Wapi niende kujenga fikra mpya

3:06:00 PM Unknown 0 Comments

WAPI NIENDE KUJENGA FIKRA MPYA
Renew your Thinking
Kwa wiki mbili mfululizo tumekuwa tukiandika kuhusu Fikra. Wapi uende, nini ufanye na kwa nini kubadilisha mfumo wa kufikiri. Kesho yetu haitaweza kubadilika kama bado fikra zetu zinafanana na jana.
Tunavaa mavazi tuliyoyawaza jana usiku, tunaenda mahali tulipowaza kabla ya kwenda. Usipobadili mfumo wa kufikiri huwezi kubadili mwenendo wa maisha. Kwanza, ni muhimu kuwa walau na dakika kumi kila siku jioni au asubuhi kwa ajili ya kukaa kimya na kufikiri. Ni muhimu kila siku upate muda wa upekee na ukimya (shut from the world) ili uweze kujitathmini na kufikiri kwa upana.
Fikra ni chakula inategemea unakula wapi. Ukila picha za ngono utakuwa mjinga, ukila udaku utakuwa na mambo yakufanana na udaku, ukila majarida ya matangazo ya pombe utakuwa mtumwa wa pombe.
Twende kwenye jambo safi, tujifunze kwenye kitabu kizuri, channel safi ya Luninga, kikundi cha busara cha WhatsApp. Usione haya kutoka kwenye kundi ambalo halina maadili. Usiogope kuchana na kuchome picha na majarida yenye kuharibu akili. Mambo ya uasherati na ulevi huharibu akili.
Imenenwa, “aziniye na mwanamke hana akili kabisa” tena ikanenwa, “mambo ya ulevi huharibu ufahamu” mambo haya huharibu ufahamu na kufanya uwezo wa mwanadamu wa kuamua na kufikri kupungua.
Hatupaswi kutafakari kila jambo, bali yale tu tuliyojifunza na kuyaona yanafaa kwa kutafakari. Ushindi wote wa mwandamu uko katika tafakari. Mungu alimwambia Joshua atafakari neno lake mchana na usiku na azungumze hilo neno kila siku. Kwa kufanya hivyo ushindi ulidhihirika katika maisha ya Joshua mwana wa Nuni. Joshua 1:8
Dunia inataka watu wajanja. Lakini maandiko yanataka kabla hatujawa wajanja tuwe watu safi, wasio na waa lolote mbele za Mungu. Daniel ni mmoja wa watu safi, alionekana na akili mara kumi kuliko waganga na wachawi. Mtume Paulo amesisitiza nini tufikiri kama tunataka kuwa wajanja na safi (pure and smart in all our way) “Mambo mliyojifunza kwangu na kuyapokea, na kuyasikia na kuyaona kwangu, yatendeni hayo; na Mungu wa amani atakuwa pamoja nanyi.” Flp 4:9
Mazoezi ya kutenga muda wa kufikiri, kujizoeza kusoma neno la Mungu na kuacha makundi mabaya kutabadilisha kabisa namna yako ya kufikiri. Barikiwa.

0 comments :

