Changamoto kwa viongozi vijana

2:09:00 PM Unknown 0 Comments

 
CHANGAMOTO KWA VIONGOZI VIJANA
(Usimzuie mtu kufanya mabaya, ana uhuru)
Changamoto kubwa inayowasonga viongozi vijana ni kumilikiwa. Kuna hatari ya viongozi vijana kumilikiwa au kuongoza kwa akili za walioko nje ya ulingo. Kuna umuhimu wa viongozi vijana kuonesha umakini mkubwa na kipekee.
Ili kummiliki kiongozi kijana watu hutumia vitisho nini kitampata au nini hakitampata. Mara nyingi wenye roho hii (spirit of manipulation) husema, fanya hivi ili upendwe na watu au usifanye hivi watu watachukia. Watu wenye roho hii hutoa hakikisho feki, humwakikishia mtu usalama ambao kimsingi ni Mungu peke yake atupaye kukaa salama katika kazi, biashara na vyeo. Katika amani nitajilaza na kupata usingizi mara, Maana Wewe, Bwana, peke yako, Ndiwe unijaliaye kukaa salama.” Zaburi 4:8
Yesu alijua Petro anaroho hii ambayo hutoka kwa shetani. Petro alimwita Yesu Kristo pembeni akimwonya kwamba, mateso hayatampata. Mara nyingi wenye roho hii hupenda kumbana mtu pembeni, humwita kipekee bila ya watu, hutoa onyo hilo kwa siri.
Ingawa Yesu Kristo alikuwa kiongozi kijana hakusita kumkemea Petro kwamba, “rudi nyuma yangu shetani”. Nakusihi kijana usiruhusu kumilikiwa kinyume na kusudi la kuumbwa kwako, usizuiwe kutekeleza yale ambayo Mungu amekuitia kutekeleza. Mathayo 16:23
Nakumbuka nikiwa kiongozi kijana mtu mmoja aliniita akinikemea na kunieleza fanya hivi au vile, na mara moja nikawa mkali nikamwambia, “Mimi ni mtu wa kanuni, sipangiwi nifanye lipi na lipi nisifanye bali napanga mwenyewe.”
Yes, I am a man of Principle! Nilijibu hivyo waziwazi kwa sababu nilijua ubaya wa roho hii ya kumiliki watu, nilikuwa nimeitafakari usiku wa kabla ya tukio. Mtu anaruhusa ya kuchagua hata mabaya, uhuru wa kuchagua (freedom of choice) ni muhimu kwa kila jamii ya kistaarabu. “Because to take away a man’s freedom of choice, even his freedom to make the wrong choice, is to manipulate him as though he were a puppet and not a person” Madeleine L’Engle
Imani hufanya watu wamilikiwe lakini maarifa huwaweka huru. Hakuna anayeruhusiwa kumiliki utashi na dhamira ya mwanadamu. Hata viongozi wa dini hawaruhusiwi. Mwanadamu ni kiumbe huru, na anapaswa kuamua apendacho.
Endelea kutembea katika uhuru wako, Mungu alimtuma mwenaye kukuokoa na shetani ili uwe huru wala si ili uwe milki ya viongozi wa dini, siasa au serikali.  Kumiliki watu ndio uchawi wa kisasa ambapo mtu hafanyi kitu bila ya kupiga simu au kuomba kibali kwa wanadamu.
Amesema Joyce Meyer, Ukiwa na shida nenda kwenye kiti cha enzi cha Mungu, usikimbilie kupiga simu. (Go to throne not to the telephone) Mtegemee Mungu na yeye atakuwa ngome yako, ngao yako, na kigao wala hautaondoshwa. 
Barikiwa.

0 comments :

Rafiki Mpya, Mambo Mapya

11:29:00 AM Unknown 0 Comments

  
RAFIKI MPYA, MAMBO MAPYA
(Angalia ingizo la rafiki mpya)
Imenenwa katika Mithali 28:24: “Aibaye mali ya babaye au mamaye, na kusema, Si kosa; Mwana huyo ni rafiki wa mtu mharibifu.”  Ziko tabia au mambo ambayo yanapotokea kwako au kwa rafiki yako yanataka kukuonesha kwamba umejiunga na rafiki mwovu au kikundi kibaya.

