Kipaji chako ni hiki hapa

1:34:00 PM Unknown 0 Comments

 
KIPAJI CHAKO NI HIKI HAPA
(Katika taabu ni rahisi kujua kipaji chako halisi)
Nani ni nani Tanzania, Kuna watu wanafuatana na utambulisho wao, Mchango wao na karama zao zimewatambulisha. Who is who in Tanzania? Sheikh Shaaban Robert amejulikana kwa mashairi, Askofu Moses Kulola amejulikana kwa injili, Rose Mhando amejulikana kwa nyimbo za injili. Wewe unautambulisho gani?
What is your Identity? Tunaposhindwa kujua utambulisho wetu kupitia karama na makusudi ya kuumbwa kwetu tunapoteza maana ya kuishi. Na hapa siku tukiimba vizuri tutafikiri sisi ni waimbaji na siku tukifundisha vizuri tutafikiri sisi ni walimu. Tatizo hili limewasumbua wengi na limekuwa likijulikana kama, The Crisis of Identity, ni hali ya kutokujua utambulisho wetu na mchango wetu kwa jamii.
Ukitaka kukosa mshindi katika mchezo wa mpira wa miguu usimpige refa bali ondoa magoli na hivyo kutakuwa hakuna sehemu ya kufunga na tayari mpira utapoteza ladha. Kingine unachoweza kufanya ni kuweka nguzo nyingi za magoli (yaani badala ya mbili weka nne). Malengo mengi maishani ni usumbufu. Kuwa na malengo mengi hakukupi nafasi ya kuwa mshindi ndio maana kila timu hufunga katika goli moja tu. Maisha bila ya kuwa na lengo kuu la kufanikisha hayana ladha. Ndio maana ni muhimu kujua kusudi lako na kipaji chako. 
Kipaji halisi hujidhihirisha wakati wa taabu, wakati ambao uko peke yako bila ya ulio wazoea. Unachopenda kufanya gizani bila ya kuhimizwa na mtu kinaweza kuwa kipaji chako nuruni. Kipaji cha ubondia hugunduliwa nje ya ulingo na ulingoni ni sehemu ya udhihirisho tu.
Yusufu alitabiri Gerezani, Paulo na Sila waliimba na kumsifu Bwana wakiwa gerezani mpaka milango ya Gereza ikafunguka. Je! kipaji chako kinadhihirika wakati wa shida? Kipaji halisi hakinyamazishwi na mazingira magumu.
Kipaji au karama ya Mungu huonekana hata katika taabu, Yesu aliendelea kuhubiri, kuponya na kuokoa hata akiwa msalabani. Don’t be silenced by problems
Nimeona Mungu akiponya kwa uponyaji mkuu katika mazingira ambayo sikuwa hata na utayari. Siku chache zilizopita tumeshuhudia Boss mkubwa aliyeachishwa kazi TANESCO akiendelea na kuhubiri injili. Kawaida ya kipaji halisi ni nyenzo inayotumika hata katika taabu, kamwe hainyamazi. Umri haunyamazishi kipaji chako, ana miaka 82 ya kuzaliwa bado Jimmy Swaggart anaimba, kupiga kinanda vizuri na kufundisha.
Wako wakimbizi waliotumia vipaji vyao ugenini, wako watumwa waliotawala utumwani. Wako wafanyakazi wa ndani walioishia kuwa wafalme. Ni baada ya kugundua vipaji vyao na kuvitumia hata katika mazingira magumu. Endelea kutumia kipaji chako usikate tamaa.
Mazingira magumu yanapaswa kukuhamasisha kutumia kipaji chako na si kukitelekeza kipaji chako. Kwa tafsiri yangu Paulo alimaanisha hivi, “…chochea kipaji ulichopewa na Mungu kilicho ndani yako.” 2 Tim1:6
Kileleni ndipo tunapopatikana

0 comments :