Kama si Kompyuta Basi ni Roboti

9:56:00 PM Unknown 0 Comments

 
KAMA SI KOMPYUTA BASI NI ROBOTI
(Tumia akili yako kufikiri vema)
Dunia iko kwenye kasi kubwa ya mabadiliko ya sayansi na teknolojia. Mabadiliko haya ni muhimu sana, nchi ambazo ziko mbele katika mabadiliko haya watu wake huishi maisha marefu. Si ajabu kwa Japan, Korea kusini na Kaskazini raia wake kuwa na wastani wa umri mrefu wa kuishi. Mabadiliko haya humpa mwanadamu muda wa kupumzika kwa kuwa humwondoa kwenye majukumu ya kutumia nguvu na kumwachia jukumu zito la kufikiri. Sayansi na teknolojia ni muhimu katika afya ya binadamu, usindikaji na ujenzi wa miundombinu.
Kazi kubwa ambayo mwanadamu anapaswa kubaki nayo ni kufikiri. Mabadiliko na mapinduzi hayawezi kutokea ikiwa hatukupindua sehemu iliyoko katikati ya sikio la kulia na sikio la kushoto yaani, ubongo. Kazi za mazoea kama vile kubeba mizigo, kubaki mizigo, kuandika hati, kusikiliza na nyinginezo zifananazo na hizi zinaweza kufanywa vizuri kama sina kompyuta basi ni roboti.
Hivi karibuni Japan wamezindua roboti ambaye huangalia watoto nyakati za usiku. Bila shaka roboti huyu akifika Afrika atanyang’anya kazi za watu wengi katika shule na maeneo ya malezi ya watoto. Kupitia masomo ya walimu wabobezi yaliyoko mitandaoni, “you tube” na katika maeneo mengine ya kuhifadhia itafika mahali hatutahitaji tena kukutana na mwalimu ana kwa ana. Mungu alitaka tuishi kwa kufikiri, tutumie utashi wetu. Kufikiri hakupitwi na wakati, mwenye fikra njema anaweza kushinda kipimo cha muda (time test).
Tabia za mazoea na kazi za mazoea ni rahisi kufanya kwa kutumia teknolojia pasipo kumhitaji mtu awaye yote. Tabia hizi za mazoea huua ubunifu na uwezo wetu wa kufikiri. Wastaafu wengi wanaotoka kwenye kazi zisizosumbua ubongo hushindwa kumudu maisha mapya ambayo huhitaji fikra mpya na mawazo mkakati. Fedha yao ya kustaafu huwa kama magurudumu mapya katika injini iliyoharibika kabisa. Ni wazi Teknolojia inawafukuza watu wengi kazini kuliko tumbua tumbua ya vyeti feki. Uzuri wake ni kwamba inarahisisha utendaji na ina ajiri watu wengi zaidi wanaoifahamu zaidi ya wale inaowafukuza.
Ni muhimu tuusukume ubongo na ufahamu wetu ili tupate mawazo na fikra endelevu za kutuwezesha kwenda sambamba na sayansi na teknolojia. Ni muhimu kukumbatia teknohama kuliko shahada za vyuo vikuu. Nchi za wenzetu zinapunguza udahiri vyuo na zinahimiza ufundi ili tu zikuze ujuzi na matumizi ya sayansi na teknolojia katika maisha ya kila siku.
Ile kwamba, mtakula kwa jasho haikuzuii kufunga kiyoyozi na kula kwa damu ya Yesu iliyovunja laana zote. Jasho ni matokeo ya ugumu wa kazi ni muhimu fikra zetu zituletee njia rahisi, zenye kugharimu muda mchache, rasilimali chache na ubora wa juu. Tukutane katika msimu mpya wa Weekend of Purpose. Barikiwa!!  

0 comments :

Mungu Hahitaji Kufikiri

11:50:00 AM Unknown 0 Comments

 
MUNGU HAHITAJI KUFIKIRI
MIMI NA WEWE TUNAPASWA KUFIKIRI
Mungu mwenyezi anazo sifa nyingi, ni Mungu aliyeumba majira na nyakati, nchi na vyote viijazavyo ni kazi ya mikono yake na ni mali yake. Hakuna historia wala yajayo ambayo yamefichika machoni pake. Anayejua mambo yote ya sasa, yajayo na yaliyopita. Ni Mungu wa nyakati zote, za sasa na zijazo. Mbele yake hakuna siri. Ndio maana imeandikwa, “maana naijua mipango niliyonayo kuwahusu ninyi, asema BWANA, ni mipango mizuri si mibaya” (Tafsiri yangu kutoka Yeremia 29:11)
Mwanadamu anahitaji kufikiri ili kuleta majibu kwenye changamoto inayomkabiri au inayokikabiri kizazi chake. Kunapokuwa na namna tatu, mwanadamu anahitaji kufikiri ili kupata namna moja ambayo ni bora zaidi. Kunapokuwa na njia tatu, mwanadamu anahitaji kufikiri ili kupata njia moja ambayo itampendeza Mungu, haitaharibu mazingira wala hamtamdhuru jirani yake. Baada ya kufanikiwa kupiga hatua kubwa kwenye mambo teknohama dunia sasa inahitaji kufikiri kuhusu usalama wa mazingira, hali ya joto Duniani na usalama wa vizazi vijavyo.
Fikra sahihi zinatupa nafasi ya kufanya maandalizi ya mambo yajayo. Usipofikiri kuhusu yajayo yatakapokuja yatakukuta huna maandalizi yoyote, kwa hiyo hautaweza kusimama katika nyakati hizo. Kwa mtu makini hakuna nyakati za furaha kama nyakati za mwisho ambazo tumezoea kuziita, “future
Tabia za mazoea huua uwezo wa kufikiri. Kuna mambo ambayo hujulikana na yamezoeleka haya hayadai fikra mpya katika utekelezaji wake. Wale wanafunzi ambao huamka, hula chakula, huenda darasani, kisha kuoga na kulala huwa hawana jipya maana hurudia matendo hayo kila siku. Wale ambao huamka, hufanya sala, kisha zoezi, kisha usafi, kisha masomo, kisha kuimba kwaya, kisha siasa za shuleni, kisha uongozi wa shule huwa watu bora zaidi kuliko wale wenye mambo machache na madogo kama sisimizi.
Kizazi cha sasa kinahitaji mageuzi makubwa kifikra, walio wengi wanalipwa kwa sababu ya muda wanaotumia kazini. Hawalipwi kwa sababu ya matokeo, wala kwa sababu ya akili bali wanalipwa kwa sababu ya mahudhurio yaani, muda fulani mpaka muda fulani. Tunahitaji kuhama, Shift from being paid for your time to being paid for your mind!
Akili inachuja na kuchekecha, inapima na inatoa majibu. Akili inakupa uwezo wa kufika mahali kimawazo  ambapo miguu yako haijawahi kupakanyaga kimwili. Biblia iliposema, “ uishi na mwanamke kwa akili” ilitaka ujue kwamba, hauna taarifa za kutosha kumuhusu kwa maana wewe si Mungu wake, ilitaka ufike mahali kimawazo ikiwezekana kabla yeye hajafikia maana akikutangulia kufika inawezekana usimwelewe, ilikutaka ujizoeze kufikiri, kuchambua, na kupima matakwa yake na mazingira yake. Kwa kufikiri unaweza kupambanua kati uongo na ukweli.
Kwa uzoefu wangu mdogo vijana wale walikuwa na ufinyu wa fikra miaka ile tulipokuwa shuleni hata sasa mtaani utawakuta na kibano cha fikra na mara nyingi hawa watu ni watiifu sana kwa historia, dini za mababu na ni wapesi kurithi mila na desturi zilizopo, wala hawajisumbui kuzikosoa pale zinapopwaya, mara nyingi watu hawa hupenda sana kusifia watawala, they cannot challenge the conventional knowledge!
Kwa nini tunahitaji kufikiri? Katikaa kitabu cha, “Teach your Child How to Think” mwandishi Edward de Bono ameeleza wazi, “Tunahitaji kufikiri kwa sababu hatuna taarifa za uhakika kuhusu mambo ya baadaye, tukiwa na taarifa kamili na mambo yote yakiwa wazi na utupu mbele yetu hatutakuwa na haja ya kufikiri maana kila kitu kitakuwa wazi”. Hii ndio sababu imenifanya niamini Mungu hahitaji kufikiri, hawezi kujiuliza itakuwaje ilhali anajua kila kitu.
Karibu katika, Weekend of Purpose ya April, 2018 na tuandikie katika email na blog yetu.
Bwana Mungu Akubariki,

