Mtu mgumu kutawalika

2:17:00 PM Unknown 0 Comments

 
MTU MGUMU KUTAWALIKA
Ni rahisi sana kutazama wengine na sisi wenyewe tukasahau kujitazama na kujitathmini. Tunaweza tukayajua sana mapungufu ya wengine na tukasahau wapi tunapungua. Imenenwa, “Unakiona kibanzi kwenye jicho la nduguyo na unaacha kutazama boriti ndani ya jicho lako”.
Profesa na Mhadhiri wa chuo kikuu cha Havard cha Nchini Marekani bwana Bill George anaandika hivi katika moja ya vitabu vyake, “The hardest person you will ever have to lead is yourself”.
Wewe ndio mtu usiye tawalika, wewe ndio mtu mgumu kwa viongozi wako. Mara nyingi tumezoea kusema ni fulani na kujisahau kwamba, tunayo mapungufu makubwa. Kwangu mimi mtu mgumu kumtawala ni mimi, na wewe ni vema ujijue vema.
Miili yetu inaasili ya kutokutawalika. Ukipanga mpango wa kuacha michepuko unaweza kushuhudia vita dhahiri ambayo mwili unainua, hali kadhalika unapopanga kufunga. Biblia inasema, “Ifungeni dhabihu kwa kamba kando ya madhabahu”. Imenenwa pia, “Itoeni miili yenu kama dhabihu”. Kwa nini sadaka ifungwe kwa kamba? Isipofungwa itagoma au itakimbia. Isipofungwa haitawaliki.  Warumu 12:1-3
Kufungwa ni kulazimisha, kutia adabu, kufanya tena na tena mpaka maadili mema na utii uwe sehemu ya maisha yetu. Ni ngumu ni lazima ukaze. Wachichanji wanajua, ili uchinje nguruwe unahitaji kufanya kazi, ili utoe fungu la kumi unahitaji kujua kuacha matamanio binafsi na kuwa mtii kwa Bwana.
Tukutane juu.

0 comments :

Chagua kuendelea mbele

12:52:00 PM Unknown 0 Comments

 
Chagua Kuendelea Mbele
Mara nyingi tunapokutana na changamoto katika kufikia yale tuliyopanga au kutazamia; tunaweza kuchagua mambo mawili tu, kusonga mbele au kukata tamaa na kutafuta sababu ya kulaumu na kughairi kuendelea mbele! Kile utakacho kiamua baada ya kukutana na changamoto ndicho utakachokipata baada ya changamoto hiyo kupita.
"Ukifikiri kama unaweza au hauwezi, upo sahihi "
Yaani ukifikiri na kuona kama jambo fulani unaliweza au utaweza basi ujue upo sahihi; na ukiona au kufikiri jambo fulani hauliwezi au hautaliweza basi ujue upo sahihi pia!  Na hii ndio sababu inayofanya wengine waendelee mbele na wengine kuishia kulalamika na kughairi kuendelea 'utukufu' ulio mbele yao
" Bwana akamwambia Musa, Mbona unanililia mimi? Waambie wana wa Israeli waendelee mbele" Kutoka 14 :15
Siri ya kufanikiwa wakati wa changamoto sio kurudi nyuma au kukata tamaa, siri ya mafanikio ya kweli ipo katika kuendelea mbele. Thomas Edison, mwanasayasi na mgunduzi amewahi kusema "Our greatest weakness lies in giving up. The most certain way to succeed is always to try his one more time " (Udhaifu wetu mkubwa upo katika kukata tamaa; njia ya uhakika kufikia mafanikio ni kujaribu mara nyingine: Tafsiri isiyo rasmi)
Kumbuka jambo hili, Haukuanza ili uishie njiani! Ndio, narudia tena haukuanza ili uishie njiani hivyo chagua kuendelea mbele. Mwenye hekima mmoja amewahi kusema, unapochoka usiache (usikate tama); jifunze kupumzika (ili upate nguvu ya kuendelea). Don't stop because you're tired, stop when it's done!
There's a place for you at the top

0 comments :

