Usijihurumie; Fanya kazi

11:10:00 AM Unknown 0 Comments

 
USIJIHURUMIE
Fanya kazi
Kama kuna mtu ambaye angestahili kukaa na kutokufanya shughuli yoyote basi ni malkia wa Uingereza na familia yake, Elizabeth II mwenye miaka 90 sasa. Nina hakika wewe si wa kifalme kama yeye na familia yake, lakini huenda watoto na wajuu zake, wanawajibika zaidi kuliko wewe. Wanajishughulisha na kujihatarisha kuliko wewe. Katika ukoo wake wako wanaorusha ndege, wako waliokaa jeshini muda mrefu. Wana kila kitu lakini bado wanachagua kazi na uwajibikaji. Prince Harry amekaa miaka kumi katika vikosi vya jeshi. Watoto wa watawala wengi wangetamani kuwa barabarani kila siku na magari ya kifahari, labda na kujihusisha na porojo za mitaani. Sivyo ilivyo kwa jamaa ya Elizabeth II.
Kazi ni heshima, tena kazi ni baraka. Mungu aliumba kazi kabla hata Adamu hajafanya dhambi, kwa hiyo kazi haina uhusiano na laana, kazi ilikuja kabla ya laana, Adamu alipangiwa kazi ya kulima na kutunza bustani kama sehemu ya baraka. Kula kwa jasho kulikuja baadaye sana, kukakomeshwa na msalaba wa Kristo. Mwanzo 2:15
Kanuni ya kazi inakutaka uanze na ulichonacho. Kama ni nguvu zitumie, kama ni pesa tumia kama mtaji, hakuna kichache kisichotosha kuanzia. Wote huanza kwa hatua moja. Mtaji wa masikini si nguvu zake tu, ni pamoja na akili zake mwenyewe. Kama umekaa muda mrefu bila kupata kazi unaweza kuwasaidia ofisi iliyojirani na nyumbani kwenu, ili kama hawakulipi kiasi chochote urejee kula chakula cha nyumbani. Unaweza kujiunga pia na masomo ya bodi, ni rahisi kwa mtu anayesoma masomo ya bodi kupata kazi kwa urahisi kwa kuwa anakuwa masomoni, akili yake hukumbuka mengi na huwa na ujuzi unaofanana na wakati halisi.
Malkia ambaye kimsingi anapata pesa nyingi kutoka serikali yao na angepaswa kukaa tu lakini bado anafanya yafuatayo kama yalivyoripotiwa na gazeti la Business Insider UK; “Alitimiza matukio 341 yaliyoko kwenye kalenda yake ya mwaka 2015 , analea vituo 600 vya misaada (charities) na yeye na timu yake wanajibu barua laki moja kwa mwaka wanazoandikiwa kutoka kwa watu mbalimbali.”
Maswali ya kujiuliza, Je, unaratiba ya siku? , Je, unaratiba ya mwaka? Unaweza kupanga mipango yako kwa miezi sita ijayo na ukatimiza? Kama hauna ratiba maana yake hauna sehemu ya kujipima (benchmark). Kosa la kuishi siku moja bila tathmini linaweza kupelekea kuishi mwaka mzima bila tathmini. Mtume Paulo alitathmini mpaka maana na muda wa  kwenda kanisani. Si kila anayekwenda kanisani anakwenda kukusanyika kwa faida. Kama unakwenda kanisani na haujengwi maana yake unabomolewa ama kiroho au kifikra.
Kuishi kwa ratiba ni kazi ngumu, hakutoi nafasi ya matukio ya mwendokasi. Ratiba inabana na hivyo wengi wanaona kuliko kibano cha ratiba ni bora waongozwe kwa matukio. Twende pamoja kwa vitendo, chukua karatasi na kalamu. Andika nini utafanya kwa siku ya kesho, kabla ya kulala hiyo kesho ujitathimini. Andika utakachofanya kwa wiki, mwezi hata mwaka. Weka tathmini ya wiki katikati ya wiki (Jumatano), tathmini ya mwezi katikati ya mwezi (tarehe 15) na mwisho wa mwezi, na tathmini ya mwaka iwe kila baada ya miezi mitatu (kila baada ya robo).
Mwenye hekima hufanya kazi hata kama mfukoni anapesa nyingi, asiye na hekima hufanya kazi kwa sababu pesa zimeisha mfukoni. Mahitaji ya siku hayapaswi kukupeleka kazini, bali mahitaji ya muda mrefu.
Mwenye hekima huenda kwa ratiba na kalenda, mjinga hajui hata tarehe.
Mabadiliko yanawezekana kabisa. Wewe ni baraka.