Mtoto akipata rafiki wabaya atamwibia babaye, kadhalika mtumishi akipata marafiki wabaya ataiba mali ya ofisi (mali ya BOSS). Kuchukua kitu cha nyumbani kwenu bila ridhaa ya wazazi ni wizi, kuchukua mali ya ofisi bila utaratibu si haki. Ukiona mtu anamkono mrefu, anaiba mali za kwao au ya kampuni inayomlipa mshahara ujue amepata marafiki wabaya.
Ukiona mtazamo wako juu ya amri za Mungu unabadilika (huoni yaliyokatazwa) basi jiulize ni nani ameingia katika maisha yako. Ukiona mtazamo wako juu ya mume/mke wa mtu unabadilika basi jiulize ni nani unashinda naye kila siku.  Rafiki mpya huleta tabia mpya, nzuri au mbaya.
Kuna watu wanasema kuiibia serikali si dhambi, hawa ni rafiki ya watu waovu, kuna wanaosema mume/mke ni wa kwako akiwa ndani tu, hawa nao ni rafiki ya waasherati. Biblia inakataa kitendo cha kuiba na kusema ni kosa, yuko mwizi anayejua wizi ni kosa na yuko mwizi aliyehalalisha wizi na haumii tena kwa sababu kitendo hicho kwake si dhambi.
Marafiki wabaya hufanya hata dhambi ionekane kama si kosa, humbadilisha mtu akili ili autazame uovu kama wema. Biblia inasema, “aibaye na kusema, si kosa, ni rafiki ya mtu mharibifu.” Mharibifu wa nini? Mharibifu wa akili. Mithali 28:24
Yuko pia aziniye na kusema si kosa, yuko atoaye rushwa na kusema si kosa, yuko atorokaye shuleni na kusema si kosa, yuko pia adanganyaye na kusema si kosa!
Wazazi wengi wamekataa watoto wao wasihusiane na vijana waharibifu. Wanaharibu akili, wanageuza moyo, na hivyo mtu huangamia bila kujua. Katika kuwapima marafiki tujifunze kwa Yesu: Hawa ni wanafunzi watatu marafiki wa Yesu; Petro mtu wa imani ndiyo yule Kefa, mwanafunzi msemaje aliyesema kuwa, Yesu ni Kristo, Yohana alikuwa mtu wa upendo sana ndiyo yule aliyelala kifuani pa Yesu, na Yokobo mtu mwenye tumaini saana ndiye yule alitufundisha dini njema ya kuona wagonjwa na kulisha masikini. Kwa kuzungukwa na hawa watatu Yesu alichagua kuwa salama ki akili. Alizungukwa na mwenye upendo, imani na tumaini.
Wewe pia ni wastani wa watu wako watano wa karibu, Angalia tabia zako mpya, ujue mchango na uwekezaji wa kitabia ulifanywa na rafiki zako katika maisha yako. Ikiwa haiwezekani kuwashauri kubadilika achana nao, Cut off the link! Usitoe muda wako kwa marafiki wabaya, Mungu akupe neema ya kuachana nao na kujitenga.
Tukutane juu pamoja na watu wako watano wa karibu sana.

0 comments :

Unatatua changamoto gani?

9:19:00 PM Unknown 0 Comments

 
UNATATUA CHANGAMOTO GANI?
Ili kuishi maisha yenye hamasa, swali muhimu unalotakiwa kujiuliza sio unataka kufanya nini katika maisha yako ya kuwa hapa duniani bali unatakiwa kujiuliza ni changamoto gani au tatizo gani unataka kulitatua katika kuishi kwako? Moja ya sifa kuu ya kufanana kwa watu wote waliofanikiwa ni utatuzi wa changamoto; nioneshe mtu aliyefanikiwa nikuoneshe changamoto anayotatua au aliyotatua katika kuishi kwake. Katika ulimwengu huu, usitafute jambo la kufanya; tafuta changamoto ya kutatua.
Kila aliyezaliwa na mwanadamu amebeba jawabu la changamoto fulani; kwa sababu mafanikio ya kweli yamebebwa katika kuleta majibu juu ya changamoto au upungufu uliopo mahali fulani. Watu hawatakufuata wala kukulipa kwa sababu una kipawa au ujuzi au uwezo fulani ndani yako, watu watakufuata na kuwa tayari kukulipa kwa sababu kipawa chako, ujuzi wako na uwezo wako unatatua changamoto walionayo. Thamani yako mbele ya watu inategemea kiwango chako cha utatuzi wa changamoto walizonazo watu hao.
Boresha uwezo wako wa kutatua changamoto.
Kila mara ni muhimu kuboresha uwezo wako wa kutatua changamoto, ndio maana hata watengenezaji wa simu kila mara huboresha simu wanazotengeneza kwa kuziongezea uwezo wa kutatua changamoto mbali mbali. Ndio maana utasikia iPhone 5 mara iPhone 6 mara “iPhone 6 plus”. Wanachofanya hapa si kutengeneza simu nyingine bali ni kuboresha simu iliyotengezwa hapo awali. Na kwa sababu hiyo thamani ya iPhone 6 plus ni kubwa kuliko thamani ya iPhone 6 ya kawaida. Na watu wako tayari kulipa zaidi kwa iPhone 6 plus kuliko iPhone 6 ya kawaida kwa sababu “iPhone 6 plus” imeboreshwa uwezo wake wa kutatua changamoto ya mawasiliano. 
Kuna namna nyingi za kuboresha uwezo wako wa kutatua changamoto katika eneo lako la huduma, biashara, tekinolojia, uongozi, elimu ulipata, uandishi, ofisini, kipawa, michezo (athletes); baadhi ni kwa kutafuta ujuzi zaidi, ‘kupractice’ zaidi, kujifunza kwa waliokutangulia, kujifunza kwa waliofanikiwa, kusoma vitabu vinavyohusiana na eneo umalotaka kulifanyia kazi n.k. Wazo kuu hapa ni kujitahidi kuwa bora zaidi ya jana, tafuta kuwa bora (excellent) katika kila ulichoweka nia ya kukifanya.
There’s a place for you at the top