0 comments :

Ongeza maarifa katika eneo maalum

5:37:00 PM Unknown 0 Comments

ONGEZA MAARIFA KATIKA ENEO MAALUMU
Kama ilivyo kawaida, mwanzoni mwa mwaka kila mtu anaweka malengo yake au mambo anayotaka afanikiwe au afanikishe katika kipindi cha mwaka huo. Pamoja na kwamba si kila mtu ana utaratibu wa kuandika malengo yake ya mwaka, lakini karibu kila mtu huwa na malengo au mambo analiyopanga kufanikisha katika mwaka.  Nafahamu baadhi yetu tumeweka malengo ya kusoma vitabu katika mwaka huu mpya (kama hujaweka lengo la kusoma vitabu, basi hujachelewa kufanya hivyo), hili ni jambo jema kwa kila mwenye uwezo wa kusoma.
Pamoja na mipango na malengo yako mengi uliyojiwekea kwa mwaka huu mpya, leo nataka nikupe hamasa juu ya jambo moja, nalo ni kuweka nia au malengo ya kuongeza maarifa/ujuzi na ufahamu katika eneo mahususi au maalumu katika maisha yako. Yaani badala ya kuweka lengo la kusoma tu, weka pia ni eneo gani unalotaka kuongeza ujuzi au maarifa ili kuliboresha.
Mwenyehekima mmoja amewahi kusema "Usishibishe njaa yako, shibisha maono yako [don’t feed your hunger, feed your vision]"; huu ni ushauri mmoja wa hekima ambao nimewahi kuupata kuhusu usomaji katika kuishi kwangu. Lengo hapa ni kukuepusha na tabia ya kusoma kila kinachokuja mbele yako bila malengo mahususi wala mpangilio utakao kusaidia kupiga hatua zaidi katika maisha ya kila siku. Mtu anaweza kupanga mwaka huu nataka nisome vitabu 30 au 20, lakini ukimuuliza unataka kusoma kuhusu nini au kuhusu eneo gani, ni wachache sana wanamajibu yanayoeleweka (concrete answer)
Ili kusoma kwetu kulete badiliko katika maisha yetu na mazingira tuliyopo ni muhimu ukachagua cha kusoma ukilenga kuboresha eneo mahususi katika maisha yako. Na hapa utapata fursa ya kufanya tathmini kuona kama unasogea, na kama kusoma kwako kuna kuletea faida inayoweza kupimwa [measurable results].
Kumbuka, huwezi kusoma vitabu vyote vilivyoandikwa, hivyo basi lazima ujue nini cha kusoma na nini cha kuacha hata kama kina sura nzuri, ili mwisho wa mwaka useme kwa kusoma vitabu au kwa kujifunza ujuzi fulani nimepiga hatua hii; kiuchumi, kiroho, mahusiano, ufanisi kazi, huduma, ubora wa kazi zangu n.k
There’s a place for you at the Top

0 comments :