0 comments :

Yesu ni Bwana ...

12:51:00 PM Unknown 0 Comments

 
YESU NI BWANA WA YOTE NA VYOTE
(Huwezi kuwa bwana wa wachache) 
Jumapili iliyopita (Tar. 16 Aprili 2017) tumesherehekea Pasaka, ni sikukuu kubwa kweli kweli! Pasaka ni sikukuu ya U-Bwana wa Yesu Kristo. Bila Pasaka hatuwezi kumwita Yesu Kristo awe Bwana.
Kanuni za kufanyika BWANA zinamtaka mtu awe BWANA juu ya vyote na juu ya wote. Hakuna uchache, ukiwashinda wachache ni sawa na hakuna. Ndio maana Yesu ni BWANA hadi kwa wasiomjua na kumwamini. Ili uwe BWANA lazima uwashinde wote, na uwaweke chini ya miguu yako wote, wa kabila zote na nchi zote. Ili uwe BWANA ni lazima ushinde magonjwa, Yesu hakuwahi kuugua, ili uwe BWANA ni lazima ushinde dhambi, Yesu hakutenda dhambi. “bali alijifanya kuwa hana utukufu, akatwaa namna ya mtumwa, akawa ana mfano wa wanadamu; tena, alipoonekana ana umbo kama mwanadamu, alijinyenyekeza akawa mtii hata mauti, naam, mauti ya msalaba. Kwa hiyo tena Mungu alimwadhimisha mno, akamkirimia Jina lile lipitalo kila jina;” Wafilipi 2:8-9
Mapema kabisa katika siku zake YESU Kristo aliwashinda maadui zake wote. Alimshinda adui, dhambi, mapepo, umasikini, laana, balaa na mikosi. Maadui wa mwanadamu ndio walikuwa maadui wa Kristo Yesu. Alibakia adui mmoja tu jina lake mauti.
Sheria za U-bwana zinabana sana. Hata ukiwashinda adui wote akibakia mmoja bado wewe hautapewa ubwana. Sheria inataka asisalie hata mmoja ambaye hujamkanyaga miguuni pako. Ni kama alivyofanya Daudi kwa kuwapiga adui zake wote, asisalie hata mmoja.
Adui aliyekuwa amesalia ni kifo na tunaposherekea Pasaka tunafuraha kwani Yesu Kristo ameshinda kifo cha kiroho na cha kimwili. Pasaka inamtangaza Yesu kuwa BWANA wa vyote na wa wote kwa kuwa hakuna kilichosalia tena ambacho hajakishinda. Katika pasaka Yesu anashinda kilichosalia ambacho ni kifo. Baada ya hapo hakuna adui mwingine tena machoni pa BWANA YESU KRISTO.
Pasaka ni pigo la ushindi, ndio maana jiwe lilikutwa mbali, maana shujaa Yesu Kristo alitoka kwa ushindi.
Ukubali au ukatae Yesu Kristo atabaki kuwa BWANA. Hakuna tena kuitisha uchaguzi ili watu waamue awe BWANA au asiwe. Hata nchi yote na dunia yote waamue kukataa, Yesu hatabadilika bali ataendelea kuitwa BWANA na kutawala mbinguni na Duniani.
Yeye ni BWANA si tu juu ya watu bali hata juu ya vitu na hali ya hewa. Ndio maana kwa jina la BWANA Yesu; upepo, UKIMWI, Upofu, na kila hali mbaya hukaa kimya. “Kwa hiyo tena Mungu alimwadhimisha mno, akamkirimia Jina lile lipitalo kila jina; ili kwa jina la Yesu kila goti lipigwe, la vitu vya mbinguni, na vya duniani, na vya chini ya nchi; na kila ulimi ukiri ya kuwa YESU KRISTO NI BWANA, kwa utukufu wa Mungu Baba” Wafilipi 2:9-11
BWANA YESU ASIFIWE…..hiyo ndio furaha ya Pasaka. Hiyo ndiyo sherehe ya Pasaka yaani, U-BWANA WA KRISTO YESU.
Jiandae kwa msimu wa tano wa weekend of purpose, tukutane Dar-es-salaam.
Barikiwa.

