Kanunu ya Mazingira

3:53:00 PM Unknown 0 Comments


KANUNI YA MAZINGIRA
(Vigezo lazima vikamilike)

Ili mbegu iweze kuota ni lazima vigezo vinavyohusika vikamilike. Uoteshaji wa mbegu hauhitaji maombi tena haufanyiki kwa mafungo bali kwa kutimiza vigezo vinavyotakiwa katika kanuni ya mazingira. Ili mbegu ikue inahitaji yafuatayo: maji, mwanga, joto na hewa. Mambo haya yakitimia hata kama mkulima ni mweusi mbegu itaota na hata kama ni mweupe mbegu itaota. Ukitii na kutimiza vigezo mafanikio ni lazima.

Kuna watu ili wafanikiwe wanahitaji mazingira ya kanisani, wengine mazingira ya biashara wengine mazingira ya shuleni na wengine viwandani. Yule wa kanisani hawezi kuwika sokoni halikadhalika wa sokoni hawezi kuwika kanisani. Ni muhimu kila mtu ajue mazingira yanayobeba kipaji chake. Mito na bahari ndiyo inayobeba kipaji cha samaki cha kuogelea.

Unadhani mazingira gani yanaweza kubeba kipaji chako? Je, ni katika mazingira gani watu wanauona uwepo wako?  Je, ni katika tasnia gani unapata utoshelevu wa mahitaji yako? Ni katika mazingira gani Mungu anatukuzwa kwa ajili yako na wewe unatakaswa?

Nimewahi kusoma makala moja isemayo, tasnia ya filamu imeajiri watu wengi nchini Nigeria kuliko mafuta. Ingawa Nigeria wanasifika kwa kutoa mafuta lakini ni mazingira ya filamu ndiyo yamewaajiri watu wengi zaidi. Ni bora kupingwa na watu wengi katika mazingira sahihi kuliko kukubaliwa na watu wote katika mazingira ambayo si sahihi kwa ukuaji na ustawi wako.

Bora upinzani wa jinamizi la usiku kuliko ule wa mazingira yaani, unaamka mapema kwenda kufanya kitu usichopenda. Unawahi kuamka kwende katika mazingira usiyoyataka. Kama umeitwa katika mazingira ya michezo basi siasa haikufai. Ni raha sana mtu anapokuwa katika mazingira sahihi, Christiano Ronaldo anasema yuko tayari kucheza soka hata bila ya kulipwa. Anaupenda mpira wa miguu, yuko radhi kucheza bure mpira ni maisha yake. Usain Bolt angeendelea kung’ang’ana na mpira wa miguu huenda asingekuwa chochote, lakini utii wake kwa kanuni ya mazingira ulimpeleka kwenye riadha ambapo anashikilia rekodi ya dunia.

Mwenye hekima mmoja amewahi kusema: “There are no bad people there are misplaced people”.  Hakuna watu wabaya ila kuna watu ambao wapo katika mazingira ambayo si sahihi kwao. Mazingira mabaya si yale yasiyo na pesa bali ni yale ambayo hayakusaidii kufikia ndoto zako na kuwa unachotaka kuwa. Mazingira yanapaswa kukubeba kwa sababu kwa asili mtu hawezi kubeba mazingira. Kuyabeba mazingira ni kazi ngumu. Ndio maana

Rai yangu kwako leo ni kukusihi utii kanuni ya mazingira na kwenda kwenye eneo lako husika. Wahubiri wengi wamekuwa na simulizi za kuacha kazi na kwenda kwenye wito wao, jambo hilo si mtindo bali ni kanunu ya msingi ya mazingira.

Nenda shule, nenda kwenye biashara, nenda kanisani, nenda kwenye huduma, nenda kwa watoto, nenda kwa yatima nenda kwa watu ambao umeitiwa. Wengine wameitwa katika mazingira ya ujasiliamali wengine wameitwa katika mazingira ya uongozi. Sote tunapaswa kuyatafuta mazingira yetu na kuyatii. Petro alicha mazingira ya baharini [uvuvi] na akaenda katika mazingira yenye watu wengi [kwenye uinjilishaji na utumishi] huko akafanikiwa sana.

Tii mazingira yako, ipende kanuni ya mazingira….

0 comments :