Nyuma ya mafanikio ya kila mtu

2:45:00 PM Unknown 0 Comments

NYUMA YA MAFANIKIO YA KILA MTU
(THE SPIRIT BEHIND YOUR SUCCESS)
Ulimwengu usioonekana umekuwa ukitegemeza ulimwengu unao onekana. Ulimwengu wa roho unategemeza ulimwengu wa mwili, Ulimwengu wa roho unaamuru ‘dictate’ ulimwengu wa nyama. Tumezoea kusema nyuma ya mafanikio ya kila mwanaume  kuna mwanamke, hii si sahihi saana.
Ukweli ni kwamba nyuma ya kila mwanaume kuna roho, na si mwanaume tu bali ni nyuma ya kila mwanadamu kuna roho. Nyuma ya mafanikio ya Yusufu kulikuwa na Roho bora, Nyuma ya ustadi wa Daudi kulikuwa na Roho Mtakatifu.
Kila mwanadamu unayemwona, ni ama anapelekwa na Roho wa Bwana au roho wa shetani. Nyuma ya kazi yako kuna roho, nyuma ya Uhasibu wangu kuna roho pia. Kama alivyowahi kusema Mtumishi wa Mungu Nabii Makandiwa, “Hakuna dakika wala sekunde ambapo mwanadamu anaweza kwenda sehemu yoyote bila uongozi wa Roho wa Mungu au roho wa shetani”. Ni ama uko chini ya uongozi wa Roho wa Mungu au roho wa shetani. Warumi 8:14
Umewaona watu sokoni, kanisani, shuleni, au safarini? Ni ama wanaongozwa na Roho wa Mungu au roho ya shetani. Kila siku na kila saa chini ya uongozi wa Roho Mtakatifu, kinyume na hali hii ni uongozi wa Roho wa shetani.
Nyuma ya kila kiongozi kuna roho, matendo ya viongozi hudhihirisha roho wanazozitumikia, Namna pekee ya kujua roho/Roho unayemtumikia ni kwa kuchunguza matunda unayozaa. Matunda ya chuki, uasi, wizi, mgawanyiko, majanga, ukame, njaa, na vita hudhihirisha utawala fulani kiroho. Zamani Mungu alisema na watu wake kwa mvua, njaa, ukame na magonjwa, hata sasa mambo haya huzungumza kitu kutoka ulimwengu wa Roho.
Zingatia haya;
  1. Nyuma ya mafaniko ya kila mwanadamu kuna roho.
  2. Ulimwengu wa roho unatawala ulimwengu tunaoishi na kutembea ndani yake.
  3. Mwanadamu hawezi kuishi bila nguvu ya rohoni.
Tukutane ijumaa, shalom.

0 comments :

USHINDI UPO NDANI YAKO, SIO NJE

9:30:00 AM Unknown 0 Comments


 

USHINDI UPO NDANI YAKO, SIO NJE!

Nimewahi kumsikia mtu akisema kwamba, Ikiwa watu elfu watasema unaweza lakini wewe ukajiambia nafsini mwako na kuamini kuwa hauwezi, kufanikisha jambo fulani au kufanikiwa katika eneo fulani la kimaisha; uwezekano wa wewe kuja kufanikiwa katika eneo hilo ni mdogo sana sawa na hakuna. Na ikiwa watu elfu watasema hauwezi lakini wewe ukasema nafsini mwako na kuamini kuwa utafanikiwa, basi mafanikio huwa dhahiri baada ya muda tu.
Ni ukweli usiopingika kwamba, ikiwa mtu ataona ushindi ndani yake ni rahisi kuona ushindi katika maisha ya kila siku; na ikiwa mtu hataona ushindi ndani yake basi uwezekano wa kuona ushindi nje ni nadra sana sawa na hakuna. Na hapa ndipo panapo tofautisha kati ya mshindi na mshindwa, aliyefanikiwa na aliyeshindwa, anayesonga mbele na anayekwama.
“Maana aonavyo nafsini mwake, ndivyo alivyo” Mithali 23:7
Jambo kuu tunalotaka upate hapa ni kwamba, kama kuna mahali au eneo unataka kuona ushindi katika maisha yako basi utambue kuwa ushindi upo ndani yako sio nje, yaani ushindi huanzia ndani yako. Hauwezi kushinda nje kama haujaweza kushinda ndani yako kwanza. Kumbe hatuwezi kuona badiliko lolote la kudumu kiuchumi au kifedha au kihuduma endapo ndani yetu hatuoni wala kuamini kama tunaweza kufanikiwa na kupata badiliko hilo. You must feel and see it before you realize it.
Njia kuu moja wapo ya kukuwezesha kuona ushindi ndani yako katika eneo fulani la kimaisha ili kuupata ushindi huo nje ni kusikia, kile unacho ruhusu [kusikika] ndani yako ndicho hupata nafasi katika maisha yako. Sauti [maneno] unayoisikiliza au uliyoipa ruhusa ndani yako ndio huamua hatima yako. Hauwezi kujidhihirisha kama samba endapo ndani unajiona kama swala. Ukiona ushindi utaongea kama mshindi, utatembea kama mshindi; ukiona kushindwa hauwezi kuwa na ujasiri na kuongea kama mshindi.
Unapoona ushindi ndani yako, na ukakutana na changamoto akili hupata nguvu ya ziada na kuanza kutafuta namna ya kuondoa au kutumia changamoto hiyo ili kufikia ushindi, lakini kama ndani huoni ushindi, umekata tama akili ‘inaparararizi’ na inakosa nguvu ya kufikiri namna ya kuondoa au kutumia changamoto, hata changamoto ndogo akili huona mlima mkubwa. Na hapa ndipo panapo tofautisha katika ya mshindi na mshindwa, aliyefanikiwa na aliyeshindwa, anayesonga mbele na anayekwama. Ndani ya moyo wako unaona nini? Unachoona ni muhimu sana, kwa sababu kinaweza kukukwamisha au kukufanikisha.
There’s a place for you at the top