0 comments :

Ndio maana haukuweza

11:45:00 AM Unknown 0 Comments

 
NDIO MAANA HAUKUWEZA
Zingatia Uhalisia Gal 6:7
Imewatokea wengi kushindwa kufikia malengo, ni jambo la kawaida kwa wengi kushindwa kupungua uzito, si ajabu kwa wanafunzi kufeli mtihani. Kila unaposhindwa jitahidi kurudi kwenye misingi. Wakristo wengi wameanguka katika dhambi na kwao ni muhimu kurejea katika misingi.
Mambo hayatokei yenyewe tu, na kama wakristo tunahitaji miujiza na si maajabu. We need miracles not magic! Maajabu yako hata kwa waganga wa kienyeji, maajabu ni kupata pesa bila kufanya kazi, kufaulu bila kusoma, kahaba kuolewa au asiyehaki kuinuliwa. Ni ajabu kwa anayekula kupita kiasi kupungua uzito.
Miujiza ni tofauti na maajabu. Miujiza inakutaka ushirikiane na Mungu, miujiza inatualika tuungane na Mungu. Miujiza ni mchanganyiko wa sala na kazi, pia miujiza ni mchanganyiko wa imani na matendo. Miujiza hutokea pale watu wanapoamua itokee. Amesema Joel Osteen “Ni imani yetu ndiyo huamsha nguvu ya Mungu”.
Ili muujiza utokee lazima pawepo na imani, sala, mafungo, bidii ya kazi upendo na amani. Upendo unachagiza sana uwepo wa muujiza. Ofisi ambayo upendo umetawala watu watamaliza kazi kwa wakati (finishing before deadline). Maajabu hutokea tu bila sababu, lakini miujiza inahitaji muda, uwekezaji, bidii na upendo. Mungu wetu ni mtenda miujiza (miracles) si maajabu (magic). Kama hauna muda na mpenzi wako usitarajie muujiza wa amani na upendo bali tarajia maajabu ya amani na upendo. Galatia 6:7
Maajabu yanafanya muuzaji mwenye lugha mbaya apate wateja, muujiza hutokea pale muuzaji mwenye busara na kauli nzuri anapopata wateja wengi na kuuza sana sana. Waganga wa kienyeji (chief magic promiser) hawakufundishi huduma nzuri kwa wateja bali wanawahadaa wateja na kufanya upate usichostahili. Usiende kwao, wala kwa wasoma nyota. Wagalatia 6:7
Hata biblia imekataa, kuvuna usipopanda, kupewa usichoomba, kupata usichostahili. Wengi tunao ujuzi wa kutufikisha kileleni, lakini hatuna maarifa ya kutufanya tudumu hapo. Haifai kupenda kuona maajabu. Maajabu hayawezi kudumu maana hata hatujui kwa nini hutokea. Lakini muujiza wa Yesu ukitokea na sisi tunajua tukitimiza yanayotakiwa utatokea tena. Siku moja mpwa wangu alimuona Pastor Chris akiwapuliza watu wanaanguka baadaye na yeye akafanya na akapata matokeo yale yale. Siku za mbeleni nami pia katika kuombea watu nikafanya nikapata matokeo yale yale.
Ushindi ni tabia, mafanikio ni tabia pia. Soma biblia na tazama tabia za waliotendewa miujiza utakuta zinafanana. Si rahisi kuushinda ulimwengu kama bado haujajishinda mwenyewe, si rahisi kuaminiwa na watu ikiwa bado haujimini wewe mwenyewe. Madhara ya kutokujiamini ni sawa sawa na kutokumwamini Mungu.
Batromayo kipofu alihakikisha anapaza sauti na Yesu akamsikia licha ya kelele za umati mkubwa, Zakayo alipanda juu ya mti ili amwone Yesu, mama aliyetokwa na damu alipenya katika ya kundi la watu maana haikuwa rahisi kumgusa Yesu. Muujiza unataka ujipange, uwe juu ya viwango vya watu, muujiza utataka upige kelele mpaka Yesu asikie, muujiza unataka upenye katikati ya watu katika usaili.
Mara ya kwanza ulipoimba vizuri Mungu alitaka ujue kipaji chako, pale ulipohubiri vizuri Mungu alitaka ujue wito wako, pale ulipotengeneza bidhaa nzuri Mungu alitaka ujue kazi yako lakini utambulisho huo haukusaidii kama hautendi hivyo mara kwa mara. Kwa mshindi kushinda ni mazoea, kipaji chako kikiwa tabia yako hapo utadumu. 
Wiki hii ikawe mwanzo wa miujiza katika maisha yako katika jina la Yesu Kristo. Amen

0 comments :