Mungu ni mwakilishi wetu

11:58:00 AM Unknown 0 Comments

 
MUNGU NI MWAKILISHI WETU.
(Anajua kupigana vizuri kuliko sisi)
Tunaishi kwenye ulimwengu wenye changamoto nyingi, watu wanafukuzwa kazi, yatima wanadhulumiwa; wanafunzi wanafeli, wazazi wanagombana, wapenzi wanaachana na vikao vya kazi havimaliziki kwa usalama.
Yote haya yanamfanya mwanadamu ajitahidi kuyakabili bila ya Mungu. Kuna kitu kinamwambia mwanadamu apigane mwenyewe, kuna msukumo usiotaka kumruhusu Mungu apigane.
Kwa nini tunashindwa kumruhusu Mungu aingilie kati? Ni kwa sababu tunadhani tunajua kupigana kuliko Yeye au ni kwa sababu tunafikiri atasahau. Ukweli ni kwamba Mungu anajibu kwa wakati, yuko makini kuliko wahudumu wa chumba cha watu mahututi.
Siku moja usiku baada ya kuona nyumba yangu imezingirwa na mambo yasiyofaa niliamua kumwita BWANA YESU na dakika ile ile shwari ilirejea. Namshangaa Mungu kwa maana amewapa mamlaka kuu wale wanaompigania. Hudson Taylor akijua fika atakwenda nchi ya mbali kwa uinjilishaji, alijifunza kumtegemea Mungu kwa kila jambo. Hata alipotaka pesa hakumwambia mkuu wake wa kazi bali alimwambia Mungu katika maombi. Ananukuliwa, “ni vema nijifunze kumwomba Mungu kwa kila jambo, maana huko China niendeko hakuna mtu wa kumwomba wala kumtegemea”.
Katika biblia tunaona Mungu amekuwa sauti ya wasio na sauti, amewakumbuka matabaka ya walioonewa. Yeye ni Mungu wa vita, anajua kupigana tena ameshinda vita zote. Kuomba ni kumchagua Mungu awe mwakilishi wako katika vita. Ndio maana biblia imeyaita maombi silaha. Waefeso 6:11
Uwezo wa mwanadamu unakikomo, hata akijitahidi hawezi kutuliza yote yanayomsonga. Taarifa ya habari si taarifa yenye habari za kutia tumaini bali ni taarifa yenye habari mbaya; mafuriko, njaa, migomo, ugomvi, kupunguzwa kazini, vifo na magonjwa.
Nakumbuka siku moja nilipopokea taarifa ya kutisha kwamba mpendwa wangu yuko mbioni kufa. Niliogopa sana! Moyo wangu ulizimia kwa hofu. Siku yangu ilikwenda mrama kabisa. Mara ghafla jioni rafiki yangu akanishauri na kutumia Zaburi 46:1-3. Na hapo nikapata nguvu, na hapo nikapata upenyo na hapo nikasimama tena. Na hapa nikajua kama ni vita si mimi nitakaye kufa, bali ni wenzangu ndio watafia nchi zao na falme zao.
“Mungu kwetu sisi ni kimbilio na nguvu, Msaada utakaoonekana tele wakati wa mateso.
Kwa hiyo hatutaogopa ijapobadilika nchi, Ijapotetemeka milima moyoni mwa bahari.
Maji yake yajapovuma na kuumuka, Ijapopepesuka milima kwa kiburi chake.” Zaburi 46:1-3
Nikamkimbilia Mungu kwa sala, tukashinda vita na mpendwa wangu akawa salama! Tishio la kifo, ajali, hukumu ya Mahakama, Waganga, Wachawi halina uwezo wowote kwa yule ajuaye kuliitia jina la BWANA, yule aliyepaka damu ya Yesu ya Pasaka.
Kujiambatanisha na Mungu ni kujiambatanisha na ushindi. Kama wakristo sisi ni washindi, maana tu uzao wa ushindi.
Mkimbilie Mungu ukiwa na cheti cha daktari, mwambie utaishi kwa neno lake wala si kwa chakula, wala si kwa neno la daktari. Ingawa tunaheshimu mchango wa kila taaluma lakini Bwana ndiye atakaya maneno yote, kwa kuwa Yeye ni mwanzo tena mwisho. Hata kama umetenda dhambi usisite kumwendea Mungu wakati wa changamoto yako. Yeye ni kimbilio wakati wa shida, shida zinaturejesha kwake.