0 comments :

Ubongo hauna rangi

7:37:00 PM Unknown 0 Comments

  
UBONGO HAUNA RANGI
(Brain has no colour)
Hakuna utofauti wa akili kati ya bara moja na lingine, hakuna utofauti katika kuumbwa kwa Mzungu na Mwafrika, sote tu sura na mfano wa Mungu. Hakuna tofauti kati ya watu wa magharibi na watu wa kusini. Kila mtu anaweza kuwa atakavyo, na anaweza mambo yote. Kila mwasisi wa Taifa ana nafasi ya kulifanya taifa lake kuwa nambari moja kwa maendeleo.
Ulipopewa rangi nyeusi ya mwili si kwamba umepewa ubongo mweusi. Ubongo hauna rangi, mtu mweusi hana ubongo mweusi, wala mtu mweupe hana ubongo mweupe, ubongo ni ubongo tu. Ukikuta ubongo mweusi basi ni wewe mwenyewe umeupaka rangi nyeusi. Wakati Wright Brothers wanavumbua urushaji wa ndege wengine wanarogana. Wakati mmoja anaun’garisha ubongo wake kwa kusoma kitabu kizuri mwingine anatazama picha za ngono na hivyo anauchafua zaidi. Sote tumefanya hayo lakini leo makala hii ni simu ya kukuamsha, Brain has no colour!
Ben Carson, Usain Bolt, Hayati Dr Myles Munroe ni miongoni mwa wachache walioihakikishia dunia kwamba, wana ngozi nyeusi lakini hawana ubongo mweusi. Hofu, mashaka, kutokujiamini, uchoyo, ubinafsi, uchafu, uchawi, ulevi, ulafi, uasherati na vingine vingi huchafua ubongo na kufanya uwe na rangi nyeusi. Ili uhakikishe hili, chunguza na utagundua jamii nyingi zenye mambo ya kishirikina ziko nyuma kielimu, na familia za kuhusudu ulevi huwa hazisongi mbele.
Kwa asili mwanadamu anazaliwa akiwa na ubongo wenye kumpa akili ya kutenda mambo yote, kuweza kila kitu kwa wakati. Yale yasiyofaa ambayo mwanadamu huona na kusikia huendelea kumharibu na kufanya awe na hofu, kujidharau, kujiwekea mipaka ya kiutendaji. Wafilipi 4:13
Usimfundishe mwanao kuwatukuza wazungu, bali mwambie ana ubongo sawa na wao na anaweza kufanya zaidi ya wao. Darasa moja, mwalimu mmoja na shule moja lakini matokeo ya watoto huwa tofauti kwa sababu ya vizuizi tunavyowawekea. Mwingine anaambiwa anga ndio kuzuizi chake mwingine anaambiwa ajira, ukiajiriwa tu inatosha mwanangu! Huna wa kuajiriwa hawezi jihusisha na tafiti za kurusha vyombo kwenda mwezini au kupasua vichwa vya watu, hii ni kwa sababu upatikanaji wa ajira ni rahisi na hivyo kufikiri kwenda mwezini au kuwa daktari bingwa ni kama kupoteza muda.
Tatizo lolote ikiwamo la ajira, kabla halijawa la Serikali ni la wazazi wa mtoto, baadaye ni la mtoto mwenyewe, na mwisho ni la nchi. Ubongo wetu unapakwa matope na mafuta machafu ya mawazo mgando ndio maana tunashindwa kufikiri kimkakati.
 Tunashindwa kupenya katika majadiliano yenye maslahi makubwa. Mawazo mabaya si kuzini na kuua watu tu, bali ni uoga. Tunaogopa kuanza, tunaogopa kugombea, tunaogopa kuamka mapema, tunaogopa kusafiri, tunaogopa kukopa, tunaogopa kuacha kazi, tunaogopa kusimamia mawazo yetu, tunaogopa kweda nchi za mbali. Ukienda uwanja wa Ndege utaona wanaoingia kwetu ni wengi kuliko wanaotoka, sisi tunaogopa wao wanakuja. Hawajui lugha yetu, wala hawajui asili yetu ila wanakuja kisha wanafanikiwa na wanaondoka. Jifunze kwa wachina waliojazana Kariakoo Dar es salaam.
Ubongo hauchakai kwa sababu unautumia sana, bali unachakaa kwa sababu hautumii akili. Ni kweli hukupata muda wa kwenda shule sawa, Je, hujapata hata muda wa kufikiri? Tofauti kati ya msomi na mtu ambaye hakusoma ipo kwenye kufikiri. Ukiweza kufikiri vizuri na kupanga kimkakati basi wewe ni msomi. Ni vijana wachache ambao hufikiri kimkakati yaani akapanda au akawekeza katika mradi utakao mlipa baada ya miaka hamsini.
Azimio la Arusha lilikuwa tunda la akili ya mwalimu Nyerere, Tuzo ya Nobel ni mtoto wa akili ya Mzee Alfered Nobel aliyesikia sifa zake mbaya na kubadilika. Afrika kusini huru ni mtoto wa akili wa Hayati Nelson Mandela, Microsoft Cooperation ni mtoto wa Bill Gate, TANU si ni mtoto wa Mwalimu Nyerere.
Je, akili yako imetuzalia nini cha maana? What is your brain child?
Wanaotumia akili zao vizuri hubuni, huanzisha na huvumbua. Huasisi mataifa, huanzisha viwanda na makampuni, huanzisha taasisi zao. Hawafi wakiwa wamelala kitandani, hufa wakiwa katika mapambano ya kukamilisha azma na wito wao.

