mia ni laki moja). Sijui kama unaelewa maana yake nini upo sekondari unatarajia kupokea laki moja ya kwako binafsi (hahahaha). Nikawaza tu nikiipata hiyo laki moja napanda elfu kumi, sasa piga hesabu hapo elfu kumi mara mia, mavuno ni kiasi gani? (tajiri mtoto anayechipukia).
Japo unaweza kucheka, inawezekana umewahi kuwaza hivyo pia. Kanuni moja muhimu sana kuhusu fedha ambayo huwa haifundishwi na leo nataka niigusie ni kanuni ya uzalishaji bidhaa au huduma (The law of production). Pamoja na kwamba sadaka na maombi ni muhimu sana kwa ustawi wa mtu; ni ukweli uliowaza kwamba hakuna aliyefanikiwa kiuchumi kwa mambo hayo TU (bila uzalishaji huduma na bidhaa) isipokuwa aliyepo upande wa kupokea.  Wazo kuu tunalotaka ulipate kwa siku ya leo ni kwamba, ukitaka kufanikiwa kiuchumi hauwezi kukwepa uzalishaji bidhaa au huduma kwa namna moja au nyingine.  Nioneshe anayeuza bidhaa au huduma, nikuoneshe mtu atakayefanikiwa kiuchumi. Zalisha huduma au bidhaa ambayo tunauhitaji nayo, na sisi tutakuwa tayari kukupa fedha kwa kuipata bidhaa/huduma hiyo kwa sababu tunaihitaji na hapo mafanikio ya kiuchumi yatakuwa dhahiri kwako.
Mungu ameahidi mvua ya Baraka, sio mvua ya fedha. Mungu ameahidi kushusha Baraka kwenye kazi ya mikono yako, kapu lako na chombo chako cha kukandia unga, mifugo yako, mazao shambani kwako, hakuna mahali ameahidi kushusha fedha toka juu. [Kumbukumbu la torati 28:4-5, 8]. Kusubiri mavuno ya sadaka uliyopanda tangu mwaka juzi ili utoke kwenye mkwamo wa kiuchumi uliona sasa, ni uvivu wa kufikiri, na ni kukosa uwajibikaji (irresponsibility).
There’s a place for you at the top!

0 comments :

