Utajiri wetu katika Kristo Yesu

9:19:00 PM Unknown 0 Comments

UTAJIRI WETU KATIKA KRISTO YESU 
(Waefeso1:17-23)

Biblia imeweka wazi kwamba, watu wamjuao Mungu wao watatenda mambo makuu. Ufunguo wa maisha yenye ufanisi upo katika kupata maarifa, ufahamu na kujua hekima ya jinsi itupasavyo kuenenda ili kuishi maisha ya ushindi katika Kristo Yesu. Ili kuona na kuishi ushindi katika maisha yetu ya kila siku itategemea na kiwango cha maarifa na ufahamu wetu juu ya “siri” za ufalme wa Mungu. Hakuna njia ya mkato katika hilo. [Mithali 4:7-9]

Linda Maamuzi yako ...

8:24:00 PM Unknown 0 Comments

LINDA MAAMUZI YAKO, HASA WAKATI UNAPOKUTANA NA CHANGAMOTO
Je baada ya miaka mitano au kumi au baada ya muda kupita kutoka sasa, utajipongeza kwa uamuzi uliochukua au utajilaumu? Utafurahi na kushangilia au utajutia na kutamani kurudi nyuma ili kusahihisha uamuzi uliochukua? Kumbuka kila kitu kipo katika uweza wa mtu mwenyewe na anawajibika kwa matokeo yote ya uchaguzi na uamuzi wake.

Fikra huru kamwe hazifungwi

7:42:00 PM Unknown 0 Comments


FIKRA HURU KAMWE HAZIFUNGWI
Mwili waweza kufungwa lakini fikra huru kamwe hazifungwi. Huwezi kubaki jela kama tayari akili yako iko nje kwenye uhuru. Kuwa na fikra chanya na sahihi ni oparesheni (brain surgery) unayoweza kuifanya mwenyewe. Ili kuwa na fikra chanya hauhitaji kwenda hospitali ya Apollo nchini India au kule John Hopkins Marekani , unahitaji taarifa sahihi tu. Neno la Mungu ambalo ni Habari njema ndio taarifa sahihi. Neno la Mungu ni taa ya miguu yetu, hutupa hekima kuliko watu wa rika letu. 

Pasipo Msongo wa Mawazo II

6:38:00 PM Unknown 0 Comments



PASIPO MSONGO WA MAWAZO II
(STRESS FREE ZONE)
1.    Mpaka lini?
Wabeba maono wengi, watu wenye mipango ya muda mrefu na wenye shabaha za kipekee wanaweza kuwa wahanga wa swali hili. Hili huwakumba wengi ambao wanaona umri unakwenda, wanatamani wasimamishe saa ili watekeleze mpango kazi wao. Wana mipango na mawazo ya kiuchumi na kijamii ambayo wanashuhudia waziwazi  yakipishana na muda. Swali hili huua moyo wa Rick Warren anasema, “Hurry Kills Prayer.” sala na kutangaza maombolezo.