0 comments :

Ili kufikia malengo yako

2:10:00 PM Unknown 0 Comments

 
ILI KUFIKIA MALENGO YAKO
Kila mwaka mpya unapoanza watu wengi huwa na kawaida ya kujiwekea malengo katika mwaka husika. Karibu kila mtu au mahali huzungumia mipango au malengo anayotamani na kujipangia; Lengo ni kupata taswira ya mahali ambapo mtu anataka kwenda au kufanikisha katika mwaka huo. Hili ni jambo zuri kwa kuwa linaleta hamasa, nguvu na matumaini ya kusonga mbele katika maisha ya kila siku; kwa kuwa kama mtu hajui anapotaka kwenda (hana malengo au mipango) njia yoyote itamfikisha.
Changamoto moja ambayo hutokea ni kwamba watu wengi huwa na hamasa kubwa juu ya kuweka na kutamani kutimiza malengo yao mwanzoni mwa mwaka; lakini kadiri muda unavyozidi kwenda hamasa na nguvu ya kuyaendea malengo waliojiwekea hupungua au hutoweka kabisa. Na hivyo wanapofika mwisho wa mwaka wanagundua kuwa hawana kitu cha kuonesha au wanakitu kidogo tu ukilinganisha na malengo waliokuwa nayo wakati wanaanza mwaka.
Jambo hili tunaweza kuliona hata kwa wanaisraeli walipokuwa wanatolewa katika utumwa na kupelekwa katika nchi yao ya ahadi. Wakati wanatoka walikuwa na hamasa kubwa na nguvu na matumaini ya kufikia nchi ya ahadi; lakini kwa kadiri walivyokuwa wanaendelea na safari hamasa, matumaini na nguvu ya kufikia ahadi iliyokuwa mbele yao ilikuwa ikipungua kwa baadhi yao. Ukitizama safari yao utagundua kuwa kilichofanya hamasa na matumaini yao kupungua kadiri walivyosonga mbele, ni kitendo cha wao kuacha kuangalia (Paying attention) Ahadi na kuanza kuangalia changamoto walizokuwa wanakutana nazo njiani.
Je unapokutana changamoto katika mipango uliojiwekea katika mwaka huu, unachagua kuangalia nini? Unaangalia changamoto au unaangalia malengo yako? Ukitumia muda mwingi kutafakari changamoto uwe na uhakika hamasa na nguvu hupungua na hatimaye huweza kutoweka kabisa. Lakini ukitumia muda wako kutafakari malengo yako na kutafuta namna ya kufanikisha (Mfano; Kutafuta maarifa zaidi kwa kusoma vitabu au kurudi shule tena, kutenga muda mwingi zaidi wa kufanyia kazi jambo hilo, kutafuta ushauri, kujifunza kwa waliokutangulia/ waliofanikiwa, kurudia tena uliposhindwa mara ya kwanza n.k) uwe na uhakika mwisho wa mwaka au muda uliojiwekea  utakuwa na kitu cha kuonesha na sio maneno matupu ya kwanini ulishindwa.
Katika kufikia malengo au mipango uliojiwekea mwanzoni mwa mwaka au mwezi au kipindi chochote kile changamoto hutokea au naweza kusema haziepukiki kwa namna moja au nyingine. Changamoto ndizo zinatufanya tushangilie na kuwa na moyo wa shukrani pale ambapo tumefikia malengo hayo. Kumbuka jambo hili: Kama ni rahisi (hakuna changamoto) kila mtu angefanya. Changamoto haziji ili kufisha ahadi yako, bali zinakupa fursa ya kuona Ukuu na Utukufu wa Mungu kwa namna ambayo hujawahi kuona. Ni changamoto ya wanaisraeli ndio iliyofanya tutambue Mungu anaweza kufanya njia mahali pasipo na njia. Mtu hapewi tuzo kwa kusimulia namna changamoto zilivyomkwamisha; hupewa tuzo kwa kuonesha namna gani ameweza kufikia malengo yake katikati ya changamoto.
There’s a place for you at the top!