USIWAPELEKE MAHALI USIPOWEZA KUWATOA

10:09:00 PM Unknown 0 Comments

 
USIWAPELEKE MAHALI USIPOWEZA KUWATOA
Hili ni jambo la msingi kwa kiongozi wa ngazi yoyote ile, haijalishi ni ngazi ya familia, kata, kampuni, taasisi binafsi au kiongozi wa siasa. Kuna maeneo ukiwafikisha watu au ukiwapeleka unaowaongoza hautaweza kuwatoa wote kwa usalama. Kiongozi lazima awe na kipimo cha madhara na uathirika unaoweza kujitokeza kabla ya kuchukua uamuzi wake.
Kwenye biblia kuna kisa cha Lutu aliyemuita Ibrahimu mjomba. Huyu baada ya kuipeleka familia yake katika miji ya Sodoma na Gomora alishindwa kuwatoa wote. Huko alimpoteza mkewe.  Alitamani waokoke familia nzima kama walivyoingia lakini hakuweza. Ingawa haijaandikwa lakini nina hakika Lutu alijisikia vibaya kumpleleka mkewe mahali asipoweza kumtoa. Sodoma ilikuwa ni uchaguzi wa Lutu nyakati za kutengana na Ibrahamu, haukuwa uchaguzi wa mkewe Lutu. Lakini mkewe Lutu akatazama nyuma yake, akawa nguzo ya chumvi.” Mwanzo 19:26
Rais Obama aliyekuwa kinara katika kuangusha Serikali ya hayati Rais Gadafi wa Libya alinukuliwa akijutia kushindwa kuijenga Libya mpya. Obama amewafikisha watu wa Libya mahali ambapo hawezi kuwatoa. Mpaka ameondoka hajaweza kujenga Libya mpya aliyoahidi na badala yake imekuwa pango la magaidi na wapiganaji.
Amesisitiza mwenye hekima mmoja kwamba, “In life you cannot undo every action” akimaanisha, “Katika maisha si kila kitu unaweza kukirejesha tena katika uhalisia wake.” Kuna akili zilizoharibika, kuna familia zilizoharibika, kuna vikundi vilivyoharibika; kuna jamii zilizoharibika, pia kuna kampuni zilizoharibika na si wote watakao weza kufanya urejesho. Kwa kuwa zoezi la urejesho ni gumu na zito basi ni busara kuepuka uovu, tabia hatarishi na mazingira yake. Huwezi kuepuka moshi ikiwa unapika kwa kuni, kwa hiyo katika kubadilisha mwenendo huwezi kupuuza mchango wa mazingira yako. Mazingira hatarishi ya Sodoma na Gomora ndio chanzo cha uharibifu wa mke wa Lutu.
Kama baba wa familia au kiongozi (Lutu) ni lazima uogope maamuzi au maeneo ambayo huna uhakika kwamba, wale unaowaongoza watatoka salama. Yuko rafiki anayeweza kukufundisha tabia mbaya ambayo huwezi kuiacha, yako makundi mabaya ambayo yanaweza kukufundisha tabia hatarishi ambazo huwezi kuzikomesha. Je, unamkumbuka uathirika uliingia lini maishani mwako? Ulevi, ubwiaji wa unga na dawa za kulevya, utazamaji wa picha chafu na uasherati? Ni baada ya kujisamehe sisi wenyewe ndipo tunapoweza kumsogelea Yesu mwanamapinduzi ili atusamehe na kutupa upya.
Watu wengi wamekuwa wanamwogopa Yesu kwa kuwa ni mwanamapinduzi na wanajua wakimsogelea atapindua tabia zao na atapanda tabia njema. Mwanamke Msamaria aliyekutana na Yesu kwenye kisima cha Yakobo alikuwa na uathirika. Alikuwa amekuwa na wanaume watano, that was an addiction! Na kwa muda ule mfupi Yesu alipindua maisha yake.
Muda, afya njema, ufahamu, malezi ya watoto, umoja na mshikamano ni moja ya mambo ya kulinda sana kwa kuwa hayarejeshiki kirahisi na pengine hayarejesheki kabisa baada ya kuharibiwa.
Jilinde!

0 comments :

Utimilifu wa kusudi lako......

