Kuelekea Uhuru wa Kifedha - II

2:33:00 PM Unknown 0 Comments

 
KUELEKEA UHURU WA KIFEDHA II
(THE BIBLICAL LAWS OF MONEY)
Toleo lililopita tuliangazia kanuni moja muhimu sana ili kuelekea mafanikio ya kiuchumi katika maisha ya mtu; kanuni ya uzalishaji bidhaa au huduma. Kanuni hii huwa haimzungumziwi sana lakini ni kanuni muhimu sana kuelekea uhuru wa kifedha. Kumbuka, Fedha unazozitafuta zipo kwa watu, ili kuzipata lazima uwe na kitu cha kubadillishana (exchange). Hakuna namna utafikia uhuru wa kifedha endapo hakuna bidhaa wala huduma ambayo unaweza kutoa na watu wakakupa fedha.
Kwa mtu ambaye ameajiriwa maana yake anauza huduma, na hivyo mwisho analipwa mshahara. Mshahara unakuja kama matokeo baada ya kutoa huduma, vivyo hivyo mfanyabiashara au mjasiriamali au hata makampuni hupata fedha kutokana na bidhaa au huduma wanayozalisha.  Fedha ni matokeo ya bidhaa au huduma anayotoa mtu. Mwalimu wangu mmoja amewahi kusema, “If you don’t create or add value to others (through goods or service), you are not entitled to receive money” (Kama hauna bidhaa au huduma unayoweza kutoa kwa watu, haustahili kupokea fedha ya mtu: Tafsiri isiyo rasmi)
Mtu pekee anayeweza kuwa na uhakika wa kupata fedha bila kubadilishana na huduma au bidhaa moja kwa moja ni serikali, yenyewe inakusanya kodi. Hivyo watu watake au wasitake ni lazima serikali ikusanye fedha kutoka kwao kama kodi kwa mujibu wa sheria za nchi husika. Mimi na wewe hatukusanyi kodi, watu hawalazimiki kisheria kutupa fedha zao; hivyo basi ili kupata fedha zao lazima tuwe na kitu wanachokiitaji na kwa sababu hiyo wako tayari kukilipia ili kukipata kitu hicho. Na hapo ndipo tunapoweza kuona fedha inaingia mifukoni mwetu.
Swali unaloweza kujiuliza au unalotakiwa kujiuliza sasa, ni bidhaa gani au huduma gani unaweza kuizalisha au kutoa ambayo watu (jamii inayokuzunguka) wanahaja nayo na watakuwa tayari kuilipia ili kuipata? Iwe umeajiriwa au hujaajiriwa hili ni swali muhimu sana kama unataka kufikia uhuru wa kifedha (kutimiza mahitaji yako YOTE, na kupata ziada kwa ajili ya kufikia mahitaji mengine yanayokuzunguka; maana utamsaidiaje anayehitaji ‘chakula’ wakati hata wewe huna: Mathayo 25:37-40).
Sam Adeyemi amewahi kusema  It is not the absence of money that makes a person poor; it’s the absence of right idea (thought) that has value”. Yaani “Si ukosefu wa fedha ndio humfanya mtu kuwa masikini bali ukosefu wa wazo lenye thamani”. Hivyo kumbe fedha ni matokeo tu; yaani matokeo  ya wazo lenye thamani ambalo huzaa bidhaa au huduma; ambazo mtu hubadilishana (exchange) na fedha.
There’s a place for you at the top!

0 comments :