Mtu Jasiri

1:31:00 PM Unknown 0 Comments

MTU JASIRI
Katika ulimwengu wa sasa majasiri wengi hawajulikani. Dunia ya leo imewatukuza wasemaji ikaacha wakimya, imemdharau mtu mpole ikampa heshima mtu mkali. Katika vikao wasikilizaji wazuri hawatambuliwi kama majasiri wa kusema. Kusikiliza si jambo jepesi, hakuna mtu mgumu kumsikiliza kama mtu mkorofi na mtu asiyejua.
Si wengi wanauzoefu na uwezo wa kusikiliza kwa makini, wengi hupenda kusikilizwa si kusikiliza. Huwezi kusikiliza na huku unatazama televisheni au unasikiliza redio. Ni rahisi kuukusanya mwili lakini si akili ya usikivu. Huwezi kusikiliza ikiwa unataka kusema, unaweza kusikiliza ikiwa unataka kusikiliza. Alisema Winston Churchil, “Courage is not only what it takes to stand up and talk but courage is also what it takes to sit down and listen” kwa tafsiri “Inamhitaji mtu jasiri kusimama na kuzungumza, lakini inamhitaji mtu jasiri pia kukaa kimya na kusikiliza”.
Amenukuliwa mzee Kinana Katibu Mkuu CCM akisema, “kiongozi lazima asikilize wananchi”.  Kiongozi si lazima awe kwenye kampuni, kwenye taasisi ya umma au kwenye siasa, badala yake anaweza akawa kwenye familia baba wa familia, mama wa familia, kaka wa familia au dada wa familia.  Siku chache katika nafasi ya uongozi jambo kubwa nililojifunza ni kwamba, uongozi ni kusikiliza, It’s all about listening!
Ni raha kusikiliza, msikivu anaraha kwa kuwa anauelewa mpana. Je, ungependa kuitwa mwongeaji sana au msikivu sana. Je, ungependa mtu akitoka nyumbani kwako aseme hajawahi ona msemaji kama wewe au aseme hajawahi kukutana na mtu msikivu kama wewe.  Si vema mtu akushangae kwa kusema, “What a talker
Ni mtu jasiri peke yake anaweza kuwasikiliza waliotengwa, waliosetwa na wasio stahili katika jamii. Si rahisi kuwasikiliza wahalifu, mtu jasiri pekee anaweza kufanya hivyo.
Kwa kiongozi mpya wa nafasi na ngazi yoyote nasisitiza neno moja, sikiliza, sikiliza, sikiliza.
Tukutane kileleni wasikivu wanapopatikana.

0 comments :