8:25:00 PM Unknown 0 Comments

 
UTIMILIFU WA KUSUDI LAKO UTAHITAJI MAFUNGO
Ni kwa zaidi ya miaka mitatu sasa Programu yetu (Life Minus Regret) imekuwa kazini katika kuwasaidia watu kujua makusudi ya kuumbwa kwao na kuyaishi. Tumekuwa tukiwahamasisha vijana wamjue Mungu ili naye awaambie wao (vijana) ni akina nani. Ni Mungu aliyemwambia Yeremia, “nimekuweka uwe nabii wa mataifa” ni Yesu aliyemwambia Petro, “lisha kondoo zangu”, na baadaye akamwambia tena, “chunga kondoo zangu.” Hawa wote walipata kuambiwa kazi zao na wito wao kwa sababu walitafuta kumjua Mungu na kuhusiana naye.
Mambo matatu ni muhimu katika kuhusiana na Mungu; kusali, kufunga na kutoa sadaka. Yesu akasema “nanyi msalipo…,” maana yake anategemea tutakuwa tunasali mara kwa mara, tena akasema, “nanyi mfungapo….” Pia akihimiza “nanyi mtoapo sadaka…” Haya matatu aliyafundisha kwa kuwa yote ni muhimu kufanyika mara kwa mara ili kumkamilisha mtu. Mathayo 5:2, 5, 6 na 16
Sala, sadaka na mafungo ni vitu muhimu katika kuhusiana na Mungu. Katika eneo la sala na sadaka wengi wanajitahidi, changamoto iko katika eneo la ushindi na mafanikio ambalo ni eneo la kufunga. Wengi hupanga kufunga na kabla siku haijafika hughairi na kufakamia chakula. Shetani hatoi ruhusa katika hili kwani anajua lina baraka, tena halijali idadi.
Mafungo ni muhimu kwa ajili ya huduma yako na kusudi lako. Kama Yesu angeweza kutimiza kusudi lake bila mafungo asingelifunga. Alifunga siku 40 kwa sababu ilikuwa muhimu. Huduma nyingi huzaliwa kipindi cha mafungo. Huduma ya mitume waliotengwa yaani, Barnaba na Sauli ilikuwa ni baada ya maombi na mafungo. Matendo ya Mitume 13:2
Jentezen Franklin katika kitabu chake cha: “Fasting” anakiri huduma yake ilizaliwa kipindi cha mafungo, Mchungaji Oyadepo na wengine wengi huelezea jinsi mafungo yalivyofungua njia katika wito wao na makusudi ya Mungu maishani mwao.
Ukiweza unaweza kukataa kula chochote kile kwa muda fulani. Pia katika kufunga unaweza kataa chakula cha nguvu yaani, wanga na ukashinda siku yako yote ukinywa maji tu au chai tu. Siku hizi nikifunga huwa nakunywa maji tu, hii huondoa maswali kwa wanaonizunguka kujua kwamba nimefunga au sikufunga. Usifunge na kujinyima vimiminika kiasi cha kukosa nguvu ya kuomba. Unaweza kunywa chai au juice pekee kwa saa 12 au 24 na hayo ni mafungo mazuri kwani nina hakika utakuwa na nguvu katika kuomba na kusali wala hutaomba kwa ulegevu.
Usichokijua nyuma ya mafanikio ya watu wengi wakuu ni yako mafungo na sadaka. Mafungo hufanya mwili na nafsi visielekee kwenye chakula na badala yake vimwelekee Mungu. Kuna jambo bado halijatimia katika huduma na wito wako nalo litahitaji mafungo. Ni muhimu kwa kukupa upenyo na kukufungulia yaliyofungwa.
Barikiwa

0 comments :

Furahia Maisha Yako

11:09:00 AM Unknown 0 Comments

 
FURAHIA MAISHA YAKO!!
Mungu ametuumba si tu kwa ajili ya ibada na kazi, bali hata kwa ajili ya kufurahia maisha haya. Kutembelea fukwe, kula vizuri, kusafiri, kushiriki matukio ya furaha na pengine hata kuwa na mitoko ya hapa na pale kwa wale wapendanao. Alisema Ratan Tata yule mmiliki wa kiwanda cha kutengeneza magari ya TATA, “Hakuna faida yoyote ikiwa utapanda cheo siku ambayo mnatengana na mpenzi wako…maisha hayahitaji uwe shupavu na makini kiasi hicho” alimaanisha mafanikio ya kazini yaende sambamba na furaha ya nyumbani, tukichukulia maisha kuwa magumu sana kila siku itakuwa ni mapambano bila ya pumziko.
Biblia inaweka wazi katika kitabu cha Mhubiri 3:13, “tena ni karama ya Mungu kila mtu apate kula na kunywa, na kujiburudisha kwa mema katika kazi yake yote.” Napenda mstari ulivyotafisiriwa kwa lugha nyingine, “It is a gift of God to enjoy the good of all his labor”.
Mungu anapenda kila mtu apate muda wa kufurahia matokeo ya kazi zake. Baada ya kazi nzito ni furaha, partying and enjoying!!! Hatuna maana kwamba mioyo yetu izame katika anasa la hasha! Bali kuwe na muda wa kupumzika na kufurahia maisha ambayo ni zawadi kutoka kwa Mungu.
Maneno ya Reba Mc Entire huwa ni ya kuchekesha lakini yana maana alisema, “to succeed in life you just need a wishbone, backbone and a funny bone”. Ni kweli kabisa kila siku ni lazima tuwe na msingi wa kutumaini na kutamani yajayo lakini ni lazima ucheshi na furaha viwe kama uti wa mgongo wa mafanikio yetu.
Namna rahisi ya kufurahia haya maisha ni kuwa sababu ya wengine kufurahi. Katika mchakato wa kufanya watoto, majirani, mke, mume, binti wa kazi, au mfanyakazi mwenzio afurahi utajikuta wewe mwenyewe unafurahi. Furaha inatabia ya kurudi kwenye chanzo chake, hakikisha unakuwa chanzo cha furaha.
Maisha haya si marefu kiasi kwamba tukumbatie huzuni, ukiishi miaka 50 unamapumziko ya Jumamosi na Jumapili 2500 tu na inawezekana zimeshapungua, kama una mika 25 umeshatumia nusu ya majuma hayo. Jipange.
Enjoy…………
Kwa makala nyingine nyingi kama hizi tembelea; www.lifeminusregeret.blogspot.com

