Unatakiwa Kwenda

5:41:00 PM Unknown 0 Comments

 
UNATAKIWA KWENDA
Toka ulipo, piga hatua
Mathayo 7:7, Ombeni na dumuni katika maombi, tafuteni mpaka mpate, bisheni na kuendelea kubisha hodi mpaka mfunguliwe. Maneno yote haya yanaonesha umuhimu wa kupiga hatua ili kupata (It’s about a constant movement to achieve), hatutafuti katika eneo moja bali tunatafuta popote mpaka tupate. Wachache tu ndio walioitwa wafanikiwe mahali walipo, wengi wameitwa ili waende mahali fulani. Kuna mafanikio makubwa kwa wale watakao amua kwenda. Mwaka huu ni wako, unaitwa kwenda shule, kwenda mji fulani, kujiunga na chuo fulani, kwenda katika kikundi fulani au nchi fulani.
Katika kwenda kwako utafanikiwa. Umeitwa kwenda kwa watoto, kwenda kwa masikini, wagonjwa na wanafunzi. Kila mtu ameitwa kwa ajili ya watu fulani, wanaharati wameitwa kwa ajili ya haki na uhuru wa raia na wanafanya hivyo kwa nguvu zao zote. Wako walioitwa katika biashara, uongozi, uchungaji, uimbaji na uinjilisti, na wanapaswa kwenda. Nenda ukaanze mwaka huu.
Musa aliwaendea wana wa Israel hawakuwapo alipo yeye, Yesu alitujia ulimwenguni akitokea mbinguni, Wakoma waliliendea jeshi la washami na mama Theresa aliwafuata masikini wa Calcutta nchini India. Inakupasa kuwaendea, usisubiri wakufuate. It’s all about going!
Reinhard Bonnke alitoka Ujerumani akaja Africa, Hudson Taylor alitoka kwao akaenda China kama Mmisionari akiacha hata mchumba wake aliyesusa kuondoka. Ibrahimu alitoka kwa Tera babaye akaenda mahali alipoitiwa na Mungu. You have to move!
Mamia ya watu wanaothubutu kuondoka na kuanza jambo hufanikiwa, na hii ndiyo roho waliyonayo waasisi wa mataifa na makampuni. Kuliko kufia kitandani kwako ni afadhali kufia barabarani katika njia yako kulekea mafanikio yako.
Ni muda wa kusimama, ni muda wako wa kutoka nyuma na kusogea mbele. Kuna nyakati moja nilikuwa safarini nikitafakari huku nikiwa nimechoka na hali ya masiha yangu (status of life) na niliwaza kama ndoto zangu zitatimia au hazitatimia na zimekufa. Naye Mungu akanijibu kwa wimbo, “mwota ndoto hafi mpaka zimetimia”. Ndivyo ilivyokuwa kwa mwota ndoto Yusufu, kwa mwota ndoto Barack Obama, kwa mwota ndoto Nelson Mandela na ndivyo ilivyo kwako ikiwa unandoto za kufanya jambo fulani zuri la kushangaza dunia.
Usiishi bila dunia yako, jiunganishe na kujiambatanisha na watu, watu ni kila kitu kwa mwota ndoto. Haruni ni muhimu kwa Musa, wenye dhambi ndio wateja wa duka la Yesu, masikini ndio wateja wa wanasiasa, wagonjwa ndio wateja wa madaktari. Tambua ulimwengu wako, uendee, jiambatanishe nao.
Ukubwa ni namna unavyotumikia kundi uliloitiwa na Mungu, na jinsi mwalimu anavyowatendea wanafunzi wake. Tukutane mwezi wa tano, usikose Weekend of Purpose, msimu huu wa tano BWANA amekuandalia mambo motomoto kuhakikisha unafanikiwa na ndoto zako zinatimia.
Barikiwa……

0 comments :