Weekend of purpose ya kesho

8:59:00 AM Unknown 0 Comments

 
WEEKEND OF PURPOSE YA KESHO
(Ni Jumamosi ya kesho 13/05/2017 kuanzia saa tatu asubuhi)
Ni zaidi ya miaka miwili sasa tangu Mungu atupe wazo la kufanya , “Weekend Of Purpose” wazo hili tulilipata kwa BWANA. Nyakati hizo baada ya kumaliza Chuo kikuu tulikuwa tunakutana Tegeta siku za weekend kwa ajili ya kubadilishana mawazo, kusali, na kutiana moyo katika harakati za muda huo na baadaye. Siku moja katika kuomba kwetu ndipo BWANA alipotusemesha kuhusu jambo hili nasi tukalitenda.
Tukaanza kuandaa “Weekend Of Purpose” ya msimu wa kwanza na hatimaye kesho itakuwa ya tano. Ni siku mbili ambazo Bwana Alituambia tuwafundishe watu makusudi ya kuumbwa kwao, kwamba anawajua na amewaumba kwa kusudi maalumu. Kazi yetu ni kukufanya ujue kusudi la kuumbwa kwako na kukukumbusha umuhimu wa kulitenda na kukupa mbinu za kulifanikisha pia. Yeremia 1:5
Siku ya mwisho, wako watakaojuta kwa nini hawakufanya hili na lile, na wako watakaofuraha na kusema, I am so glad I did! Raha ya kifo cha mtu wa Mungu ni kutimiza kusudi. Kifo cha mtu wa Mungu kinamfurahisha Mungu maana ni usingizi wa amani baada ya kazi. Ni faida kuu, kuishi kusudi uliloitiwa na BWANA. Kifo ni kitamu kazi yako ikiisha vizuri, kinyume na hapo ni janga. Zaburi 116:15
Tunazo shuhuda za waliohudhuria Weekend Of Purpose ya kwanza na baada ya kujua kusudi la kuumbwa kwao, waliacha yale yasiyo ya kwao na leo hii wanafuraha kwa sababu wanatumikia kile ambacho Mungu alitaka wafanye.
Jaribu kufikiri kama Petro angeendelea kuvua samaki milele, angetoa hesabu gani mbele za Mungu; ambaye kwa hakika hakumweka awe mvuvi wa samaki, bali awe mhubiri wa injili. Utajisikiaje siku hiyo Yesu akikwambia nilikuumba uwe nahodha wa meli ilhali wewe umeishi maisha yako yote kama daktari wa meno. Ni kazi yetu katika Weekend Of Purpose kukusaidia kujua karama na makusudi ya kuumbwa kwako. Mafundisho yatakusaidia umalize vizuri sana, Zaburi 116:15
Katika “Weekend Of Purpose” utajengwa kitabia kama mwenye hekima mmoja alivyosema, “iweni watakatifu kwanza ndipo muwe wamisionari” neno hili ni kwa kila kada, iweni watakatifu kwanza ndipo muwe madereva, iweni watakatifu kwanza ndipo muwe wahandisi, iweni watakatifu kwanza ndipo muwe wagavi. Utajengwa ili tabia yako ifanane na kazi yako na kusudi uliloitiwa. Mhasibu ukionekane katika taswira ya fundi makenika (fundi wa magari) akiwa gereji bila shaka utaambiwa rudi nyumbani kavae ki-hasibu. Tabia ni matendo na mazoea yanayohusu matamshi, mavazi, matendo na mwenendo wote.
Karibu sana kesho Jumamosi saa tatu, ukifika Mawasiliano au Makumbusho panda magari yaliyoandikwa Bunju/Tegeta au Bagamoyo shuka kituo kinaitwa CHAMA KWA MASISTA- pale BOKO, vuka barabara, elekea upande huo wa kuume wa kanisani mpaka utakapoona geti la Masista wa Karmeli ambalo liko mbele baada ya kumaliza uzio wa kanisa utakuwa umefika.
Hautajutia kufika ni faida tupu, tukutane hapo. Mungu akubariki.

0 comments :