0 comments :

Uvivu na Uuaji

2:30:00 PM Unknown 0 Comments

UVIVU NA UUAJI.
Maneno haya mawili si rahisi kuyatenganisha, ni kama chanda na pete. Uvivu una hasara kubwa sana na matokea yake ni uuaji. Utaua karama yako au kipaji chako, utaua mtaji na pengine utapoteza yale ambayo wengine waliyasumbukia kwa muda mrefu na walikupatia wewe uyaendeleze.
Uvivu haufanyi tu ukose yale unayoyatamani kuyapata bali unakupokonya hata lile dogo ulilonalo tayari. Muuzaji hodari atachukua wateja wa yule dhaifu na mvivu katika biashara. Kile usichokitunza huondoka na hii ni kanuni wazi. Kile usichokilinda kitaibwa hii haipingiki, ndio maana ikananenwa shika sana ulichonacho.
Nyakati za mfalme Sulemani katika maandiko, yuko mama aliyemlalia mtoto wake na kumuua kisha kugombea mtoto wa mwenzake. Alilala wakati wanawake wenzake hupumzika tu maana wanajua mtoto ni muhimu kwao kwa saa 24. Ni uzembe wa hali ya juu kusinzia hadi kuua mtoto uliyemsumbukia kwa muda mrefu (1Wafalme3:19). Inawezekana wewe na mimi tukiendelea kulala kuna vitu vitakufa. Rafiki yangu mmoja aliwahi kuniambia, “Alphonce, vijana hatulali tunapumzika tu” Ukipenda usingizi utaua ndoto zako na hatma yako.
Siku nyingine nikajifunza kuachana na neno sana. Nakushauri pia uondoe neno “sana” katika misamiati yako. Nimechoka sana, nimesoma sana, nimetembea sana ni sentensi zenye kuhalalishi na kutoa udhuru wa kutofanya kitu kinachotakiwa au cha ziada. Hii ni dalili ya uvivu, neno sana lazima liondoke. Aliyechoka sana atatamani kulala sana lakini aliyechoka atatamani kupumzika na kurejea tena ulingoni. “So avoid using the word ‘very’ because it’s lazy
Mwingine anaweza kuwaza, Uvivu ni nini? Ni ile hali ya kughairisha mambo. Nitafanya jioni, nitafanya kesho na hatimaye nitafanya mwakani. Uvivu pia ni hali ya kushindwa kuzingatia jambo moja, ni kuitawanya akili katika mambo mengi ambayo pengine si ya msingi. Uvivu pia ni ule uoga unakuja wakati wa kupanga mipango mikubwa na migumu na hivyo mtu kwa kujihurumia anajipangia mipango midogo na ya kawaida sana. Mvivu anakubali huondoka mapema hata kama kazi haijaisha, kamwe hapambani mpaka mwisho.  Kwa hiyo uvivu ni ile hali ya kuishia njiani.
Inawezekana umepoteza fursa nyingi na sasa huna cha kushika. Lile neno shika sana ulichonacho halina tena nguvu kwako maana huna cha kushika. Usiogope, Yesu Kristo aliye ufufuo na uzima na kweli anaouwezo wa kufufua yaliyokufa. Yeye alimwita Lazaro aliyekufa na akatoka mzima. Kwake huyu Mungu mwenye nguvu, na Mfalme wa ajabu twaweza kuomba, Ee Bwana fufua kazi zako ndani yetu.
Amka sasa uangaze….


0 comments :