USHINDI UPO NDANI YAKO, SIO NJE

9:30:00 AM Unknown 0 Comments


 

USHINDI UPO NDANI YAKO, SIO NJE!

Nimewahi kumsikia mtu akisema kwamba, Ikiwa watu elfu watasema unaweza lakini wewe ukajiambia nafsini mwako na kuamini kuwa hauwezi, kufanikisha jambo fulani au kufanikiwa katika eneo fulani la kimaisha; uwezekano wa wewe kuja kufanikiwa katika eneo hilo ni mdogo sana sawa na hakuna. Na ikiwa watu elfu watasema hauwezi lakini wewe ukasema nafsini mwako na kuamini kuwa utafanikiwa, basi mafanikio huwa dhahiri baada ya muda tu.
Ni ukweli usiopingika kwamba, ikiwa mtu ataona ushindi ndani yake ni rahisi kuona ushindi katika maisha ya kila siku; na ikiwa mtu hataona ushindi ndani yake basi uwezekano wa kuona ushindi nje ni nadra sana sawa na hakuna. Na hapa ndipo panapo tofautisha kati ya mshindi na mshindwa, aliyefanikiwa na aliyeshindwa, anayesonga mbele na anayekwama.
“Maana aonavyo nafsini mwake, ndivyo alivyo” Mithali 23:7
Jambo kuu tunalotaka upate hapa ni kwamba, kama kuna mahali au eneo unataka kuona ushindi katika maisha yako basi utambue kuwa ushindi upo ndani yako sio nje, yaani ushindi huanzia ndani yako. Hauwezi kushinda nje kama haujaweza kushinda ndani yako kwanza. Kumbe hatuwezi kuona badiliko lolote la kudumu kiuchumi au kifedha au kihuduma endapo ndani yetu hatuoni wala kuamini kama tunaweza kufanikiwa na kupata badiliko hilo. You must feel and see it before you realize it.
Njia kuu moja wapo ya kukuwezesha kuona ushindi ndani yako katika eneo fulani la kimaisha ili kuupata ushindi huo nje ni kusikia, kile unacho ruhusu [kusikika] ndani yako ndicho hupata nafasi katika maisha yako. Sauti [maneno] unayoisikiliza au uliyoipa ruhusa ndani yako ndio huamua hatima yako. Hauwezi kujidhihirisha kama samba endapo ndani unajiona kama swala. Ukiona ushindi utaongea kama mshindi, utatembea kama mshindi; ukiona kushindwa hauwezi kuwa na ujasiri na kuongea kama mshindi.
Unapoona ushindi ndani yako, na ukakutana na changamoto akili hupata nguvu ya ziada na kuanza kutafuta namna ya kuondoa au kutumia changamoto hiyo ili kufikia ushindi, lakini kama ndani huoni ushindi, umekata tama akili ‘inaparararizi’ na inakosa nguvu ya kufikiri namna ya kuondoa au kutumia changamoto, hata changamoto ndogo akili huona mlima mkubwa. Na hapa ndipo panapo tofautisha katika ya mshindi na mshindwa, aliyefanikiwa na aliyeshindwa, anayesonga mbele na anayekwama. Ndani ya moyo wako unaona nini? Unachoona ni muhimu sana, kwa sababu kinaweza kukukwamisha au kukufanikisha.
There’s a place for you at the top

0 comments :