0 comments :

Unatakiwa Kwenda

5:41:00 PM Unknown 0 Comments

 
UNATAKIWA KWENDA
Toka ulipo, piga hatua
Mathayo 7:7, Ombeni na dumuni katika maombi, tafuteni mpaka mpate, bisheni na kuendelea kubisha hodi mpaka mfunguliwe. Maneno yote haya yanaonesha umuhimu wa kupiga hatua ili kupata (It’s about a constant movement to achieve), hatutafuti katika eneo moja bali tunatafuta popote mpaka tupate. Wachache tu ndio walioitwa wafanikiwe mahali walipo, wengi wameitwa ili waende mahali fulani. Kuna mafanikio makubwa kwa wale watakao amua kwenda. Mwaka huu ni wako, unaitwa kwenda shule, kwenda mji fulani, kujiunga na chuo fulani, kwenda katika kikundi fulani au nchi fulani.
Katika kwenda kwako utafanikiwa. Umeitwa kwenda kwa watoto, kwenda kwa masikini, wagonjwa na wanafunzi. Kila mtu ameitwa kwa ajili ya watu fulani, wanaharati wameitwa kwa ajili ya haki na uhuru wa raia na wanafanya hivyo kwa nguvu zao zote. Wako walioitwa katika biashara, uongozi, uchungaji, uimbaji na uinjilisti, na wanapaswa kwenda. Nenda ukaanze mwaka huu.
Musa aliwaendea wana wa Israel hawakuwapo alipo yeye, Yesu alitujia ulimwenguni akitokea mbinguni, Wakoma waliliendea jeshi la washami na mama Theresa aliwafuata masikini wa Calcutta nchini India. Inakupasa kuwaendea, usisubiri wakufuate. It’s all about going!
Reinhard Bonnke alitoka Ujerumani akaja Africa, Hudson Taylor alitoka kwao akaenda China kama Mmisionari akiacha hata mchumba wake aliyesusa kuondoka. Ibrahimu alitoka kwa Tera babaye akaenda mahali alipoitiwa na Mungu. You have to move!
Mamia ya watu wanaothubutu kuondoka na kuanza jambo hufanikiwa, na hii ndiyo roho waliyonayo waasisi wa mataifa na makampuni. Kuliko kufia kitandani kwako ni afadhali kufia barabarani katika njia yako kulekea mafanikio yako.
Ni muda wa kusimama, ni muda wako wa kutoka nyuma na kusogea mbele. Kuna nyakati moja nilikuwa safarini nikitafakari huku nikiwa nimechoka na hali ya masiha yangu (status of life) na niliwaza kama ndoto zangu zitatimia au hazitatimia na zimekufa. Naye Mungu akanijibu kwa wimbo, “mwota ndoto hafi mpaka zimetimia”. Ndivyo ilivyokuwa kwa mwota ndoto Yusufu, kwa mwota ndoto Barack Obama, kwa mwota ndoto Nelson Mandela na ndivyo ilivyo kwako ikiwa unandoto za kufanya jambo fulani zuri la kushangaza dunia.
Usiishi bila dunia yako, jiunganishe na kujiambatanisha na watu, watu ni kila kitu kwa mwota ndoto. Haruni ni muhimu kwa Musa, wenye dhambi ndio wateja wa duka la Yesu, masikini ndio wateja wa wanasiasa, wagonjwa ndio wateja wa madaktari. Tambua ulimwengu wako, uendee, jiambatanishe nao.
Ukubwa ni namna unavyotumikia kundi uliloitiwa na Mungu, na jinsi mwalimu anavyowatendea wanafunzi wake. Tukutane mwezi wa tano, usikose Weekend of Purpose, msimu huu wa tano BWANA amekuandalia mambo motomoto kuhakikisha unafanikiwa na ndoto zako zinatimia.
Barikiwa……

0 comments :

Tumia akili zako ....