0 comments :

Kipaji chako ni hiki hapa

1:34:00 PM Unknown 0 Comments

 
KIPAJI CHAKO NI HIKI HAPA
(Katika taabu ni rahisi kujua kipaji chako halisi)
Nani ni nani Tanzania, Kuna watu wanafuatana na utambulisho wao, Mchango wao na karama zao zimewatambulisha. Who is who in Tanzania? Sheikh Shaaban Robert amejulikana kwa mashairi, Askofu Moses Kulola amejulikana kwa injili, Rose Mhando amejulikana kwa nyimbo za injili. Wewe unautambulisho gani?
What is your Identity? Tunaposhindwa kujua utambulisho wetu kupitia karama na makusudi ya kuumbwa kwetu tunapoteza maana ya kuishi. Na hapa siku tukiimba vizuri tutafikiri sisi ni waimbaji na siku tukifundisha vizuri tutafikiri sisi ni walimu. Tatizo hili limewasumbua wengi na limekuwa likijulikana kama, The Crisis of Identity, ni hali ya kutokujua utambulisho wetu na mchango wetu kwa jamii.
Ukitaka kukosa mshindi katika mchezo wa mpira wa miguu usimpige refa bali ondoa magoli na hivyo kutakuwa hakuna sehemu ya kufunga na tayari mpira utapoteza ladha. Kingine unachoweza kufanya ni kuweka nguzo nyingi za magoli (yaani badala ya mbili weka nne). Malengo mengi maishani ni usumbufu. Kuwa na malengo mengi hakukupi nafasi ya kuwa mshindi ndio maana kila timu hufunga katika goli moja tu. Maisha bila ya kuwa na lengo kuu la kufanikisha hayana ladha. Ndio maana ni muhimu kujua kusudi lako na kipaji chako. 
Kipaji halisi hujidhihirisha wakati wa taabu, wakati ambao uko peke yako bila ya ulio wazoea. Unachopenda kufanya gizani bila ya kuhimizwa na mtu kinaweza kuwa kipaji chako nuruni. Kipaji cha ubondia hugunduliwa nje ya ulingo na ulingoni ni sehemu ya udhihirisho tu.
Yusufu alitabiri Gerezani, Paulo na Sila waliimba na kumsifu Bwana wakiwa gerezani mpaka milango ya Gereza ikafunguka. Je! kipaji chako kinadhihirika wakati wa shida? Kipaji halisi hakinyamazishwi na mazingira magumu.
Kipaji au karama ya Mungu huonekana hata katika taabu, Yesu aliendelea kuhubiri, kuponya na kuokoa hata akiwa msalabani. Don’t be silenced by problems
Nimeona Mungu akiponya kwa uponyaji mkuu katika mazingira ambayo sikuwa hata na utayari. Siku chache zilizopita tumeshuhudia Boss mkubwa aliyeachishwa kazi TANESCO akiendelea na kuhubiri injili. Kawaida ya kipaji halisi ni nyenzo inayotumika hata katika taabu, kamwe hainyamazi. Umri haunyamazishi kipaji chako, ana miaka 82 ya kuzaliwa bado Jimmy Swaggart anaimba, kupiga kinanda vizuri na kufundisha.
Wako wakimbizi waliotumia vipaji vyao ugenini, wako watumwa waliotawala utumwani. Wako wafanyakazi wa ndani walioishia kuwa wafalme. Ni baada ya kugundua vipaji vyao na kuvitumia hata katika mazingira magumu. Endelea kutumia kipaji chako usikate tamaa.
Mazingira magumu yanapaswa kukuhamasisha kutumia kipaji chako na si kukitelekeza kipaji chako. Kwa tafsiri yangu Paulo alimaanisha hivi, “…chochea kipaji ulichopewa na Mungu kilicho ndani yako.” 2 Tim1:6
Kileleni ndipo tunapopatikana

0 comments :