Tumia akili zako ....

4:32:00 PM Unknown 0 Comments

 
TUMIA AKILI ZAKO VIZURI WALA HAZITACHAKAA
Zitumie, usizitumaini.
Akili zako zitaimarika kwa sababu ya kutumika wala hazitachakaa. Akili huchakaa kwa kutokutumika wala si kwa kutumika. Tofauti na akili, Vitu vingi huchakaa pale vinapotumika sana (subjected to wear and tear), vifaa vingi hupungua uwezo wake wa kazi na ufanisi kwa sababu ya kutumika. Vingine hupungua hata thamani. Akili huimarika kwa kutumiwa na mwenye nazo. Usizihurumie akili zako, watoto wadogo wanauwezo wa kujua lugha zaidi ya saba na wala akili zao hazichakai. Wanaweza kuongea; kijerumani, Kiswahili, kifaransa, Kiingereza, kihispania; Kichina, Kitaliano na kireno. Unaweza ukaona jinsi akili yako ilivyolala kwa kushika na kutenda mambo machache.
Siri ya mafanikio iko katika moyo wa kila kitu. Ni wajibu wetu kujua undani wa kila jambo na kutafuta usahihi wake kabla ya kuliendea. Kufeli kunaanza kwa kufanya usichokijua au kuungana na usiyemjua vizuri, au kwenda njia moja na usiyemjua au ofisi ambayo maono yake hayajulikani. Know the heart of the thing that you want to pursue!
Luka mwinjili alitafuta kwa tafiti kujua moyo wa injili na habari za Yesu. Alitafiti kabla ya kuandika, alitafiti kabla kuamini na kuwaaminisha wengine. Aliandika baada ya kupata kujua usahihi wake: “nimeona vema mimi nami, kwa kuwa nimejitafutia usahihi wa mambo hayo yote tangu mwanzo, kukuandikia kwa taratibu, Theofilo mtukufu,” Luka 1:3
Kama unataka kufanikiwa katika siasa jitahidi kusoma na kufanya tafiti ili kujua usahihi wa siasa. Kama unataka kufanikiwa katika ndoa lazima ujue usahihi wa ndoa, vivyo hivyo katika ugunduzi na uvumbuzi, uimbaji, uinjilishaji na kadhalika.  Wakati mwingine walioko katika medani hizo watakupa kuujua undani wake kama utakaa nao vizuri. Wengine wako Ulaya ila kupitia vitabu vyao na kaseti zao unaweza kukaa nao na kujua usahihi wa tasnia zao. Kwa vitabu mimi hukaa na Benny Hinn, Mike Murdock na Jimmy Swaggart.
Kila siku binadamu anafanya maamuzi (hutumia akili) zaidi ya elfu tatu (3000) lakini kwa sababu mengi ni ya mazoea si rahisi kugundua kwamba akili kubwa imetumika. Tunapanga tuvae nini, tule nini, twende wapi, tufanye nini na nani na wapi.
Maamuzi haya madogo na mazoea hayatujengi sana kwa kuwa hayushughulisha sana akili ukilinganisha na kufanya tafiti, uvumbuzi na ufumbuzi wa matatizo. Kila mtu amezaliwa kutatua tatizo fulani kwa haiba yake, mwonekano wake na vionjo vyake. Ndio maana si vizuri kujaribu kumuumba upya mtu ambaye tayari amesha umbwa na BWANA Mungu.
Hivyo ulivyo unafaa kwa kutatua jambo fulani katika jamii yako, shuleni kwako, au kazini kwako. Mkimya anafaa kwa uongozi wa ngazi ya sera, “policy level” kama Musa, wakati msemaji anafaa kwa utendaji wa kila siku kama Haruni. Kwa hiyo tunawahitaji watu wa vionjo vyote, maandiko yanasema watu wakali humiliki mali, they are strict
Ile kwamba unafanya maombi haina maana kwamba, usipime, usifanye utafiti, wala haina maana kwamba usipeleleze taarifa za hiyo biashara, za hiyo kazi, au za huyo mtu. Ile kwamba umeomba haina maana kwamba, usiulize waliokutangulia katika tasnia hiyo, ile kwamba unaimani haina maana usisome. Use your brain to trace and investigate! Kuna nyakati nilikataa kufanya kazi kwenye ofisi za tumbaku kwa akili ya kawaida tu, kwamba wanauza saratani. Matokeo ya sigara ni saratani kwa hiyo kama mkristo sikuwa na haja ya kufanya maombi bali kutumia akili tu kujua matokea.
Mungu hajaondoa wala hajasitisha matumizi ya macho, masikio, pua, mdomo na ubongo. Kuna nyakati nyingine fahamu za mwanadamu ziko sahihi wala huhitaji maombi hapo. Ndiyo, “God does not set aside our natural faculties”.
Tukutane kileleni …………. usikose msimu wetu wa tano.

0 comments :