4:32:00 PM Unknown 0 Comments

 
TUMIA AKILI ZAKO VIZURI WALA HAZITACHAKAA
Zitumie, usizitumaini.
Akili zako zitaimarika kwa sababu ya kutumika wala hazitachakaa. Akili huchakaa kwa kutokutumika wala si kwa kutumika. Tofauti na akili, Vitu vingi huchakaa pale vinapotumika sana (subjected to wear and tear), vifaa vingi hupungua uwezo wake wa kazi na ufanisi kwa sababu ya kutumika. Vingine hupungua hata thamani. Akili huimarika kwa kutumiwa na mwenye nazo. Usizihurumie akili zako, watoto wadogo wanauwezo wa kujua lugha zaidi ya saba na wala akili zao hazichakai. Wanaweza kuongea; kijerumani, Kiswahili, kifaransa, Kiingereza, kihispania; Kichina, Kitaliano na kireno. Unaweza ukaona jinsi akili yako ilivyolala kwa kushika na kutenda mambo machache.
Siri ya mafanikio iko katika moyo wa kila kitu. Ni wajibu wetu kujua undani wa kila jambo na kutafuta usahihi wake kabla ya kuliendea. Kufeli kunaanza kwa kufanya usichokijua au kuungana na usiyemjua vizuri, au kwenda njia moja na usiyemjua au ofisi ambayo maono yake hayajulikani. Know the heart of the thing that you want to pursue!
Luka mwinjili alitafuta kwa tafiti kujua moyo wa injili na habari za Yesu. Alitafiti kabla ya kuandika, alitafiti kabla kuamini na kuwaaminisha wengine. Aliandika baada ya kupata kujua usahihi wake: “nimeona vema mimi nami, kwa kuwa nimejitafutia usahihi wa mambo hayo yote tangu mwanzo, kukuandikia kwa taratibu, Theofilo mtukufu,” Luka 1:3
Kama unataka kufanikiwa katika siasa jitahidi kusoma na kufanya tafiti ili kujua usahihi wa siasa. Kama unataka kufanikiwa katika ndoa lazima ujue usahihi wa ndoa, vivyo hivyo katika ugunduzi na uvumbuzi, uimbaji, uinjilishaji na kadhalika.  Wakati mwingine walioko katika medani hizo watakupa kuujua undani wake kama utakaa nao vizuri. Wengine wako Ulaya ila kupitia vitabu vyao na kaseti zao unaweza kukaa nao na kujua usahihi wa tasnia zao. Kwa vitabu mimi hukaa na Benny Hinn, Mike Murdock na Jimmy Swaggart.
Kila siku binadamu anafanya maamuzi (hutumia akili) zaidi ya elfu tatu (3000) lakini kwa sababu mengi ni ya mazoea si rahisi kugundua kwamba akili kubwa imetumika. Tunapanga tuvae nini, tule nini, twende wapi, tufanye nini na nani na wapi.
Maamuzi haya madogo na mazoea hayatujengi sana kwa kuwa hayushughulisha sana akili ukilinganisha na kufanya tafiti, uvumbuzi na ufumbuzi wa matatizo. Kila mtu amezaliwa kutatua tatizo fulani kwa haiba yake, mwonekano wake na vionjo vyake. Ndio maana si vizuri kujaribu kumuumba upya mtu ambaye tayari amesha umbwa na BWANA Mungu.
Hivyo ulivyo unafaa kwa kutatua jambo fulani katika jamii yako, shuleni kwako, au kazini kwako. Mkimya anafaa kwa uongozi wa ngazi ya sera, “policy level” kama Musa, wakati msemaji anafaa kwa utendaji wa kila siku kama Haruni. Kwa hiyo tunawahitaji watu wa vionjo vyote, maandiko yanasema watu wakali humiliki mali, they are strict
Ile kwamba unafanya maombi haina maana kwamba, usipime, usifanye utafiti, wala haina maana kwamba usipeleleze taarifa za hiyo biashara, za hiyo kazi, au za huyo mtu. Ile kwamba umeomba haina maana kwamba, usiulize waliokutangulia katika tasnia hiyo, ile kwamba unaimani haina maana usisome. Use your brain to trace and investigate! Kuna nyakati nilikataa kufanya kazi kwenye ofisi za tumbaku kwa akili ya kawaida tu, kwamba wanauza saratani. Matokeo ya sigara ni saratani kwa hiyo kama mkristo sikuwa na haja ya kufanya maombi bali kutumia akili tu kujua matokea.
Mungu hajaondoa wala hajasitisha matumizi ya macho, masikio, pua, mdomo na ubongo. Kuna nyakati nyingine fahamu za mwanadamu ziko sahihi wala huhitaji maombi hapo. Ndiyo, “God does not set aside our natural faculties”.
Tukutane kileleni …………. usikose msimu wetu wa tano.