0 comments :

UNATAKA KUFANIKIWA KATIKA NINI?- IV

10:10:00 PM Unknown 0 Comments

UNATAKA KUFANIKIWA KATIKA NINI?-IV
(Amua kuthubutu)
Mtu mmoja amewahi kusema, “Maisha hayatupi tunachokitaka, bali hutupa kile ambacho tupo tayari kukifanyia kazi”. Kile ambacho unatamani kitokee katika maisha yako au katika eneo lolote la maisha yako ni lazima uwe tayari kufanyia kazi ili kiwe halisi. Nioneshe mtu mwenye udhubutu katika yale anayoyatamani, nikuoneshe mtu mwenye matokeo katika maisha yake.
Kuhamasika (motivated) pekee katika jambo fulani hakutaleta matokeo katika maisha kama hakuna udhubutu wa kufanyia kazi jambo hilo. Wako wengi waliopita semina au kusikia mafanikio ya watu wengine, na wakahamasika kweli kufikia malengo waliyojiwekea lakini baada ya muda hakuna wanachoweza kuonesha kama matokeo ya kuhamasika kwao. Na hii ni kwa sababu walihamasika lakini hawakuchukua hatua ya kufanyia kazi matamanio yao.
Mwenyehekima mmoja amewahi kusema, baada ya mwaka kupita au mwezi au muda fulani, tutabaki tukijilaumu na kutamani kama tungedhubutu kuyafanya yale tuliyoyahairisha. Do it today or regret tomorrow. Kumbuka: hakuna jambo lolote lenye thamani ambalo huja kirahisi, ni matokeo ya kazi (nothing worth comes easy, it takes work).
Mtu mvivu husema,Simba yuko nje; nitauawa katika njia kuu” Mithali 22: 13
Adui mkubwa katika eneo la udhubutu ni visingizio; unaweza kuwa katika kundi la watu wanaoeleza kwa nini hawakuweza kufikia malengo yao, au ukawa katika kundi la wachache wanaoleza namna gani wameweza kufikia mafanikio yao katikati ya changamoto nyingi. Kumbuka, ulimwengu hautoi heshima kwa wanaoeleza kwanini haiwezekani, au kwanini hawakuweza au wanaoeleza namna ambavyo watu waliwakatisha tama walipotaka kuanza. Usijipe majibu ya kushindwa au kwamba haiwezekani kabla haujadhubutu. “Maisha hayatupi tunachokitaka, bali hutupa kile ambacho tupo tayari kukifanyia kazi”.

There’s a place for you at the top

0 comments :