Mheshimu Rais Wako

2:20:00 PM Unknown 0 Comments

MHESHIMU RAIS WAKO
(Ni kwa Heshima ya aliyemweka katika kiti hicho)
Ukiwa mtawala au mmiliki wa biashara unaweza kumweka yeyote asimamie biashara hiyo kwa niaba yako, asimame kama mwakilishi wako. Mwakilishi huyu bila shaka atakuwa na amri (authority and power) kwa wale utakao waweka chini yake ili awaongoze na kuwasimamia vema. Mwakilishi huyu akidharauliwa bila shaka wewe uliyemweka umedharauliwa pia. Serikali  haziwekwi na wapiga kura, zinawekwa na Mungu. Maeneo mengi tumeshuhudia wenye kura nyingi wakikosa Urais. Wanademokrasia wenye imani wanaelewa hili.
Tunapaswa kuwaheshimu viongozi si kwa sababu ni wema au ni wabaya bali, ni kwa heshima ya yule aliyewaweka watuongoze yaani, Mungu Baba. Ameandika Mchungaji Kenneth Copeland, “Hakukuwa na Serikali korofi kama ile ya wakati wa Yesu Kristo, lakini bado Yesu alitaka iheshimiwe na akasema, ‘yaliyo ya Kaisari apewe Kaisari.’” Kwa maneno mengine Kristo aliwataka watu walipe kodi kwenye Serikali ambayo kimsingi ilikuwa inawakandamiza, hata wao hawakuamini kama Yesu amesema waheshimiwe kama Serikali. Serikali yaweza kuwa dhalimu lakini Mungu aliyeiweka kwa majira husika si dhalimu, na anamakusudi nayo.
Muda mzuri wa kuiheshimu Serikali ni pale inapofanya vibaya, maana ikifanya vema hata wapagani huiheshimu (Luka 6:28). Muda mzuri wa kubariki ni pale watu watakapo kulaani. Katika agano la kale Serikali ya Farao yule wa wakati wa Musa ilikuwa korofi na yenye kiburi hata mbele za Mungu, lakini Mungu alisema ni yeye aliyeiweka kwa makusudi yake. Kuna kusudi kwa serikali yako. Serikali haijiweki madarakani inawekwa. Katika Warumi 9:17 neno nimekusimamisha linaweza kuwa na maana, nimekuweka. Kwa maana maandiko yasema juu ya Farao, ya kwamba, Nilikusimamisha kwa kusudi hili, ili nionyeshe nguvu zangu kwako, jina langu likatangazwe katika nchi yote.Warumi 9:17
Tunamuheshimu mkuu wa nchi  kwa sababu tunayo hofu ya Mungu aliyemweka. Si kila Mtawala (Boss) anastahili heshima kutokana na tabia yake, wengine wanatabia mbaya. Pamoja na hayo kila Mkristo anapaswa kutoa heshima kwa kila mtawala bila kujali tabia yake.
Angalizo:
Katika kumtii kiongozi lazima tuhakikishe hatumkosei Mungu, kiongozi asigeuke sanamu moyoni mwetu. Sauti ya kiongozi ikiwa kinyume na injili ya Kristo na ipuuzwe. Mijadala mambo ya mapenzi ya jinsia moja, mauji ya holela, utoaji wa mimba unaohalalishwa kisheria, ndoa za mitala ni mambo ambayo ni kinyume na injili. Yapuuzwe hata kama msemaji atakuwa ni mkuu wa Nchi.
Mungu anaweza kubadilisha moyo wa kiongozi ikiwa watu watasimama kuomba. Maombi kwa Mungu mwenye nguvu yanaweza kuelekeza nchi wapi ielekee ikiwa mwombaji ataomba kwa bidii. Mungu anaendesha mioyo ya watawala kupitia maombi ya watakatifu.
Endelea kuombea nchi yako….., Shallom Israel, Shallom Tanzania….


0 comments :

Uzuri unadanganya

10:08:00 AM Unknown 0 Comments

UZURI  UNADANGANYA.
(Beauty is fleeting)
Nimewahi kupewa ushauri kutoka kwa watu mbalimbali kuhusu masuala ya mahusiano na ndoa. Nimejitahidi pia kusoma walau vitabu kadhaa. Yote kwa yote kuhusu ndoa na mahusiano sitasahau ushauri huu, “uzuri/urembo unadanganya.” Kwa nini unadanganya? Kwa sababu si wa kudumu, na si kitu utakachokihitaji kila siku.
Si vema kumpuuza mtu mwenye hekima anapofumbua kinywa chake kusema kitu. Solomon mtu mwenye hekima sana ndiye aliyesema katika Mithali 31:30, “uzuri si wa kudumu” Yaani sura, mpangilio wa meno, rangi na umbo zuri havisemi kweli maana baada ya muda mtu huzeeka na ngozi hukunjamana, na mara urembo wote hutoweka. Maana yake uonavyo leo sivyo itakavyokuwa milele. Kwa lugha nyingi si mambo utakayoyahitaji baadaye. Baada ya muda kupita utagundua haukuhitaji sura bali ulihitaji, upendo, ushirika, amani na uaminifu. Kwa nyakati tofauti wachungaji na wenye hekima wameonya kwamba,kufanya uamuzi kwa kujali mwonekano wa nje ni hatari.
Amesema mwenye hekima huyu, “Mwanamke aliye na umbo zuri na sura nzuri pasina maarifa kichwani afaa kwa usiku mmoja, lakini yule mwenye ufahamu na maarifa afaa kwa maisha yote.” Ndoa ni agano la maisha si la usiku mmoja. Mwonekano wa nje hautoshi kutoa taswira ya ndani ya utu, uchapakazi, uaminifu na upendo.
Urembo ukisimama peke yake hautoshi, utanashati peke yake hausaidii. Haipasi kuwa urembo na utanashati, badala yake inafaa kuwa urembo na akili, urembo na uchapakazi, urembo na ibada, urembo na upendo, urembo na uaminifu.
Ili urembo usikudanganye basi ni lazima uwe umeujua ukweli. Tafuta watu wanaoheshimika utagundua si kwa rangi zao wali si kwa urembo na utanishati wao bali ni kwa kujitoa sadaka, kuishi maisha ya heshima, uaminifu na utu wema.
Wewe si Mr. Tanzania unaanzaje kuoa Miss Tanzania? Urembo unadanganya. 
Tukutane kileleni………

0 comments :