0 comments :

Kutambua uwezo wako, .....

12:07:00 PM Unknown 0 Comments

 
KUTAMBUA UWEZO WAKO; CHUKUA HATUA
(Unlock your potentials)
Hakuna mtu aliyewahi kufikiri kuwa, binadamu anaweza kukimbia mita mia (100) kwa sekunde tisa nukta tano nane (9.58) mpaka pale mwanariadha kutoka Jamaica, Usain bolt alipoweka rekodi hiyo ya dunia katika mji wa Berlin nchini Ujerumani mwaka 2009 ambayo haijavunjwa mpaka sasa. Wala hakuna mtu aliyewahi kufikiri kuwa binadamu anaweza kuruka juu (bila ya msaada wa kitu chochote) umbali wa mita 2.5 yaani zaidi ya futi 8 mpaka pale mwanamichezo Javier Sotomayor (Cuba) alipoweka rekodi ya dunia kwa kuruka umbali huo mwaka 1993.
Watu wote ambao tumeona uwezo wao ukidhihirika hata kutushangaza wakati mwingine, wana namna ya kufikiri ambayo huwatofautisha na watu wengine na hivyo hupata matokeo bora katika kile wanachokifanya kuliko watu wengi.  Je, wewe namna yako ya kufikiri ipoje, je unafiri namna utakavyoshindwa ukijaribu? Namna ambavyo haiwezekani? Kwamba hakuna aliyeweza kufanikiwa katika jambo hilo? Kwamba hapo ulipo imetosha? Au unafikiri namna [njia] ya kushinda/kufanikiwa katika kile unachotaka kufanya? Namna ambavyo utaweza?.
Ile kwamba hakuna aliyeweza jambo hilo kabla yako, haina maana kwamba jambo hilo haliwezekani! Kumbuka hakuna aliyewahi kumuua Goliati kabla ya Daudi, hakuna aliyewahi kusimamisha jua kabla ya Joshua, hakuna aliyewahi kutabiria mifupa na ikawa hai kabla ya Ezekiel. Hakuna aliyewahi kurusha ndege kabla ya the Wringht brothers (kwanza mara ya kwanza iliruka umbali wa futi 120 na kukaa angani kwa sekunde 12)!
Hii haina maana kwamba hakukuwa na watu wengine kabla yao, inawezekana wapo waliopata mawazo kama yao kabla lakini hawakuchukua hatua yoyote katika kuyafanyia kazi. Inawezekana hofu, kughairi mara kwa mara, kutokuzingatia vipaumbele na kila sababu walizokuwa nazo ndio viliwakwamisha na hivyo wamefukiwa na historia bila ya kutambua uwezo waliokuwa nao. Mwanariadha Usain Bolt amewahi kusema, “Anything is possible. I don’t think limits” (Kila kitu kinawezekana. Huwa sifikirii vikwazo: Tafsiri isiyo rasmi). Watu hawa wanatufundisha kuwa, hakuna mtu ataweza kutambua uwezo aliona nao au umbali unaoweza kwenda mpaka pale amechukua hatua.
Kumbuka, hautaweza kutambua uwezo wako katika kuimba mpaka umeimba, hautaweza kutambua uwezo wako katika kuongoza mpaka umechukua hatua na kuongoza, hautaweza kutambua uwezo wako katika kufanya kazi mpaka umeifanya hiyo kazi. Hautaweza kutambua /kujua umbali gani unaweza kwenda katika jambo lolote mpaka umeanza na hatua moja, iwe ni katika huduma, kazi, biashara n.k!
Wazo kuu tunalotaka ulipate siku ya leo ni kwamba; Ili kutambua uwezo wako na umbali unaoweza kwenda katika jambo lolote ni muhimu kuchukua hatua katika kufikia kilele cha uwezo [Abilities, gifts, talents] ambao Mungu ameweka ndani yako ili kuwafaidia wengine na kumpa yeye Utukufu.
“Vivyo hivyo nuru yenu na iangaze mbele ya watu, wapate kuyaona matendo yenu mema, wamtukuze Baba yenu aliye Mbinguni”
There’s a place for you at the top

0 comments :